Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 58

Uendelee Kuwa Mushikamanifu kwa Yehova

Uendelee Kuwa Mushikamanifu kwa Yehova

Wakristo wa kweli hawapendi kitu yoyote ao mutu yeyote aharibishe urafiki wao na Yehova. Tuko hakika kama na weye ni vile. Yehova anaona ushikamanifu wako kuwa wa maana sana. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9.) Ni mambo gani inaweza kufanya ikuwe nguvu kwako kuendelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova? Na nini njo inaweza kukusaidia?

1. Namna gani wengine wanaweza kufanya ikuwe nguvu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova?

Watu fulani watajaribu kutufanya tuache kumutumikia Yehova. Ni watu gani? Kwa mufano, watu fulani wenye wameacha kumutumikia Yehova, wanaeneza habari za uongo juu ya tengenezo ya Yehova kusudi waregeze imani yetu. Wale watu ni waasi-imani. Tena, viongozi fulani wa dini wanaeneza habari za uongo juu yetu juu ya kufanya wale wenye hawako waangalifu waache kumutumikia Yehova. Ni hatari kabisa kubishana na waasi-imani, kusoma vitabu vyao, kufungula site zao za Enternete ao kuangalia video zao. Yesu alisemaka jambo fulani juu ya wale wenye wanajaribu kuchochea wengine waache kumutumikia Yehova kwa ushikamanifu. Alisemaka hivi: “Muwaache. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kama kipofu anamuongoza kipofu, wote wawili wataanguka ndani ya shimo.”​—Matayo 15:14.

Halafu kama mutu fulani mwenye tunajua anaamua kama hapendi tena kuwa Shahidi wa Yehova? Tunaweza kuumia sana wakati mutu mwenye tunajua anafanya vile. Anaweza kutuambia kama atavunja uhusiano na siye ikiwa tunaendelea kumutumikia Yehova. Nia yetu kubwa inapaswa kuwa kubakia kwanza washikamanifu kwa Yehova. (Matayo 10:37) Njo maana tunatii amri ya Yehova yenye inatuambia tuepuke kuwa na uhusiano na watu wa vile.​—Soma 1 Wakorinto 5:11.

2. Namna gani maamuzi yetu inaweza kuonyesha kama tuko washikamanifu kwa Yehova ao hapana?

Kama tunamupenda Yehova, tutaepuka mambo yote yenye iko na uhusiano na dini ya uongo. Tunapaswa kuepuka kazi, matengenezo, ao jambo ingine yoyote yenye iko na uhusiano na dini ya uongo. Yehova anatuambia hivi: “Mutoke [kwa Babiloni Mukubwa], watu wangu.”​—Ufunuo 18:2, 4.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo yenye unaweza kufanya juu mutu yeyote asiregeze ushikamanifu wako kwa Yehova. Na tuone namna unaweza kuonyesha kama uko mushikamanifu kwa Yehova wakati unatoka mu Babiloni Mukubwa.

3. Fanya angalisho na waalimu wa uongo

Unapaswa kufanya nini kama unasikia mutu iko nasema mambo ya mubaya juu ya tengenezo ya Yehova? Musome Mezali 14:15, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini hatupaswe kuamini kila kitu yenye tunasikia?

Musome 2 Yohana 10, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Tunapaswa kutendea waasi-imani namna gani?

  • Hata kama hatuzungumuze moja kwa moja na waasi-imani, ni mu njia gani tunaweza kukutana na mafundisho yao?

  • Unawaza Yehova atajisikia namna gani kama tunasikiliza mambo ya mubaya yenye watu wanasema juu yake, na juu ya tengenezo yake?

4. Endelea kuwa mushikamanifu kwa Yehova wakati ndugu ao dada anafanya zambi

Kama unajua kuwa mutu fulani mu kutaniko alifanya zambi nzito, unapaswa kufanya nini? Tuone kanuni yenye Mungu alipatiaka taifa ya zamani ya Israeli. Musome Mambo ya Walawi 5:1.

Sawa vile ile andiko inaonyesha, ikiwa tunajua kama mutu fulani alifanya zambi nzito, tunapaswa kuambia wazee mambo yenye tunajua. Lakini mbele ya kufanya vile, ni muzuri kuambia ule mwenye alifanya zambi aende yeye peke kwa wazee na kutubu zambi yake. Kama haende kuongea na wazee, tutaonyesha kama tuko washikamanifu kwa Yehova kwa kuenda kuwaambia mambo yenye tunajua. Juu ya nini kufanya vile kunaonyesha kama . . .

  • tunapenda Yehova Mungu?

  • tunapenda mutu mwenye alifanya zambi?

  • tunapenda wengine mu kutaniko?

Kama Mukristo mwenzako iko na tatizo fulani, umusaidie!

5. Utoke kabisa mu Babiloni Mukubwa

Musome Luka 4:8 na Ufunuo 18:4, 5, na kisha ujibie hii maulizo:

  • Jina yangu ingali ku liste ya waamini wa dini fulani ya uongo?

  • Niko mu tengenezo fulani yenye iko na uhusiano na dini ya uongo?

  • Kazi yangu inaunga mukono dini ya uongo mu njia fulani?

  • Kuko mambo ingine mu maisha yangu yenye ninapaswa kubadilisha juu nijitenge kabisa na dini ya uongo?

  • Kama ninajibia ndiyo ku ulizo hata moja, ninapaswa kufanya mabadiliko gani?

Mu hali zote, ukamate uamuzi wenye utakusaidia uendelee kuwa na zamiri safi, na kuonyesha kama uko mushikamanifu kwa Yehova.

Utafanya nini kama unaombwa kutoa muchango kwa tengenezo fulani ya kidini ya kusaidia watu?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Inaomba nijue mambo yenye waasi-imani wanasemaka juu ya Mashahidi wa Yehova. Ile itanisaidia niweze kutetea kweli.”

  • Unawaza ni muzuri kufanya vile? Juu ya nini unasema vile?

KWA KIFUPI

Juu tuendelee kuwa washikamanifu kwa Yehova, tunapaswa kuepuka watu wenye hawako washikamanifu kwake, na tunapaswa kujitenga kabisa na dini ya uongo.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini hatupaswe kuangalia, kusoma, ao kusikiliza mawazo ya waasi-imani?

  • Tunapaswa kutendea namna gani wale wenye hawapendi tena kuwa Mashahidi wa Yehova?

  • Tunaweza kufanya nini juu ya kuonyesha kama tunatii amri ya kutoka mu dini ya uongo?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona mambo yenye unapaswa kufanya wakati wengine wanaeneza habari za uongo juu ya Mashahidi wa Yehova.

“Unajua Ukweli wa Mambo?” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 8, 2018)

Watu fulani wenye kupinga kweli wamefanya nini juu ya kujaribu kuregeza imani yetu?

Ukuwe Muangalifu Juu Wasikudanganye (9:32)

Mu habari “Nimemutafuta Mungu Tangu Ningali Mutoto,” ona namna padri fulani wa dini ya Shinto aliachana kabisa na dini ya uongo.

“Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 2011)