Mambo ya kufanya juu upate faida wakati uko najifunza hii kitabu
Chunguza kwanza kurasa za mwanzo-mwanzo na kisha uangalie VIDEO.
SEHEMU YA KWANZA
Wakati uko natayarisha kila somo, soma sehemu ya kwanza. Maulizo yenye kuwa juu ya kila fungu (A) na maandiko (B) inakazia mawazo makubwa. Utaona pia kama maandiko fulani iko na neno “soma.”
SEHEMU YA KATIKATI
Maneno ya kwanza-kwanza (C) yenye iko chini ye sehemu Tujifunze Mambo Mingi Zaidi inaonyesha mambo yenye itazungumuziwa. Vichwa vidogo-vidogo (D) vinaonyesha mawazo makubwa yenye itazungumuziwa. Pamoja na mwalimu soma maandiko, jibia maulizo, na uangalie video.
VIDEO zinakusaidia uelewe muzuri mambo yenye uko najifunza. Video fulani zinaonyesha mambo yenye ilitokea kabisa. Na zingine zinachezwa tu lakini zinaonyesha hali zenye zinatokeaka.
Angalia picha na usome maelezo ya picha (E), na ufikirie namna unaweza kujibia ulizo ao maulizo yenye iko mu sehemu Watu Fulani Wanasemaka (F).
SEHEMU YA MWISHO
Kwa Kifupi na Maulizo ya kujikumbusha (G) njo sehemu zenye zinamalizia somo. Andika tarehe yenye mumemaliza kujifunza somo fulani. Sehemu Pima kufanya hivi (H) inakuonyesha jambo ya kufanya juu ujifunze mambo mingi zaidi ao juu utumikishe mambo yenye umejifunza. Mu sehemu Habari Zingine (I) muko mambo ingine yenye, kama unapenda, unaweza kusoma ao kuangalia.
Mu Hii Kitabu Muko:
|
|
|
|
Namna ya kutafuta maandiko mu Biblia
Biblia iko na vitabu 66. Iko na sehemu mbili: Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu (“Agano la Kale”) na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo (“Agano Jipya”).
Andiko inaonyeshwa na jina ya kitabu ya Biblia (A), sura (B), na mustari ao mistari (C).
Kwa mufano, Yohana 17:3 maana yake kitabu ya Yohana, sura ya 17, mustari wa 3.