Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Faraja

Faraja

Faraja katika Maandiko inayotusaidia kushinda baadhi ya mambo yanayosababisha tuvunjike moyo

Hisia kali za kuwa na hatia

Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

2Fa 22:​8-13; 23:​1-3—Baada ya Sheria ya Musa kusomwa kwa sauti, Mfalme Yosia na raia wake wanatambua kwamba wana hatia kubwa

Ezr 9:​10-15; 10:​1-4—Kuhani Ezra na watu wengine wana hisia kali za hatia kwa sababu baadhi yao wamekosa kumtii Yehova na kuoa wanawake wa kigeni

Lu 22:​54-62—Mtume Petro anahisi hatia na kuhuzunika sana baada ya kukana mara tatu kwamba hamjui Yesu

Kut 3:11; 4:10—Nabii Musa anahisi hafai au hastahili anapoambiwa aende kukutana na Farao ili awatoe watu wa Mungu kutoka Misri

Yer 1:​4-6—Yeremia anahisi yeye ni kijana sana na hana uzoefu wa kutumikia akiwa nabii wa Yehova kwa watu wenye kiburi

  • Maandiko yenye kufariji:

  • Kut 3:12; 4:​11, 12—Kwa subira, Yehova anamhakikishia nabii Musa kwamba atamsaidia katika mgawo wake

    • Yer 1:​7-10—Yehova anamhakikishia nabii Yeremia kwamba atamsaidia kukabiliana na changamoto zitakazotokea

  • Kukata tamaa kwa sababu ya udhaifu na dhambi zetu

    • Tazama “Kukata Tamaa

    • Kukata tamaa wengine wanapotuvunja moyo, wanapotuumiza, au hata kutusaliti

Tazama “Kukata Tamaa

Kutoweza kufanya mengi kwa sababu ya ugonjwa au umri mkubwa

  • Zb 71:​9, 18; Mhu 12:​1-7

    • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Fa 20:​1-3—Mfalme Hezekia analia sana kwa sababu amepata ugonjwa mbaya ambao ungemsababishia kifo

    • Flp 2:​25-30—Epafrodito ameshuka moyo kwa sababu kutaniko limesikia kwamba anaumwa na ana wasiwasi kuwa wanaweza kuhisi ameshindwa kutimiza mgawo wake

  • Maandiko yenye kufariji:

  • 2Sa 17:​27-29; 19:​31-38—Mzee mshikamanifu Barzilai anapewa mgawo wa heshima kubwa, lakini kwa kuwa ana sifa ya kiasi anaukataa kwa sababu anahisi kwamba ana umri mkubwa na hawezi kutimiza mgawo huo

    • Zb 41:​1-3, 12—Mfalme Daudi alipokuwa mgonjwa sana, alikuwa na uhakika kwamba Yehova angemtegemeza

    • Mk 12:​41-44—Yesu anamsifu mjane maskini kwa mchango wake kwa sababu alitoa kila kitu alichokuwa nacho

Mahangaiko

Tazama “Mahangaiko

Mateso

Tazama “Mateso

Maumivu ya kihisia ya muda mrefu kwa sababu ya kutendewa kwa njia isiyofaa na wengine

Shaka kuhusu thamani yetu

  • Tazama “Shaka

    • Uchungu; kuweka kinyongo

    • Baadhi ya watu wana uchungu kwa sababu ya matatizo mengi wanayokabili au ukosefu wa haki

  • Mhu 9:​11, 12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ru 1:​11-13, 20—Naomi anahisi kwamba Yehova amemwacha kwa sababu ni mjane na ana huzuni ya kufiwa na watoto wake wawili

    • Ayu 3:​1, 11, 25, 26; 10:1—Ayubu anahisi uchungu kwa sababu amepoteza mali zake, amefiwa na watoto wake kumi, na ana afya mbaya

Maandiko yenye kufariji:

Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:

Ru 1:​6, 7, 16-18; 2:​2, 19, 20; 3:1; 4:​14-16—Naomi anakuwa na furaha tena baada ya kurudi kwa watu wa Mungu, kukubali msaada wao, na kuwasaidia wengine

  • Ayu 42:​7-16; Yak 5:11—Ayubu anavumilia kwa imani, na Yehova anambariki sana

    • Wengine wanakuwa na uchungu kwa sababu ya matendo yasiyo ya fadhili ya watu wengine

    • Mhu 4:​1, 2

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 1:​6, 7, 10, 13-16—Hana anaumia sana moyoni kwa sababu ya matendo yasiyo ya fadhili ya Penina na kuhukumiwa vibaya na Kuhani Mkuu Eli

  • Ayu 8:​3-6; 16:​1-5; 19:​2, 3—Wafariji watatu wa uwongo wa Ayubu ni waadilifu kupita kiasi na wanamshutumu isivyo haki, na kufanya Ayubu ahisi vibaya zaidi

1Sa 1:​9-11, 18—Hana alihisi vizuri baada ya kummiminia Yehova moyo wake

Ayu 42:​7, 8, 10, 17—Baada ya Ayubu kuonyesha roho ya kusamehe, Yehova anamrudishia afya nzuri na furaha yake

Wivu; husuda

Tazama “Wivu

Woga usiofaa; Hofu

Tazama “Woga