Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 54

Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”

Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”

Yesu ndiye Kichwa cha kutaniko la Kikristo. (Waefeso 5:23) Leo, Yesu akiwa mbinguni anaongoza wafuasi wake duniani kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Soma Mathayo 24:45.) Kwa kuwa aliwekwa rasmi na Yesu, “mtumwa” huyo ana mamlaka kwa kadiri fulani, lakini bado anaendelea kuwa mtumwa wa Kristo na kuwatumikia ndugu za Kristo. Mtumwa huyo ni nani? Naye anatutunza jinsi gani?

1. “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ni nani?

Sikuzote, Yehova ametumia mwanamume fulani au kikundi kidogo cha wanaume kuwaongoza watu wake. (Malaki 2:7; Waebrania 1:1) Baada ya kifo cha Yesu, mitume na wazee huko Yerusalemu ndio walioongoza. (Matendo 15:2) Kwa kufuata kielelezo hicho, leo kikundi kidogo cha wazee, yaani, Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, huandaa chakula cha kiroho na kuelekeza kazi ya kuhubiri. Kikundi hicho ni “mtumwa mwaminifu na mwenye busara ambaye [Yesu] alimweka rasmi.” (Mathayo 24:45a) Washiriki wote wa Baraza Linaloongoza ni Wakristo watiwa-mafuta. Baada ya uhai wao kufikia mwisho hapa duniani, wana tumaini la kutawala pamoja na Kristo katika Ufalme wake mbinguni.

2. Mtumwa mwaminifu anaandaa chakula gani cha kiroho?

Yesu alisema kwamba mtumwa mwaminifu ‘angewapa Wakristo wenzake chakula chao kwa wakati unaofaa.’ (Mathayo 24:45b) Kama vile chakula cha kimwili kinavyotusaidia kuendelea kuwa na nguvu na afya, chakula cha kiroho, yaani, mwongozo kutoka katika Neno la Mungu, hutupatia nguvu tunazohitaji ili kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova na kutimiza kazi ambayo Yesu ametupatia. (1 Timotheo 4:6) Tunapata chakula hicho cha kiroho kupitia mikutano, makusanyiko ya mzunguko na ya eneo, na pia kupitia machapisho na video zinazotegemea Biblia ambazo hutusaidia kuelewa mapenzi ya Mungu na kuimarisha urafiki wetu naye.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kwa nini tunahitaji “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” yaani, Baraza Linaloongoza.

Baraza Linaloongoza huandaa chakula cha kiroho, mwongozo, na msaada hususa kwa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote

3. Watu wa Yehova wanapaswa kupangwa kwa utaratibu

Chini ya mwongozo wa Yesu, Baraza Linaloongoza hupanga kazi ya Mashahidi wa Yehova. Kulikuwa na mpango kama huo katika kutaniko la Kikristo la karne ya kwanza. Onyesha VIDEO.

Soma 1 Wakorintho 14:33, 40, kisha mzungumzie swali hili:

  • Mistari hii inaonyeshaje kwamba Yehova anataka Mashahidi wake wawe na utaratibu?

4. Mtumwa mwaminifu hupanga kazi yetu ya kuhubiri

Kazi ya kuhubiri ndiyo kazi muhimu zaidi ambayo Wakristo wa karne ya kwanza walifanya. Soma Matendo 8:14, 25, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kati ya Wakristo wa karne ya kwanza, ni nani walioelekeza kazi ya kuhubiri?

  • Petro na Yohana waliitikiaje mwongozo kutoka kwa mitume wenzao?

Kazi ya kuhubiri ndiyo kazi muhimu zaidi inayopangwa na Baraza Linaloongoza. Onyesha VIDEO.

Yesu alikazia umuhimu wa kazi ya kuhubiri. Soma Marko 13:10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini Baraza Linaloongoza linaona kazi ya kuhubiri kuwa kazi muhimu sana?

  • Kwa nini tunahitaji “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” ili kupanga kazi hii inayofanywa ulimwenguni pote?

5. Mtumwa mwaminifu huandaa mwongozo

Baraza Linaloongoza huandaa mwongozo kwa Wakristo ulimwenguni pote. Wanaamuaje mwongozo unaofaa kutolewa? Chunguza jinsi baraza linaloongoza la Wakristo wa karne ya kwanza lilivyofanya hivyo. Soma Matendo 15:1, 2, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni suala gani lililosababisha kutoelewana kati ya Wakristo wa karne ya kwanza?

  • Paulo, Barnaba, na wengine walitafuta wapi mwongozo ili kutatua suala hilo?

Soma Matendo 15:12-18, 23-29, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kabla ya kufanya uamuzi fulani, baraza linaloongoza lilichunguza nini ili kupata mwongozo wa Mungu kuhusiana na jambo hilo?​—Ona mstari wa 12, 15, na 28.

Soma Matendo 15:30, 31 na 16:4, 5, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Wakristo wa karne ya kwanza waliitikiaje mwongozo uliotolewa na baraza linaloongoza?

  • Yehova aliwabariki jinsi gani walipotii mwongozo huo?

Soma 2 Timotheo 3:16 na Yakobo 1:5, kisha mzungumzie swali hili:

  • Baraza Linaloongoza hutafuta wapi mwongozo ili kufanya maamuzi leo?

WATU FULANI HUSEMA: “Ukisikiliza Baraza Linaloongoza, unawafuata wanadamu.”

  • Ni nini kinachokuthibitishia kwamba Yesu anaelekeza Baraza Linaloongoza?

MUHTASARI

Baraza Linaloongoza ndiye “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” aliyewekwa rasmi na Kristo. Wanatoa mwongozo na kuandaa chakula cha kiroho kwa Wakristo duniani pote.

Ungejibuje?

  • Ni nani aliyemweka rasmi “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”?

  • Baraza Linaloongoza hututunza jinsi gani?

  • Je, unaamini kwamba Baraza Linaloongoza ndiye “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi Baraza Linaloongoza lilivyopangwa ili kufanya kazi yake.

“Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova Ni Nini?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Jifunze jinsi Baraza Linaloongoza linavyohakikisha kwamba tunapokea chakula cha kiroho kinachofaa.

Kutokeza Machapisho Sahihi (17:18)

Washiriki wa Baraza Linaloongoza wanahisije kuhusu kazi ambayo Yesu amewapa?

Pendeleo la Pekee (7:04)

Mikutano na makusanyiko yetu yanathibitishaje kwamba Yehova anaelekeza Baraza Linaloongoza?

Yehova Anawafundisha Watu Wake (9:39)