SOMO LA 53

Chagua Burudani Inayomfurahisha Yehova

Chagua Burudani Inayomfurahisha Yehova

Yehova ni “Mungu mwenye furaha.” (1 Timotheo 1:11) Anataka tuwe na furaha na tufurahie maisha. Anafurahi tunapotenga muda ili kujifurahisha. Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia wakati wetu wa kupumzika katika njia inayofurahisha na yenye kuridhisha, na wakati uleule inayomfurahisha Yehova.

1. Tunapaswa kukumbuka nini tunapochagua burudani?

Unapenda kufanya nini unapopumzika? Baadhi ya watu wanapenda kupumzika nyumbani wakisoma kitabu, kusikiliza muziki, kutazama sinema, au kutumia Intaneti. Wengine hufurahia kutumia wakati pamoja na marafiki wakipanda milima, kuogelea, au kucheza michezo mbalimbali. Lolote lile tunalochagua kufanya, tunapaswa kuhakikisha kwamba tunachagua burudani ‘inayokubalika kwa Bwana.’ (Waefeso 5:10) Ni muhimu kuchagua burudani inayofaa kwa sababu burudani nyingi zinazopendwa leo zinahusisha mambo ambayo Yehova anachukia kama vile ukatili, ukosefu wa maadili katika ngono, au kuwasiliana na roho waovu. (Soma Zaburi 11:5.) Ni nini ambacho kitatusaidia kuchagua burudani kwa hekima?

Ikiwa tutachagua marafiki wanaompenda Yehova, wanaweza kutujenga na kutusaidia kuchagua burudani inayofaa. Kama tulivyojifunza katika Somo la 48, mtu “anayetembea na wenye hekima atakuwa na hekima.” Kinyume chake, tunaposhirikiana kwa ukawaida na watu wasiopenda viwango vya Mungu ‘tutaumia.’​—Methali 13:20.

2. Kwa nini hatupaswi kutumia muda mwingi katika burudani?

Hata ikiwa burudani tunazochagua zinafaa, tunapaswa kuwa makini tusitumie muda mwingi sana. Kwa sababu huenda tukakosa muda wa kutosha kufanya mambo yaliyo muhimu zaidi. Biblia inatuhimiza ‘tutumie vizuri kabisa wakati wetu.’​—Soma Waefeso 5:15, 16.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi ya kufanya maamuzi mazuri kuhusu burudani.

3. Epuka burudani zisizofaa

Kwa nini tunapaswa kuwa makini tunapochagua burudani? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Michezo ya kale ya Waroma inafanana jinsi gani na baadhi ya burudani za leo?

  • Katika video hiyo, Danny alijifunza nini kuhusu burudani?

Soma Waroma 12:9, kisha mzungumzie swali hili:

  • Mstari huu unawezaje kukusaidia kuchagua burudani inayofaa?

Ni baadhi ya mambo gani ambayo Yehova anachukia? Soma Methali 6:16, 17 na Wagalatia 5:19-21. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

  • Ni mambo gani yaliyotajwa katika mistari hii ambayo ni ya kawaida katika burudani za leo?

 Jinsi ya kuchagua burudani kwa hekima

Jiulize hivi:

  • Nini? Je, burudani hii inahusisha jambo lolote ambalo Yehova anachukia?

  • Lini? Je, burudani hii itachukua muda wa mambo yaliyo muhimu zaidi?

  • Nani? Je, burudani hii itafanya nishirikiane kwa ukaribu au kwa ukawaida na watu ambao hawampendi Yehova?

Ili tuwe salama, tunapaswa kukaa mbali kabisa na hatari. Hivyo, tunapaswa kuepuka burudani yoyote tunayohisi kwamba haifai

4. Tumia muda wako kwa hekima

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Ingawa ndugu katika video hiyo hakuwa akitazama jambo lisilofaa, tatizo lilikuwa wapi?

Soma Wafilipi 1:10, kisha mzungumzie swali hili:

  • Mstari huu unaweza kutusaidiaje kuamua muda tutakaotumia katika burudani?

5. Chagua burudani zinazofaa

Ingawa baadhi ya burudani hazimfurahishi Yehova, kuna mambo mengi sana yanayofaa tunayoweza kufanya ili kujifurahisha. Soma Mhubiri 8:15 na Wafilipi 4:8, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unapenda kufurahia burudani gani?

Unaweza kufurahia burudani zinazofaa

WATU FULANI HUSEMA: “Hakuna ubaya wa kufurahia burudani zenye ukatili, ukosefu wa maadili, au kuwasiliana na roho waovu ikiwa sifanyi mambo hayo.”

  • Wewe ungesemaje?

MUHTASARI

Yehova anataka tuchague na kufurahia burudani zinazofaa.

Ungejibuje?

  • Wakristo wanapaswa kuepuka burudani za aina gani?

  • Kwa nini tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu muda tunaotumia katika burudani?

  • Kwa nini unapaswa kuchagua burudani zinazomfurahisha Yehova?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyoweza kufanya maamuzi mazuri kuhusu burudani.

“Je, Tafrija Unayochagua Inakujenga?” (Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 2011)

Katika simulizi “Nilishinda Chuki Niliyokuwa Nayo,” ona sababu iliyofanya mwanamume fulani abadili burudani aliyopenda.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 2010)

Ona jinsi mama fulani anavyofanya uamuzi wa hekima kuhusu burudani zinazohusisha hadithi za ulimwengu wa roho waovu.

Epuka Burudani Zenye Mazoea ya Kuwasiliana na Roho (2:02)