Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo


Jinsi ya kunufaika zaidi na masomo haya ya Biblia

Jinsi ya kunufaika zaidi na masomo haya ya Biblia

Kwanza pitia muhtasari huu, kisha onyesha VIDEO.

SEHEMU YA KWANZA

Ili kujitayarisha kwa ajili ya kila somo, soma sehemu ya kwanza. Maswali yaliyoandikwa kwa wino mzito (A) na maandiko (B) yanakazia mambo makuu. Soma maandiko yaliyo na neno “soma.”

SEHEMU YA KATIKATI

Maneno yaliyo mwanzoni (C) katika sehemu ya Chimba Zaidi yanaeleza habari ambazo zitazungumziwa. Vichwa vidogo (D) vinaonyesha mambo makuu. Ukiwa pamoja na mwalimu wako, soma maandiko, jibu maswali, na utazame video.

Visanduku vilivyoandikwa VIDEO vinakuelekeza kwenye marejeo yaliyo na habari zaidi kuhusu mambo yanayozungumziwa. Baadhi ya video hizo zina masimulizi ya mambo halisi. Na video nyingine ni maigizo ingawa zinaonyesha mambo yanayoweza kutokea kihalisi.

Chunguza picha kwa makini na maelezo ya picha (E), na ufikirie jinsi unavyoweza kujibu swali lililo chini ya Watu Fulani Husema (F).

SEHEMU YA MWISHO

Somo linakamilishwa kwenye sehemu ya Muhtasari na Ungejibuje? (G). Andika tarehe ambayo somo limekamilishwa. Kwenye Lengo (H) kuna sehemu ya mambo ambayo unaweza kufanyia kazi. Chini ya Chunguza Zaidi (I) kuna habari za ziada ambazo unaweza kusoma au kutazama.

Jinsi ya kupata mistari ya Biblia

Biblia ni mkusanyo wa vitabu vidogo 66. Imegawanywa katika sehemu mbili: Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu (“Agano la Kale”) na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (“Agano Jipya”).

Maandiko yanaonyeshwa kwa jina la kitabu cha Biblia (A), kisha sura (B), na mstari au mistari (C).

Kwa mfano, Yohana 17:3 inamaanisha kitabu cha Yohana, sura ya 17, mstari wa 3.