Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 58

Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova

Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova

Wakristo wa kweli wameazimia kwamba hawataruhusu kamwe kitu au mtu yeyote aharibu uhusiano wao na Yehova. Tuna hakika wewe pia unahisi hivyo. Yehova anathamini ushikamanifu wako. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9.) Ni hali gani zinazoweza kufanya iwe vigumu kwako kuendelea kuwa mshikamanifu kwa Yehova, na ni nini kinachoweza kukusaidia?

1. Wengine wanawezaje kufanya iwe vigumu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova?

Watu fulani watajaribu kutushawishi tuache kumtumikia Yehova. Je, kuna watu wanaoweza kufanya jambo baya hivyo? Baadhi ya watu ambao wameacha kumtumikia Yehova, wanaeneza uwongo kuhusu tengenezo la Mungu ili kuharibu imani yetu. Watu hao wanaitwa waasi-imani. Pia, baadhi ya viongozi wa dini hueneza uwongo kutuhusu ili kuwafanya watu wasio waangalifu waache kumtumikia Yehova. Ni hatari kubishana na watu wanaotupinga, kusoma vitabu na mijadala yao kwenye mitandao, kutembelea tovuti zao, au kutazama video zao. Yesu alisema hivi kuhusu wale wanaojaribu kuwavunja moyo wengine waache kuwa washikamanifu kwa Yehova: “Waacheni. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili watatumbukia ndani ya shimo.”​—Mathayo 15:14.

Utafanya nini ikiwa mtu unayemfahamu ameamua kwamba hataki tena kuwa Shahidi wa Yehova? Tunaweza kuvunjika moyo mtu tunayempenda anapofanya hivyo. Huenda tukalazimika kuchagua kuwa washikamanifu kwa mtu huyo au kwa Yehova. Tunapaswa kuazimia kuendelea kuwa washikamanifu kwa Mungu badala ya mtu au kitu kingine chochote. (Mathayo 10:37) Basi tunatii amri ya Yehova kwamba tunapaswa kuacha kushirikiana na mtu kama huyo.​—Soma 1 Wakorintho 5:11.

2. Ni maamuzi gani yanayoweza kuonyesha kwamba sisi ni washikamanifu kwa Yehova?

Upendo wetu kwa Yehova utatuchochea kuepuka kushirikiana kwa njia yoyote na dini za uwongo. Hatupaswi kufanya kazi au kushirikiana na shirika lolote la kidini wala kujihusisha na shughuli zozote zinazohusiana na dini za uwongo. Yehova anatuonya hivi: “Tokeni [katika Babiloni Mkubwa], watu wangu.”​—Ufunuo 18:2, 4.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyoweza kuepuka kumruhusu mtu yeyote avunje ushikamanifu wako kwa Yehova. Pia, chunguza jinsi unavyoweza kuonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa kujitenga na Babiloni Mkubwa.

3. Jihadhari na walimu wa uwongo

Tunapaswa kutendaje tunaposikia habari zisizofaa kuhusu tengenezo la Yehova? Soma Methali 14:15, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kwa nini hatupaswi kuwa wepesi kuamini kila jambo tunalosikia?

Soma 2 Yohana 10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Tunapaswa kuwatendeaje waasi-imani?

  • Mbali na kuepuka kushirikiana na waasi-imani moja kwa moja, ni mambo gani mengine tunayopaswa kuepuka ili tusishawishiwe na mafundisho yao?

  • Unafikiri Yehova atahisije ikiwa tutasikiliza mambo yasiyofaa yanayosemwa kumhusu au kuhusu tengenezo lake?

4. Uwe mshikamanifu kwa Mungu, Mkristo mwenzako anapotenda dhambi

Unapotambua kwamba mtu fulani kutanikoni amefanya dhambi nzito, unapaswa kuchukua hatua gani? Fikiria kanuni iliyo katika Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli wa kale. Soma Mambo ya Walawi 5:1.

Kulingana na mstari huo, tunapotambua kwamba mtu fulani amefanya dhambi nzito, tunapaswa kuwaambia wazee habari tunazojua. Hata hivyo, kabla ya kuchukua hatua hiyo, ni jambo la fadhili kumhimiza mtu huyo aende kwa wazee na kuungama dhambi yake. Asipofanya hivyo, ushikamanifu wetu kwa Yehova utatuchochea kuwaambia wazee habari tunazojua. Kuchukua hatua hizo kunaonyeshaje upendo mshikamanifu kwa . . .

  • Yehova Mungu?

  • mtu aliyetenda dhambi?

  • watu wengine kutanikoni?

Ikiwa Mkristo mwenzako yuko hatarini, msaidie!

5. Jitenge na Babiloni Mkubwa

Soma Luka 4:8 na Ufunuo 18:4, 5, kisha ujibu maswali haya:

  • Je, bado jina langu limeandikwa kwenye orodha ya wafuasi wa dini ya uwongo?

  • Je, ninashirikiana na shirika linalohusiana na dini nyingine?

  • Je, kazi yangu inaunga mkono dini ya uwongo kwa njia yoyote?

  • Je, kuna hatua nyingine ambayo ninahitaji kuchukua ili kujitenga na dini ya uwongo?

  • Ikiwa nimejibu ndiyo kwa mojawapo ya maswali hayo, ninapaswa kufanya mabadiliko gani?

Katika visa hivyo vyote, fanya uamuzi utakaokuacha ukiwa na dhamiri safi na utakaoonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa Yehova.

Utafanya nini ukiombwa utoe mchango wa kusaidia mashirika ya kidini?

WATU FULANI HUSEMA: “Ninahitaji kujua mambo ambayo waasi-imani wanasema kuhusu Mashahidi wa Yehova ili nitetee ukweli.”

  • Je, hilo ni jambo la hekima? Kwa nini?

MUHTASARI

Ili tuendelee kuwa washikamanifu kwa Yehova, tunapaswa kuepuka kushirikiana na watu ambao si washikamanifu kwake. Pia, tunapaswa kujitenga kabisa na dini za uwongo.

Ungejibuje?

  • Kwa nini hatupaswi kutazama, kusoma, au kusikiliza habari za waasi-imani?

  • Tunapaswa kuwatendeaje wale ambao hawataki tena kuwa Mashahidi wa Yehova?

  • Tunawezaje kutii agizo la kutoka kwenye dini za uwongo?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyopaswa kutenda unaposikia habari za uwongo kuhusu Mashahidi wa Yehova.

“Je, Una Habari Kamili?” (Mnara wa Mlinzi, Agosti 2018)

Baadhi ya wapinzani wamefanya nini ili kujaribu kudhoofisha imani yetu?

Jihadhari na Udanganyifu (9:26)

Katika simulizi “Nimekuwa Nikimtafuta Mungu Tangu Utotoni,” soma kuhusu kuhani wa dini ya Shinto aliyeacha kushirikiana na dini ya uwongo.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2011)