Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 60

Usiache Kufanya Maendeleo

Usiache Kufanya Maendeleo

Mupaka hapa, umejifunza mambo mingi juu ya Yehova. Na mambo yenye umejifunza imefanya umupende na pengine imekuchochea ujitoe kwake na kubatizwa. Kama hauyabatizwa, pengine uko nafikiria kufanya vile hapa kesho-kesho. Lakini, ubatizo haiko njo mwisho. Unaweza kuendelea kumukaribia Yehova milele. Namna gani?

1. Juu ya nini unapaswa kuendelea kutia nguvu urafiki wako na Yehova?

Tunapaswa kujikaza sana juu urafiki wetu na Yehova uendelee kuwa nguvu. Juu ya nini? “Ili tusipeperushwe mbali” naye. (Waebrania 2:1) Tunaweza kufanya nini juu tuendelee kumutumikia Yehova kwa uaminifu? Tunapaswa kuendelea kuhubiri kwa bidii na kutafuta njia zingine za kumutumikia Yehova zaidi. (Soma Wafilipi 3:16.) Kumutumikia Yehova njo jambo ya maana sana mu maisha!​—Zaburi 84:10.

2. Unapaswa kuendelea kufanya nini ingine?

Hata kama tunafikia mwisho wa mazungumuzo yetu ya Biblia, maisha yako ya Kikristo, itaendelea. Biblia inasema kama tunapaswa “kuvaa utu mupya.” (Waefeso 4:23, 24) Wakati utaendelea kujifunza Biblia na kufika ku mikutano, utajifunza mambo ingine ya mupya juu ya Yehova na sifa zake. Fikiria namna unaweza kuonyesha sifa zake mu maisha yako. Kila mara, ikiwa unaona kama kuko jambo fulani yenye unapaswa kubadilisha mu maisha yako, ufanye vile juu umufurahishe Yehova.

3. Yehova atafanya nini juu ya kutusaidia tusiache kufanya maendeleo?

Biblia inasema hivi: “Mungu . . . yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu. Atawafanya kuwa imara, atawatia nguvu, atawafanya ninyi musitikisike.” (1 Petro 5:10) Siye wote tunapataka majaribu. Lakini, Yehova anatupatia mambo yote yenye tuko nayo lazima juu tuweze kushinda ile majaribu. (Zaburi 139:23, 24) Anatuambia kama atatupatia hamu na nguvu ya kuendelea kumutumikia kwa uaminifu.​—Soma Wafilipi 2:13.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna unaweza kuendelea kufanya maendeleo na namna Yehova atakubariki.

4. Usiache kuzungumuza na Rafiki yako wa sana na kumusikiliza

Kusali na kujifunza Biblia kumekusaidia ukuwe rafiki ya Yehova. Namna gani ile mambo mbili inaweza kukusaidia uendelee kumukaribia hata zaidi?

Musome Zaburi 62:8, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu urafiki wako na Yehova ukuwe nguvu, unaweza kufanya nini juu sala zako zikuwe muzuri zaidi?

Musome Zaburi 1:2 na maelezo ya chini, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu urafiki wako na Yehova ukuwe nguvu, unaweza kufanya nini juu upate faida zaidi wakati uko nasoma Biblia?

Unaweza kufanya nini juu upate faida zaidi wakati uko nafanya funzo yako ya pekee? Juu ya kuona mambo yenye inaweza kukusaidia, muangalie VIDEO, kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.

  • Ni mashauri gani yenye iko mu hii video yenye unaweza kutumikisha?

  • Unaweza penda kujifunza mambo gani?

5. Ujiwekee miradi ya kiroho

Kujiwekea miradi ya kiroho kutakusaidia usiache kufanya maendeleo. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.

  • Vile uliona mu video, Cameron alipata faida gani juu alijiwekea miradi ya kiroho?

Haiko kila mutu njo anaweza kuenda kuhubiri mu inchi ingine. Lakini, siye wote tunaweza kujiwekea miradi yenye tutaweza kufikia. Musome Mezali 21:5, na kisha uzungumuzie miradi yenye ungependa kujiwekea . . .

  • mu kutaniko.

  • mu kazi ya kuhubiri.

Namna gani kanuni yenye iko mu ile andiko inaweza kukusaidia ufikie miradi yako?

Miradi yenye unaweza kujiwekea

  • Kufanya sala zako zikuwe muzuri zaidi.

  • Kusoma Biblia yote.

  • Kujikaza kujua kila mutu mu kutaniko.

  • Kuanzisha na kuongoza funzo ya Biblia.

  • Kuwa painia musaidizi ao painia wa kawaida.

  • Kama uko ndugu, ujikaze kutimiza mambo yenye inaombwa juu ufikie kuwa mutumishi wa huduma.

6. Furahia maisha milele

Musome Zaburi 22:26, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Unaweza kufanya nini juu ufurahie maisha leo na milele?

KWA KIFUPI

Endelea kutia nguvu urafiki wako pamoja na Yehova, na kujiwekea miradi ya kiroho. Kama unafanya vile, utafurahia maisha milele!

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini unaweza kuwa hakika kama Yehova atakusaidia uendelee kumutumikia kwa uaminifu?

  • Unaweza kufanya nini juu ya kutia nguvu urafiki wako pamoja na Yehova?

  • Namna gani miradi ya kiroho inaweza kukusaidia ufanye maendeleo ya kiroho?

Pima kufanya hivi mwaka kesho

HABARI ZINGINE

Nini njo yenye Yehova anaona kuwa ya maana sana, tendo moja tu ya ajabu ya kuonyesha kama tuko washikamanifu kwake ao kumutumikia kwa uaminifu kila siku mu maisha yetu?

Ukuwe Muaminifu Kama Abrahamu (9:20)

Hata mutumishi muaminifu wa Yehova anaweza kupoteza furaha. Ona namna mutu anaweza kupata tena furaha.

Kujifunza na Kutafakari Kutakuletea Tena Furaha (5:25)

Juu ya nini ni jambo ya maana Mukristo akomale kiroho, na nini njo inaweza kumusaidia?

“Ujikaze Kukomala Kiroho Juu ‘Siku Kubwa ya Yehova Iko Karibu’” (Munara wa Mulinzi, 15 Mwezi wa 5, 2009)