Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SOMO LA 60

Endelea Kuimarisha Urafiki Wako na Yehova

Endelea Kuimarisha Urafiki Wako na Yehova

Katika masomo haya ya kujifunza Biblia, umejifunza mambo mengi kumhusu Yehova. Mambo ambayo umejifunza yamekusaidia kumpenda sana na huenda yamekuchochea kujiweka wakfu kwake na kubatizwa. Ikiwa bado hujachukua hatua hiyo, labda unafikiria kufanya hivyo hivi karibuni. Lakini baada ya kubatizwa, bado unahitaji kuendelea kumkaribia Yehova. Unaweza kuendelea kumkaribia Yehova milele. Jinsi gani?

1. Kwa nini unapaswa kuendelea kuimarisha urafiki wako na Yehova?

Tunapaswa kujitahidi kuendelea kuimarisha urafiki wetu na Yehova. Kwa nini? “Ili tusipeperushwe kamwe” mbali naye. (Waebrania 2:1) Ni nini kinachoweza kutusaidia tuendelee kumtumikia Yehova kwa uaminifu? Ni kwa kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri na kutafuta njia nyingine za kumtumikia Mungu wetu kikamili zaidi. (Soma Wafilipi 3:16.) Kumtumikia Yehova ndiyo maisha bora zaidi!​—Zaburi 84:10.

2. Unapaswa kuendelea kufanya nini kingine?

Ingawa umekamilisha masomo haya ya kujifunza Biblia, bado utaendelea kuishi maisha ya Kikristo. Biblia inasema kwamba tunapaswa “kuvaa utu mpya.” (Waefeso 4:23, 24) Unapoendelea kujifunza Neno la Mungu na kuhudhuria mikutano ya kutaniko, utajifunza mambo mapya kumhusu Yehova na sifa zake. Tafuta njia za kuiga utu wake kikamili zaidi katika maisha yako. Endelea kufanya mabadiliko yoyote yanayohitajika ili kumfurahisha Yehova.

3. Yehova atakusaidiaje uendelee kumkaribia?

Biblia inasema hivi: ‘Mungu atamaliza mazoezi yako, atakufanya uwe imara, atakutia nguvu, atakupa msingi imara. (1 Petro 5:10) Sisi sote hushawishiwa kufanya mambo mabaya. Lakini Yehova hutupatia msaada tunaohitaji ili tupinge vishawishi hivyo. (Zaburi 139:23, 24) Anaahidi kwamba atakupa hamu na nguvu za kuendelea kumtumikia kwa uaminifu.​—Soma Wafilipi 2:13.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyoweza kuendelea kumkaribia Yehova na jinsi atakavyokubariki.

4. Endelea kuwasiliana na Rafiki yako wa karibu zaidi

Kusali na kujifunza Biblia kumekusaidia uwe rafiki ya Yehova. Mambo hayo yanawezaje kukusaidia umkaribie hata zaidi?

Soma Zaburi 62:8, kisha mzungumzie swali hili:

  • Ili kuimarisha urafiki wako na Yehova, unawezaje kuboresha sala zako?

Soma Zaburi 1:2, na maelezo ya chini, kisha mzungumzie swali hili:

  • Ili kuimarisha urafiki wako na Yehova, unawezaje kuboresha usomaji wako wa Biblia?

Unaweza kufanya nini ili unufaike zaidi na funzo lako la kibinafsi? Ili kupata mapendekezo, onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Unaweza kutumia madokezo gani yaliyo katika video hiyo?

  • Ungependa kujifunza kuhusu habari gani?

5. Jiwekee malengo ya kiroho

Kujiwekea malengo katika utumishi wa Yehova kutakusaidia uendelee kumkaribia zaidi. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Katika video hiyo, Cameron alinufaikaje kwa kujiwekea malengo ya kiroho?

Si kila mtu anayeweza kuhamia katika nchi nyingine ili kuhubiri. Hata hivyo, sisi sote tunaweza kujiwekea malengo tunayoweza kutimiza. Soma Methali 21:5, kisha ufikirie malengo unayoweza kujiwekea . . .

  • katika kutaniko.

  • katika utumishi wa shambani.

Kanuni iliyo katika andiko hilo inawezaje kukusaidia kutimiza malengo yako?

Malengo unayoweza kujiwekea

  • Kuboresha sala zako.

  • Kusoma Biblia nzima.

  • Kumfahamu kila mtu katika kutaniko lenu.

  • Kuanzisha na kuongoza funzo la Biblia.

  • Kutumikia ukiwa painia msaidizi au painia wa kawaida.

  • Ikiwa wewe ni ndugu, unaweza kujitahidi kuwa mtumishi wa huduma.

6. Furahia maisha milele!

Soma Zaburi 22:26, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unaweza kufanya nini ili ufurahie maisha sasa na milele?

MUHTASARI

Endelea kuimarisha urafiki wako na Yehova na ujiwekee malengo ya kiroho. Nawe utafurahia maisha sasa na milele!

Ungejibuje?

  • Kwa nini unaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova atakusaidia uendelee kumtumikia kwa uaminifu?

  • Unawezaje kuimarisha urafiki wako na Yehova?

  • Malengo ya kiroho yanawezaje kukusaidia umkaribie Yehova zaidi?

Lengo la Muda Mrefu

CHUNGUZA ZAIDI

Yehova anathamini nini zaidi, je, ni tendo moja kubwa la ujitoaji au ni kumtumikia kwa uaminifu maisha yetu yote?

Uwe Mwaminifu Kama Abrahamu (9:20)

Hata mtumishi mwaminifu wa Yehova anaweza kupoteza shangwe. Ona jinsi ya kupata shangwe tena.

Pata Shangwe Tena Kupitia Kujifunza na Kutafakari (5:25)