Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 57

Unapaswa Kufanya Nini Kama Unaangukia mu Zambi Nzito?

Unapaswa Kufanya Nini Kama Unaangukia mu Zambi Nzito?

Hata kama unamupenda Yehova sana na unajikazaka sana juu usifanye jambo fulani yenye inaweza kumuumiza, wakati fulani utafanya makosa. Lakini, zambi fulani ziko nzito kuliko zingine. (1 Wakorinto 6:9, 10) Kama unafanya zambi nzito, ukumbuke kama Yehova angali anakupenda; iko tayari kukusamehe na kukusaidia.

1. Tunapaswa kufanya nini juu Yehova atusamehe?

Watu wenye wanamupenda Yehova wanahuzunikaka sana wakati wanatambua kama wamefanya zambi nzito. Lakini, hii maneno ya Yehova inawapatiaka nguvu: “Hata kama zambi zenu ziko na rangi nyekundu yenye kungaa, zitafanywa kuwa nyeupe kama teluji.” (Isaya 1:18) Kama tunatubu kwa moyo wote, Yehova atatusamehe kabisa. Tunapaswa kufanya nini ili kuonyesha kama tunatubu? Tunapaswa kuhuzunikia sana mambo yenye tulifanya, kuacha kufanya ile mambo, na kumulilia Yehova atusamehe. Kisha tunapaswa kujikaza kubadilisha mawazo ao tabia za mubaya zenye zilifanya tuangukie mu ile zambi. Na tunapaswa kutumikisha kanuni za Yehova mu maisha yetu.​—Soma Isaya 55:6, 7.

2. Kama tunaangukia mu zambi nzito, wazee wanafanyaka nini juu ya kutusaidia?

Kama tunafanya zambi nzito, Yehova anatuambia ‘tuite wazee wa kutaniko.’ (Soma Yakobo 5:14, 15.) Wale wazee wanamupenda Yehova na wanapenda watu wake. Wamefundishwa namna wanaweza kutusaidia juu tukuwe tena na urafiki muzuri na Yehova.​—Wagalatia 6:1.

Wazee wanaweza kufanya nini juu ya kutusaidia kama tunaangukia mu zambi nzito? Wazee wawili ao watatu watatumia mashauri yenye iko mu Biblia juu ya kuturekebisha. Na watatuambia mambo yenye tunaweza kufanya juu tuepuke kuangukia tena mu zambi. Wanaweza kuamua tuache kwanza kufanya mambo fulani mu kutaniko kwa wakati fulani, mupaka wakati urafiki wetu na Yehova utakuwa tena muzuri. Kama mutu anafanya zambi nzito lakini hatubu, wazee watamutenga juu asichochee wengine mu kutaniko kufanya mambo ya mubaya.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna Yehova anatusaidiaka kama tunafanya zambi nzito.

3. Kutubu kunatusaidiaka tukuwe tena na urafiki muzuri na Yehova

Kila zambi yenye tunafanya inaumizaka Yehova. Njo maana tunapaswa kutubu kwake. Musome Zaburi 32:1-5, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini hatupaswe kuficha zambi zetu, lakini tunapaswa kutubu zambi zetu kwa Yehova?

Kisha kutubu zambi zetu kwa Yehova, tutajisikia muzuri zaidi kama tunaomba wazee watusaidie. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, wazee walifanya nini juu ya kumusaidia Canon amurudilie Yehova?

Tunapaswa kuambia wazee mambo yote waziwazi, bila kuwaficha kitu. Wako pale juu ya kutusaidia. Musome Yakobo 5:16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini ni mwepesi kwa wazee kutusaidia kama tunawaambia mambo waziwazi?

Tubu zambi yako, usifiche wazee kitu, na ukubali musaada wa Yehova wenye upendo

4. Kuko faida wakati mutu anatengwa na kutaniko

Kama mutu mwenye alifanya zambi nzito anakatala kufuata kanuni za Yehova, hawezi kubakia mu kutaniko. Anatengwa, na hatuwezi tena kupitisha wakati pamoja naye, ao hata kumusemesha. Musome 1 Wakorinto 5:6, 11 na 2 Yohana 9-11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Sawa vile chachu inachachishaka donge lote, kupitisha wakati na mutenda-zambi mwenye hapendi kutubu, kunaweza kuwa na matokeo gani juu ya ndugu na dada mu kutaniko?

Watu wengi wenye walitengwa walifikia kumurudilia Yehova. Juu ya nini? Juu hata kama kutengwa inaumizaka sana, inasaidiaka mutu atambue makosa yake. (Zaburi 141:5) Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, namna gani kutengwa na kutaniko kulisaidia Sonja?

Wakati mutu anatengwa na kutaniko, juu ya nini ile . . .

  • inatukuza jina ya Yehova?

  • inaonyesha kama Yehova iko na usawaziko na iko na upendo?

5. Yehova anatusamehe wakati tunatubu

Yesu alitumia mufano fulani juu ya kutusaidia kuelewa namna Yehova anajisikiaka wakati mutu anatubu. Musome Luka 15:1-7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Hii habari inakufundisha nini juu ya Yehova?

Musome Ezekieli 33:11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Tunapaswa kufanya nini juu ya kuonyesha kama tumetubu kabisa?

Sawa vile muchungaji, Yehova anahangaikiaka sana kondoo wake

WATU FULANI WANASEMAKA: “Niko naogopa kuambia wazee zambi yenye nilifanya juu wasinitenge.”

  • Kama mutu iko na ile mawazo, utamuambia nini?

KWA KIFUPI

Kama tunafanya zambi nzito, lakini tunatubu kabisa na kuacha kufanya mambo ya mubaya, Yehova atatusamehe.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini tunapaswa kutubu zambi zetu kwa Yehova?

  • Tunapaswa kufanya nini juu Yehova atusamehe?

  • Kama tunafanya zambi nzito, juu ya nini tunapaswa kuomba wazee watusaidie?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna Yehova alionyesha mwanaume fulani rehema yenye kuzungumuziwa mu Isaya 1:18.

Usikuwe na Mashaka Juu ya Rehema ya Yehova Hata Kidogo (5:02)

Wakati mutu anatengwa na kutaniko, namna gani ile inamusaidia yeye na pia kutaniko?

“Sababu Gani Kutengwa na Kutaniko Ni Mupango Wenye Upendo?” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 4, 2015)

Ona namna unaweza kufasiria mutu mwenye haiko Shahidi juu ya nini wakati fulani watu wanatengwaka na kutaniko.

“Je, Mashahidi wa Yehova Wanakataa Wale Waliokuwa Katika Dini Yao Zamani?” (Inapatikana ku Enternete)

Mu habari “Nilipaswa Kumurudilia Yehova,” ona juu ya nini mwanaume mwenye alikuwa aliishaacha kweli aliona kama Yehova alipenda amurudilie.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 4, 2012)