Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 51

Useme Maneno Yenye Inamufurahisha Yehova

Useme Maneno Yenye Inamufurahisha Yehova

Wakati Yehova alituumba, alitupatia zawadi ya muzuri sana: uwezo wa kusema. Namna tunatumia uwezo wetu wa kusema inaweza kumufurahisha ao kumuhuzunisha? Ndiyo! (Soma Yakobo 1:26.) Sasa, tunaweza kufanya nini juu tutumie uwezo wetu wa kusema mu njia yenye itamufurahisha?

1. Namna gani tunapaswa kutumia uwezo wetu wa kusema?

Biblia inatuambia hivi: “Muendelee kutiana moyo na kujengana.” (1 Watesalonike 5:11) Unajua mutu fulani mwenye iko na lazima ya kutiwa moyo? Unaweza kufanya nini juu ya kumusaidia ajisikie muzuri? Umuambie kama unamuonaka kuwa mutu wa maana. Pengine unaweza kumuambia sifa zake zenye unafurahiaka. Kuko andiko fulani ya Biblia yenye inaweza kutia moyo mutu fulani mwenye unajua? Kuko maandiko mingi sana. Tena, ukumbuke kama maneno yako na namna unaisema, inaweza kufanya mutu ajisikie muzuri ao hapana. Njo maana ni muzuri ukuwe nazungumuza kwa upendo na kwa upole kila siku.​—Mezali 15:1.

2. Tunapaswa kuepuka maneno ya namna gani?

Biblia inasema hivi: “Neno lenye kuoza lisitoke katika kinywa chenu.” (Soma Waefeso 4:29.) Ni kusema, hatupaswe kusema maneno machafu, maneno makali ao ya kukosa adabu, yenye inaweza kuumiza mutu. Tunapaswa pia kuepuka kusema wengine mubaya na kuwasemea mambo ya uongo.​—Soma Mezali 16:28.

3. Nini njo itatusaidia tukuwe nasema maneno ya kutia moyo?

Mara mingi, mambo yenye tunasemaka, inaonyeshaka mambo yenye iko mu moyo wetu na mu akili yetu. (Luka 6:45) Njo maana tunapaswa kuwa na zoezi ya kufikiria sana mambo ya muzuri, ni kusema, mambo ya haki, yenye kuwa safi, yenye kustahili kupendwa, na yenye kusemwa muzuri. (Wafilipi 4:8) Na juu tukuwe nafikiria ile mambo ya muzuri, tunapaswa kuchagula mambo ya kujifurahisha ya muzuri na marafiki wazuri. (Mezali 13:20) Tena ni muzuri tukuwe nawaza mbele ya kusema. Unaweza kujiuliza hivi: Kama ninasema hivi, wengine watajisikia namna gani? Biblia inasema hivi: “Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga, lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.”​—Mezali 12:18.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye unapaswa kufanya juu maneno yako ikuwe namufurahisha Yehova na kutia wengine moyo.

4. Fikiria mambo yenye utasema, utaisema wakati gani, na namna gani

Wakati fulani, tunasemaka mambo kisha tunajiuliza juu ya nini tuliisema. (Yakobo 3:2) Musome Wagalatia 5:22, 23, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unaweza kuomba Yehova akusaidie kukomalisha sifa gani kati ya zile sifa juu ukuwe nasema mu namna yenye inamufurahisha? Zile sifa zinaweza kukusaidia namna gani?

Musome 1 Wakorinto 15:33, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Marafiki na pia mambo yenye unajifurahishaka nayo inaweza kuwa na matokeo gani juu ya namna yako ya kusema?

Musome Muhubiri 3:1, 7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Ni wakati gani inaomba kunyamaza na kungoya wakati yenye inafaa juu ya kusema jambo fulani?

5.Useme mambo ya muzuri juu ya wengine

Namna gani tunaweza kuepuka kuumiza wengine ao kusema mambo ya mubaya? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, juu ya nini ule ndugu alipenda kubadilisha namna yake ya kuzungumuza juu ya wengine?

  • Alifanya nini juu abadilike?

Musome Muhubiri 7:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunataka kusema mambo ya mubaya juu ya mutu fulani?

Musome Muhubiri 7:21, 22, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani ile andiko inaweza kukusaidia usikasirike wakati mutu anasema mambo ya mubaya juu yako?

6. Uzungumuze na watu wa familia yako kwa upendo

Yehova anapenda tuzungumuze na watu wa familia yetu kwa upole na kwa upendo. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Nini njo itakusaidia ukuwe nazungumuza na watu wa familia yako kwa upendo?

Musome Waefeso 4:31, 32, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Ni maneno ya namna gani njo inafanyaka watu mu familia wajisikie muzuri?

Yehova alisema waziwazi kama anamupenda Mwana wake, Yesu. Musome Matayo 17:5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani unaweza kufuata mufano wa Yehova wakati uko nazungumuza na watu wa familia yako?

Ukuwe na zoezi ya kupongeza wengine

WATU FULANI WANASEMAKA: “Miye ninasemaka mambo yenye inanikuya mu kichwa. Hata wengine wanielewe mubaya, sihangaike.”

  • Unawaza ni muzuri vile? Juu ya nini unasema vile?

KWA KIFUPI

Mambo yenye tunasema, inaweza kusaidia wengine ao kuwaumiza. Njo maana tunapaswa kufikiria mambo yenye tutasema, tutaisema wakati gani, na namna gani.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Namna gani unaweza kutumia uwezo wako wa kusema juu ya kusaidia wengine?

  • Unapenda kuepuka maneno ya namna gani?

  • Nini njo itatusaidia tukuwe nazungumuza kwa upole na kwa upendo?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Nini njo inaweza kutusaidia tukuwe na maneno ya kutia moyo?

Ukuwe na Ulimi wa Wenye Hekima (8:04)

Ona mambo yenye inaweza kukusaidia uepuke kusema mubaya.

“Ni Mubaya Kabisa Kutukana?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna unaweza kuepuka tabia ya kusema wengine mubaya.

Namna Gani Naweza Kuacha Kusema Wengine Mubaya? (2:36)