Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utangulizi

Utangulizi

Kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo kitakusaidia kupata mistari ya Biblia na masimulizi yatakayokusaidia kukabiliana na changamoto maishani. Pia, kitakusaidia kutafuta mistari hususa ya Biblia ambayo itawatia moyo wengine na kuwasaidia kufanya maamuzi yanayomletea heshima Yehova. Tafuta kichwa unachotaka. Kila kichwa kina maswali mazuri na maelezo mafupi kuhusu masimulizi ya Biblia yatakayokuongoza. (Tazama sanduku “ Jinsi ya Kutumia Kitabu Hiki.”) Utapata kwa wingi ushauri, mwongozo, na faraja unayohitaji kutoka katika Neno la Mungu. Pia, utapata hazina unazoweza kushiriki na wengine, yaani, mistari ya Biblia itakayowaburudisha, itakayowasaidia kutatua matatizo yao, na kuwapatia ushauri na kuwatia moyo.

Kitabu hiki hakiorodheshi maandiko yote yanayohusu habari au kichwa fulani. Lakini ni kitabu kizuri kitakachokusaidia kuanza kufanya utafiti wako. (Met 2:​1-6) Ili kufanya utafiti wa kina zaidi, tumia marejeo ya pambizoni katika Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, na hata habari za utafiti (study notes) ikiwa zinapatikana katika lugha nyingine unayoelewa. Tumia Mwongozo wa Utafiti wa Mashahidi wa Yehova au Fahirisi ili kujifunza kikamili zaidi maana ya andiko fulani na matumizi yake. Soma machapisho ya karibuni zaidi ili kuhakikisha kwamba una uelewaji wa karibuni wa kweli za Kimaandiko.

Acheni kitabu Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo kiwasaidie kupata hekima, ujuzi, na uelewaji unaopatikana katika Maandiko Matakatifu. Unapotumia kitabu hiki, utasadiki hata zaidi kwamba “neno la Mungu liko hai nalo ni lenye nguvu.”—Ebr 4:12.