Mambo Makuu ya Sehemu ya 1

Mambo Makuu ya Sehemu ya 1

Zungumzia maswali yafuatayo pamoja na mwalimu wako:

  1. Ni nini kinachokupendeza kuhusu ahadi za wakati ujao zilizo katika Biblia?

    (Ona Somo la 2.)

  2. Kwa nini unaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu?

    (Ona Somo la 3 na la 5.)

  3. Kwa nini ni muhimu kutumia jina la Yehova?

    (Ona Somo la 4.)

  4. Biblia inasema kwamba Mungu ndiye “chanzo cha uhai.” (Zaburi 36:9) Je, unaamini hivyo?

    (Ona Somo la 6.)

  5. Soma Methali 3:32.

    • Kwa nini Yehova ndiye anayepaswa kuwa Rafiki yetu wa karibu zaidi?

    • Yehova anatarajia nini kutoka kwa rafiki zake? Je, unafikiri hilo linafaa?

      (Ona Somo la 7 na la 8.)

  6. Soma Zaburi 62:8.

    • Ni mambo gani ambayo umemwambia Yehova katika sala? Unaweza kusali kuhusu mambo gani mengine?

    • Yehova anajibu sala kwa njia gani?

      (Ona Somo la 9.)

  7. Soma Waebrania 10:24, 25.

    • Unaweza kunufaikaje kwa kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

    • Je, unafikiri jitihada za kuhudhuria mikutano ni muhimu?

      (Ona Somo la 10.)

  8. Kwa nini ni muhimu kusoma Biblia kwa ukawaida? Umepanga ratiba gani ya kusoma Biblia kila siku?

    (Ona Somo la 11.)

  9. Kufikia sasa, umefurahia zaidi jambo gani kuhusu kujifunza Biblia?

  10. Tangu ulipoanza kujifunza Biblia, umekabili changamoto gani? Ni nini kitakachokusaidia uendelee kujifunza?

    (Ona Somo la 12.)