Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 53

Uchagule Mambo ya Kujifurahisha Yenye Yehova Anakubali

Uchagule Mambo ya Kujifurahisha Yenye Yehova Anakubali

Yehova ni “Mungu mwenye furaha.” (1 Timoteo 1:11) Anapenda na siye tukuwe na furaha na tufurahie maisha. Anafurahi wakati tunatia kwanza kazi pembeni juu tujifurahishe kidogo. Mu hii somo, tutaona namna tunaweza kujifurahisha mu namna ya muzuri na yenye Yehova anakubali.

1. Tunapaswa kukumbuka nini wakati tunachagula mambo ya kujifurahisha?

Unapendaka kujifurahisha na mambo gani? Watu fulani wanapendaka tu kubakia ku nyumba na kusoma kitabu, kusikiliza muziki, kuangalia filme, ao kutafuta habari ku Enternete. Wengine wanapendaka kujifurahisha na marafiki wao; wanaendaka kutembelea fasi fulani, kuogelea, kucheza muchezo fulani na mambo ingine. Kila mutu iko na mambo yenye anapendaka kujifurahisha nayo. Lakini, kila mutu anapaswa kuhakikisha kama ile mambo ‘inakubaliwa kwa Bwana.’ (Waefeso 5:10) Ni jambo ya maana kuelewa ile juu mu mambo mingi yenye watu wanajifurahishaka nayo leo, munayala mambo yenye Yehova anachukia, sawa vile mambo ya kuuana na kupigana, uasherati, ao uchawi. (Soma Zaburi 11:5.) Nini njo itatusaidia tuchagule muzuri mambo ya kujifurahisha?

Kama tunachagula marafiki wenye wanamupenda Yehova, wanaweza kutuchochea tufanye mambo ya muzuri na kutusaidia tuchagule muzuri mambo ya kujifurahisha. Sawa vile tulijifunza mu somo fulani yenye kutangulia, “mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima.” Lakini, mwenye anazoea kupitisha wakati na watu wenye hawapende sheria za Mungu “ataumia.”​—Mezali 13:20.

2. Juu ya nini ni muzuri tufikirie wakati yenye tunapitishaka mu mambo ya kujifurahisha?

Hata kama tunachagula mambo ya muzuri ya kujifurahisha, tunapaswa kuwa waangalifu juu ile mambo isitukamate wakati mingi. Kama tunapitisha wakati mingi mu mambo ya kujifurahisha, tunaweza kukosa wakati ya kufanya mambo ingine ya maana sana. Biblia inatuambia ‘tutumie muzuri zaidi wakati [yetu].’​—Soma Waefeso 5:15, 16.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna tunaweza kuchagula muzuri mambo ya kujifurahisha.

3. Epuka mambo ya kujifurahisha yenye haifae

Juu ya nini tunapaswa kuchagula muzuri mambo ya kujifurahisha? Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Ni mambo gani yenye ilikuwa mu michezo ya Waroma wa zamani yenye inakuwaka mu mambo ya kujifurahisha ya leo?

  • Vile uliona mu video, Danny alifikia kutambua nini juu ya mambo ya kujifurahisha?

Musome Waroma 12:9, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani hii andiko inaweza kukusaidia uchagule muzuri mambo ya kujifurahisha?

Yehova anachukia mambo gani? Musome Mezali 6:16, 17 na Wagalatia 5:19-21. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Ile andiko inataya mambo gani yenye inaonekanaka sana mu mambo ya kujifurahisha ya leo?

 Maulizo ya kukusaidia uchagule muzuri mambo ya kujifurahisha

Ujiulize hivi:

  • Mambo gani? Mu mambo yenye ninajifurahishaka nayo, muko mambo yenye Yehova anachukia?

  • Wakati gani? Mambo ya kujifurahisha inanikamataka wakati ya kufanya mambo ya maana zaidi?

  • Na nani? Mambo ya kujifurahisha inafanyaka nipitishe wakati mingi na watu wenye hawamupendi Yehova?

Inakuwaka muzuri zaidi mutu asikaribie hata kidogo hatari. Njo maana ni muzuri tuepuke kabisa mambo ya kujifurahisha yenye tuko nayo mashaka

4. Tumia wakati yako muzuri

Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Hata kama ndugu mwenye kuonyeshwa mu video hakukuwa naangalia mambo ya mubaya, shida yake ilikuwa nini?

Musome Wafilipi 1:10, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani hii andiko inaweza kutusaidia tufikirie wakati yenye tunapitishaka mu mambo ya kujifurahisha?

5. Chagula mambo ya muzuri ya kujifurahisha

Hata kama Yehova hakubali mambo fulani ya kujifurahisha, kuko mambo mingi ya kujifurahisha yenye anakubali. Musome Muhubiri 8:15 na Wafilipi 4:8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Unapendaka kujifurahisha na mambo gani ya muzuri?

Kuko mambo mingi ya muzuri yenye unaweza kufanya juu ya kujifurahisha

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kujifurahisha na mambo yenye iko ndani uasherati, uchawi, ao mambo ya kupigana na kuuana, haiko mubaya juu sitafanya ile mambo.”

  • Weye unawaza nini?

KWA KIFUPI

Yehova anapenda tuchagule na tufurahie mambo ya muzuri ya kujifurahisha.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Wakristo wanapaswa kuepuka mambo gani ya kujifurahisha?

  • Juu ya nini tunapaswa kufikiria wakati wenye tunapitisha mu mambo ya kujifurahisha?

  • Juu ya nini unapenda kuchagula mambo ya kujifurahisha yenye Yehova anakubali?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna kila mutu iko na daraka ya kujichagulia mambo ya kujifurahisha.

“Mashahidi wa Yehova Wanakatazaka Filme, Vitabu, ao Nyimbo Fulani?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna unaweza kuchagula muzuri mambo ya kujifurahisha.

“Unajifurahishaka na Mambo Yenye Inafaa?” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 10, 2011)

Mu habari “Nilifikia Kuachana na Ubaguzi,” ona juu ya nini mwanaume fulani alijifunza kuchagula muzuri mambo ya kujifurahisha.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 2, 2010)

Ona namna mama fulani anakamata uamuzi muzuri kuhusu mambo ya kujifurahisha yenye inaonyesha mambo ya uchawi.

Epuka Mambo ya Kujifurahisha Yenye Inaonyesha Mambo ya Uchawi (2:02)