Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 59

Unaweza Kuvumilia Mateso

Unaweza Kuvumilia Mateso

Kama mutu iko Mukristo, kuko tu siku yenye wengine watamupinga ao kumutesa. Ile inapaswa kutuogopesha?

1. Juu ya nini tunapaswa kujua kama tutateswa?

Biblia inasema hivi: “Wale wote wenye wanapenda kuishi maisha ya ushikamanifu kwa Mungu katika umoja na Kristo Yesu watateswa pia.” (2 Timoteo 3:12) Yesu aliteswa juu hakukuwa sehemu ya ulimwengu wa Shetani. Na siye hatuko sehemu ya ulimwengu. Njo maana hatushangale wakati serikali na matengenezo ya kidini ya hii ulimwengu inatutesa.​—Yohana 15:18, 19.

2. Tunaweza kufanya nini juu ya kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

Kuanzia leo, tunapaswa kujifunza kumutumainia Yehova. Kila siku tunapaswa kupanga wakati ya kusali kwake na kusoma Biblia. Tena, usikuwe nakosa mikutano. Kama unafanya vile, utapata nguvu ya kuendelea kumutumikia Yehova bila woga, hata kama watu wa familia njo wanakutesa. Hata mutume Paulo alipataka mateso juu ya imani yake. Lakini aliandikaka hivi: “Yehova ni musaidizi wangu; sitaogopa.”​—Waebrania 13:6.

Kama tunazoea kuhubiri, ile inaweza pia kutusaidia tukuwe na uhodari. Kuhubiri kunatusaidia tumutumainie Yehova, na tusikuwe tunaogopa wanadamu. (Mezali 29:25) Kama unajifunza kuhubiri kwa uhodari kuanzia leo, ile itakusaidia uendelee kuhubiri hata kama guvernema inakataza kazi yetu.​—1 Watesalonike 2:2.

3. Tunapata faida gani wakati tunavumilia mateso?

Hatufurahiake mateso, lakini wakati tunavumilia mateso, imani yetu inakuwa nguvu zaidi. Tunamukaribia Yehova zaidi juu tunaona namna anatusaidia wakati tunajisikia kama hatuna tena nguvu ya kuendelea kuvumilia. (Soma Yakobo 1:2-4.) Yehova anasikiaka mubaya sana wakati anaona tuko nateseka. Lakini anafurahiaka sana wakati anaona tunavumilia. Biblia inasema hivi: “Kama munavumilia mateso kwa sababu ya kufanya mema, jambo hilo linamupendeza Mungu.” (1 Petro 2:20) Kama tunabakia waaminifu kwa Yehova, atatubariki kwa kutupatia uzima wa milele mu dunia mupya. Mu ile dunia, watu wote watamutumikia Yehova, na hakutakuwa tena mutu mwenye atawapinga.​—Matayo 24:13.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone juu ya nini inawezekana kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova hata kama wengine wanatutesa, na tuone namna Yehova atatubariki.

4. Unaweza kuvumilia wakati watu wa familia yako wanakupinga

Yesu alisemaka kama watu wa familia yetu wanaweza kutupinga wakati tunaamua kumutumikia Yehova. Musome Matayo 10:34-36, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Nini njo inaweza kutokea wakati mutu wa familia anaamua kumutumikia Yehova?

Juu ya kuona mufano, muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Unaweza kufanya nini kama mutu wa familia ao rafiki anajaribu kukuzuia kumutumikia Yehova?

Musome Zaburi 27:10 na Marko 10:29, 30. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Kama watu fulani mu familia yako ao marafiki wanajaribu kukuzuia kumutumikia Yehova, namna gani maneno yenye iko mu hii andiko inaweza kukusaidia?

5. Uendelee kumutumikia Yehova hata kama wengine wanakutesa

Wakati wengine wanajaribu kutuzuia kumutumikia Yehova, inaombaka kuwa na uhodari juu tuendelee kumutumikia. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Juu ya nini mifano yenye iko mu hii video inakutia nguvu?

Musome Matendo 5:27-29 na Waebrania 10:24, 25. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini tunapaswa kuendelea kumuabudu Yehova hata kama kazi yetu ya kuhubiri ao mikutano yetu inakatazwa?

6. Yehova atakusaidia uvumilie

Mashahidi wa Yehova wa mu dunia yote, ikuwe vijana ao wazee, wameendelea kumutumikia Yehova kwa uaminifu, hata wakati wengine wanawatesa. Juu ya kuona mambo yenye iliwasaidia, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, nini njo ilisaidia wale Mashahidi wavumilie?

Musome Waroma 8:35, 37-39 na Wafilipi 4:13. Kisha kusoma kila andiko, muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani ile andiko inakusaidia ukuwe hakika kama na weye unaweza kuvumilia majaribu yote?

Musome Matayo 5:10-12, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini unaweza kuwa na furaha hata wakati wengine wanakutesa?

Mamilioni ya watumishi wa Yehova wamevumilia mateso. Na weye unaweza kuvumilia!

WATU FULANI WANASEMAKA: “Siwezi kuvumilia mateso.”

  • Ni maandiko gani inaweza kuwasaidia wakuwe hakika kama wanaweza kuvumilia mateso?

KWA KIFUPI

Yehova anafurahi sana wakati anaona vile tuko najikaza kuendelea kumutumikia hata kama tunateswa. Atatusaidia tuendelee kuvumilia!

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini tunapaswa kujua kama tutateswa?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kujitayarisha kwa ajili ya mateso?

  • Nini njo inaweza kukusaidia ukuwe hakika kama unaweza kuendelea kumutumikia Yehova hata upate majaribu gani?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna kijana fulani anafasiria vile Yehova alimusaidiaka kuvumilia wakati alifungwaka juu ya kukatala kujiingiza mu vita.

Endelea Kuvumilia Hata Kama Unateswa (2:34)

Ona mambo yenye ilisaidiaka bibi na bwana fulani waendelee kumutumikia Yehova kwa uaminifu kwa miaka mingi hata kama wengine walikuwa nawapinga.

Kumutumikia Yehova Wakati wa Mabadiliko (7:11)

Ona namna unaweza kuendelea kuwa hodari wakati unateswa.

“Ujitayarishe Leo kwa Ajili ya Mateso” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 7, 2019)

Ona mawazo yenye unapaswa kuwa nayo wakati watu wa familia wanakupinga, na mambo yenye unaweza kufanya juu uendelee kuishi nao kwa amani bila kuacha kuwa muaminifu kwa Yehova.

“Kweli Hailete, ‘Amani, Bali Upanga’” (Munara wa Mulinzi, Mwezi wa 10, 2017)