Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ninastahili?

Ninastahili?

Ninastahili Kuhubiri na Kutaniko?

Inawezekana unastahili kuanza kuhubiri na kutaniko kama . . .

  • Uko na zoezi ya kujifunza Biblia, kusali, na kufika ku mikutano ya kutaniko.

  • Unapenda mambo yenye uko najifunza, unaiamini, na unapenda kuilezea wengine.

  • Unamupenda Yehova na unachagula marafiki wenye wanamupenda.

  • Umeachana na mambo yote ya politike na ya dini ya uongo.

  • Unatii kanuni za Yehova na unapenda kuwa Shahidi wa Yehova.

Kama unaona kuwa unastahili kuanza kuhubiri na kutaniko, uambie mwalimu wako. Atajulisha wazee juu wazungumuze na weye ili kuona kama unastahili.

Ninastahili Kubatizwa?

Inawezekana unastahili kubatizwa kama . . .

  • Ulishakaanza kuhubiri na kutaniko.

  • Unajikazaka kuhubiri kwa ukawaida.

  • Unakuwaka unatii na kufuata muongozo wenye “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatoa.​—Matayo 24:45-47.

  • Umejitoa kwa Yehova katika sala na unapenda kumutumikia milele.

Kama unaona kuwa unastahili kubatizwa, uambie mwalimu wako. Atajulisha wazee juu wazungumuze na weye ili kuona kama unastahili.