Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 50

Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2

Unaweza Kufanya Nini Juu Familia Yako Ikuwe na Furaha?​—Sehemu ya 2

Watoto ni zawadi yenye Yehova amepatia wazazi. Na Yehova anapenda wazazi wawachunge muzuri. Yehova anapatia wazazi mashauri ya kuwasaidia kufanya vile. Yehova anaonyesha pia mambo yenye watoto wanaweza kufanya juu familia ikuwe na furaha.

1. Yehova anapatia wazazi mashauri gani?

Yehova anaomba wazazi wapende watoto wao na wajikaze kupitisha wakati mingi pamoja nao. Na tena, anapenda wazazi walinde watoto wao na watumie kanuni za Biblia juu ya kuwafundisha. (Mezali 1:8) Anaambia hivi baba: “Muendelee kuwalea [watoto wenu] katika . . . maonyo ya Yehova.” (Soma Waefeso 6:4.) Yehova anafurahi kama wazazi wanafuata mashauri yake wakati wako nakomalisha watoto wao, na kama hawaachie mutu mwingine daraka ya kukomalisha watoto wao.

2. Yehova anapatia watoto mashauri gani?

Yehova anashauria hivi watoto: “Mutii wazazi wenu.” (Soma Wakolosai 3:20.) Wakati watoto wanaheshimia na kutii wazazi wao, Yehova anafurahi na wazazi pia wanafurahi. (Mezali 23:22-25) Wakati Yesu alikuwa mutoto, alitii na kuheshimia wazazi wake hata kama alikuwa mukamilifu. Ile ni mufano muzuri yenye aliachia watoto.​—Luka 2:51, 52.

3. Munaweza kufanya nini juu familia yenu ikuwe na urafiki muzuri pamoja na Yehova?

Kama uko muzazi, ni wazi kama unapenda watoto wamupende Yehova sawa vile weye unamupenda. Unaweza kufanya nini juu ya kuwasaidia? Biblia inakuambia hivi: “Unapaswa kuyakazia [maneno ya Yehova] katika wana wako na kuongea kuyahusu wakati unakaa katika nyumba yako na wakati unatembea katika barabara.” (Kumbukumbu la Torati 6:7) ‘Kukazia’ maana yake kufundisha jambo fulani kwa kuirudilia-rudilia. Inawezekana unajua kama mara mingi inakuombaka urudilie-rudilie jambo fulani juu mutoto wako aikumbuke. Ile andiko nayo inapenda kusema kama unapaswa kuwa nazungumuza na watoto wako juu ya Yehova mara kwa mara. Ni muzuri mupange wakati ya kujifunza Biblia pamoja kila juma. Kama hamuna watoto, na nyie mutapata faida kama munapanga wakati ya kujifunza Biblia pamoja kila juma.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mashauri yenye inaweza kusaidia watu wote mu familia wakuwe na furaha na wajisikie kuwa salama.

4. Fundisha watoto wako kwa upendo

Haikuwake mwepesi kufundisha watoto. Namna gani Biblia inaweza kusaidia? Musome Yakobo 1:19, 20, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Namna gani wazazi wanaweza kuonyesha upendo wakati wako nazungumuza na watoto wao?

  • Juu ya nini muzazi hapaswe kupatia watoto nizamu wakati iko na kasirani? a

5. Linda watoto wako

Juu ya kulinda watoto wako, ni jambo ya maana sana uzungumuze nao juu ya ngono. Inaweza kuwa nguvu kufanya vile. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini haikuwake mwepesi kwa wazazi fulani kuzungumuza na watoto juu ya ngono?

  • Wazazi fulani wametumia njia gani juu wazungumuze na watoto wao juu ya ngono?

Biblia ilisemaka kama ulimwengu wa Shetani utaendelea kuharibika zaidi na zaidi, na ni vile mambo iko. Musome 2 Timoteo 3:1, 13, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Watu fulani waovu wenye mustari wa 13 unazungumuzia, wanatendeaka watoto mubaya kingono. Njo maana, ni jambo ya maana wazazi wafundishe watoto wao juu ya ngono na namna wanaweza kujilinda juu wale watu wasiwatendee mubaya.

Unajua?

Mashahidi wa Yehova wametoa vichapo mingi ili kusaidia watu waweze kufundisha watoto wao juu ya ngono na kuwalinda wasitendewe mubaya kingono. Kwa mufano, ona:

6. Heshimia wazazi wako

Namna watoto wanazungumuza na wazazi wao inaweza kuonyesha kama wanawaheshimia ao hapana. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini ni jambo ya maana mutoto azungumuze na wazazi wake kwa heshima?

  • Namna gani mutoto anaweza kuzungumuza na wazazi wake kwa heshima?

Musome Mezali 1:8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mutoto anapaswa kutenda namna gani wakati wazazi wake wanamuambia mambo ya kufanya?

7. Mumuabudu Yehova pamoja mu familia

Familia za Mashahidi wa Yehova zinapangaka wakati ya kumuabudu Yehova pamoja mu familia kila juma. Munaweza kufanya nini mu ibada ya familia? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Familia inaweza kufanya nini juu ikuwe nafanya ibada ya familia kila juma?

  • Muzazi anaweza kufanya nini juu ibada ya familia isaidie na kufurahisha kila mutu mu familia?​—Ona picha ku mwanzo wa hii somo.

  • Ni mambo gani inaweza kufanya ikuwe nguvu kujifunza pamoja mu familia?

Mu Israeli ya zamani, Yehova aliambiaka familia zikuwe na zoezi ya kuzungumuzia maandiko. Musome Kumbukumbu la Torati 6:6, 7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani unaweza kutumikisha hii kanuni?

Mambo fulani ya kufanya mu ibada ya familia:

WATU FULANI WANASEMAKA: “Biblia iko nguvu sana, watoto hawawezi kuielewa.”

  • Na weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Yehova anapenda wazazi wapende watoto wao, wawafundishe, na kuwalinda; anapenda watoto waheshimie na kutii wazazi wao; na anapenda familia zimuabudu pamoja.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wazazi wanaweza kufanya nini juu ya kufundisha na kulinda watoto wao?

  • Watoto wanaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama wanaheshimia wazazi wao?

  • Kumuabudu Yehova pamoja mu familia kila juma, iko na faida?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ni mambo gani inaweza kusaidia mutoto wako akuwe mutu muzuri wakati atakuwa mutu muzima?

“Somo Sita Zenye Watoto Wanapaswa Kujifunza” (Amuka! Na. 2 2019)

Ona mashauri yenye inaweza kusaidia wale wenye wako nachunga wazazi wao wenye wamezeeka.

“Biblia Inasema Nini Juu ya Kuchunga Wazazi Wenye Kuzeeka?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna mwanaume mwenye hakukuwa najua namna ya kukomalisha watoto, alifikia kuwa baba muzuri.

Yehova Ametufundisha Namna ya Kukomalisha Watoto Yetu (5:58)

Ona mambo yenye baba wanaweza kufanya juu wakuwe na urafiki muzuri pamoja na watoto wao wanaume.

“Baba Wanaweza Kufanya Nini Juu Wakuwe Marafiki wa Sana wa Watoto Wao Wanaume?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 11, 2011)

a Mu Biblia, “nizamu” inamaanisha kufundisha mutoto, kumuongoza, na kumusaidia abadilishe mawazo ao tabia ya mubaya. Haimaanishe hata kidogo kumutendea mubaya ao bila huruma.​—Mezali 4:1.