Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Maulizo ya Kujikumbusha ya Sehemu ya 2

Maulizo ya Kujikumbusha ya Sehemu ya 2

Uzungumuzie hii maulizo na mwalimu wako:

  1. Mungu atafanya nini dini zote za uongo?

    (Ona Somo ya 13.)

  2. Musome Kutoka 20:4-6.

    • Yehova anajisikiaka namna gani wakati watu wanatumia sanamu mu ibada?

      (Ona Somo ya 14.)

  3. Yesu ni nani?

    (Ona Somo ya 15.)

  4. Yesu iko na sifa gani zenye unafurahia sana?

    (Ona Somo ya 17.)

  5. Musome Yohana 13:34, 35 na Matendo 5:42.

    • Nani njo Wakristo wa kweli leo? Nini njo inakufanya uamini kama wao njo Wakristo wa kweli?

      (Ona Somo ya 18 na 19.)

  6. Nani njo kichwa cha kutaniko, na anaiongoza namna gani?

    (Ona Somo ya 20.)

  7. Musome Matayo 24:14.

    • Nini njo inaonyesha kama huu unabii uko natimia leo?

    • Ulishaambia nani juu ya habari njema?

      (Ona Somo ya 21 na 22.)

  8. Unawaza ni lazima ujikaze juu ufikie kubatizwa? Juu ya nini?

    (Ona Somo ya 23.)

  9. Unaweza kufanya nini juu Shetani na pepo wake wachafu wasikudanganye na wasikutendee mubaya?

    (Ona Somo ya 24.)

  10. Mungu anapenda tukuwe na maisha ya namna gani?

    (Ona Somo ya 25.)

  11. Juu ya nini tunatesekaka na kufa?

    (Ona Somo ya 26.)

  12. Musome Yohana 3:16.

    • Yehova amefanya nini juu ya kutukomboa kutoka mu zambi na kifo?

      (Ona Somo ya 27.)

  13. Musome Muhubiri 9:5.

    • Wafu wako mu hali gani?

    • Yesu atafanyia nini watu wengi wenye walishakufa?

      (Ona Somo ya 29 na 30.)

  14. Juu ya nini Ufalme wa Mungu unapita guvernema zote za wanadamu?

    (Ona Somo ya 31 na 33.)

  15. Unaamini kama Ufalme wa Mungu uko natawala sasa? Juu ya nini? Ulianza kutawala wakati gani?

    (Ona Somo ya 32.)