Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Je, Niko Tayari?

Je, Niko Tayari?

Je, Niko Tayari Kuhubiri Pamoja na Kutaniko?

Unaweza kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa ikiwa . . .

  • Unajifunza Biblia kwa ukawaida, unasali, na kuhudhuria mikutano ya kutaniko.

  • Unapenda na kuamini mambo unayojifunza na unataka kuwaambia wengine kuyahusu.

  • Unampenda Yehova na unachagua marafiki wa karibu kati ya wale wanaompenda.

  • Umejitenga na shirika lolote la kisiasa au la dini za uwongo.

  • Unaishi kulingana na viwango vya Yehova na unataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova.

Ikiwa unahisi kwamba uko tayari kuhubiri na kutaniko, mwalimu wako wa Biblia anaweza kufanya mpango ili ukutane na wazee na kuzungumzia jinsi unavyoweza kustahili.

Je, Niko Tayari Kubatizwa?

Unaweza kubatizwa ikiwa . . .

  • Wewe ni mhubiri ambaye hajabatizwa.

  • Unashiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri kulingana na uwezo wako.

  • Unaunga mkono na kufuata mwongozo wa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.”​—Mathayo 24:45-47.

  • Umejiweka wakfu kwa Yehova kupitia sala na unataka kumtumikia milele.

Ikiwa unahisi kwamba uko tayari kubatizwa, mwalimu wako wa Biblia anaweza kufanya mpango ili ukutane na wazee na kuzungumzia jinsi unavyoweza kustahili.