Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 54

“Mutumwa Muaminifu na Mwenye Busara” Anafanyaka Nini?

“Mutumwa Muaminifu na Mwenye Busara” Anafanyaka Nini?

Yesu njo Kichwa cha kutaniko ya Kikristo. (Waefeso 5:23) Iko mbinguni, lakini iko natumia “mutumwa muaminifu na mwenye busara” ili kuongoza wanafunzi wake hapa ku dunia. (Soma Matayo 24:45.) Yesu njo aliweka ule “mutumwa” na alimupatia mamlaka ya kukamata maamuzi fulani. Hata vile, ule mutumwa anapaswa kuendelea kumutii Kristo na kutumikia ndugu za Kristo. Ule mutumwa ni nani? Na anatuhangaikiaka namna gani?

1. “Mutumwa muaminifu na mwenye busara” ni nani?

Tangu zamani, Yehova anatumiaka mwanaume ao kikundi ya wanaume juu ya kuongoza watu wake. (Malaki 2:7; Waebrania 1:1) Kisha Yesu kufa, mitume na wazee katika Yerusalemu njo walikuwa naongoza. (Matendo 15:2) Vilevile leo, kikundi kidogo ya wazee njo iko naongoza. Ile kikundi inaitwa Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova. Ile kikundi njo inapatiaka watu wa Mungu chakula ya kiroho na kuongoza kazi ya kuhubiri. Ile kikundi njo “mutumwa muaminifu na mwenye busara mwenye [Yesu] ameweka.” (Matayo 24:45a) Ndugu wote wa Baraza Yenye Kuongoza ni Wakristo watiwa-mafuta. Wako na tumaini ya kutawala mbinguni pamoja na Yesu wakati maisha yao ku dunia itafikia mwisho.

2. Mutumwa muaminifu anatupatiaka chakula gani ya kiroho?

Yesu alisema kama mutumwa muaminifu atakuwa ‘anapatia [Wakristo wenzake] chakula chao kwa wakati wenye kufaa.’ (Matayo 24:45b) Chakula inatusaidiaka tukuwe na nguvu na afya ya muzuri. Vilevile, chakula ya kiroho, ni kusema mafundisho ya Neno ya Mungu, inatupatiaka nguvu ya kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova, na kufanya kazi yenye Yesu alitupatia. (1 Timoteo 4:6) Tunapataka ile chakula ya kiroho ku mikutano, ku mikusanyiko, mu vichapo na video. Ile yote inatusaidiaka tuelewe mambo yenye Mungu anapenda na tukuwe marafiki wake wa sana.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini tuko na lazima ya “mutumwa muaminifu na mwenye busara,” ni kusema Baraza Yenye Kuongoza.

Baraza Yenye Kuongoza inapatiaka Mashahidi wa Yehova wa mu dunia yote chakula ya kiroho, muongozo, na musaada

3. Watu wa Yehova wanapaswa kupangwa muzuri

Yesu anatumia Baraza Yenye Kuongoza juu ya kupanga kazi ya Mashahidi wa Yehova. Hata zamani, Yesu alitumiaka baraza yenye kuongoza juu ya kuongoza Wakristo wa kwanza-kwanza. Muangalie VIDEO.

Musome 1 Wakorinto 14:33, 40, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Ile andiko inasema mambo gani yenye inaonyesha kama Yehova anapenda watu wake wapangwe muzuri?

4. Mutumwa muaminifu anaongoza kazi ya kuhubiri

Kazi ya maana sana yenye Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa wanafanya, ilikuwa kazi ya kuhubiri. Musome Matendo 8:14, 25, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Wakati ya mitume, nani njo walikuwa naongoza kazi ya kuhubiri?

  • Petro na Yohana walifanya nini wakati mitume wenzao waliwatolea muongozo?

Kuhubiri njo kazi ya maana sana yenye Baraza Yenye Kuongoza inasimamia. Muangalie VIDEO.

Yesu alionyesha kama kazi ya kuhubiri ni ya maana sana. Musome Marko 13:10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini Baraza Yenye Kuongoza inaona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana sana?

  • Juu ya nini tuko na lazima ya “mutumwa muaminifu na mwenye busara” juu asimamie kazi ya kuhubiri mu dunia yote?

5. Mutumwa muaminifu anatupatiaka muongozo

Baraza Yenye Kuongoza inapatiaka Wakristo wa mu dunia yote muongozo. Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanafanyaka nini juu wafikie kuamua muongozo wenye inafaa kutupatia? Tuone namna baraza yenye kuongoza ya wakati ya mitume ilikuwa nafanya. Musome Matendo 15:1, 2, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nini njo ililetaka ubishi kati ya Wakristo fulani wa kwanza-kwanza?

  • Paulo, Barnaba, na wengine walitafutaka muongozo wa nani juu ya kumaliza ile ubishi?

Musome Matendo 15:12-18, 23-29, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Mbele baraza yenye kuongoza ya wakati wa mitume ikamate uamuzi, ilifanyaka nini juu ya kujua mawazo ya Mungu juu ya ile jambo?​—Ona mustari wa 12, 15, na 28.

Musome Matendo 15:30, 31 na 16:4, 5, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Wakristo wa kwanza-kwanza walifanyaka nini wakati baraza yenye kuongoza iliwapatiaka muongozo?

  • Yehova aliwabariki namna gani juu walitii?

Musome 2 Timoteo 3:16 na Yakobo 1:5, na kisha muzungumuzie hii ulizo::

  • Mbele Baraza Yenye Kuongoza ya leo ikamate maamuzi, inafanyaka nini?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza ni wanadamu tu, kuwasikiliza ni kufuata wanadamu.”

  • Nini njo inakuhakikishia kama Yesu iko naongoza Baraza Yenye Kuongoza?

KWA KIFUPI

Baraza yenye Kuongoza njo “mutumwa muaminifu na mwenye busara” mwenye Yesu aliweka. Inapatiaka Wakristo wa mu dunia yote muongozo na chakula ya kiroho.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Nani njo aliweka “mutumwa muaminifu na mwenye busara”?

  • Namna gani Baraza Yenye Kuongoza inatuhangaikiaka?

  • Unaamini kama Baraza Yenye Kuongoza njo “mutumwa muaminifu na mwenye busara”?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Baraza Yenye Kuongoza imepangwa juu iweze kufanya kazi yake.

“Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova Ni Nini” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna Baraza Yenye Kuongoza inajikazaka sana juu tupate mafundisho yenye haina makosa.

Kutayarisha Vichapo Vyenye Havina Makosa (17:18)

Ndugu wa Baraza Yenye Kuongoza wanaonaka namna gani kazi yenye Yesu amewapatia?

Ni Pendeleo Kubwa Sana (7:04)

Namna gani mikutano na mikusanyiko yetu inaonyesha kama Yehova iko naongoza Baraza Yenye Kuongoza?

Yehova Iko Anafundisha Watu Wake (9:39)