Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Shauri

Shauri

Kupokea shauri

Kwa nini tunapaswa kutafuta ushauri unaotegemea Biblia?

Kwa nini ni vizuri zaidi kusikiliza shauri badala ya kutetea matendo yetu?

Met 12:15; 29:1

Tazama pia Met 1:​23-31; 15:31

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 15:​3, 9-23—Nabii Samweli anapomrekebisha Sauli, mfalme huyo anatetea matendo yake na kukataa shauri; hivyo anakataliwa na Yehova

    • 2Nya 25:​14-16, 27—Mfalme Amazia anatenda dhambi na kukataa kurekebishwa na nabii wa Yehova, hivyo anapoteza kibali na ulinzi wa Yehova

Kwa nini tuwaheshimu waangalizi ambao wanatoa shauri?

1Th 5:12; 1Ti 5:17; Ebr 13:​7, 17

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • 3Yo 9, 10—Mtume Yohana anamshutumu Diotrefe kwa kuwatendea kwa njia isiyo ya heshima wale wanaoongoza katika kutaniko la Kikristo

Kwa nini tuwasikilize watu wenye umri mkubwa?

Law 19:32; Met 16:31

Tazama pia Ayu 12:12; 32:7; Tit 2:​3-5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 23:​16-18—Mfalme Daudi anasikiliza shauri kutoka kwa Yonathani, ambaye amemzidi miaka 30, naye anaimarishwa na shauri hilo

    • 1Fa 12:​1-17—Mfalme Rehoboamu anakataa ushauri wenye usawaziko wa wanaume wazee na kusikiliza ushauri usiofaa wa vijana, na kusababisha matokeo mabaya

Ni nini kinachoonyesha kwamba wanawake waaminifu na watumishi wa Yehova ambao ni vijana wanaweza kutoa ushauri unaofaa?

Ayu 32:​6, 9, 10; Met 31:​1, 10, 26; Mhu 4:13

Tazama pia Zb 119:100

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 25:​14-35—Abigaili anampatia Mfalme Daudi ushauri ambao unaokoa uhai wa watu wengi wasio na hatia na kumlinda Daudi asiwe na hatia ya damu

    • 2Sa 20:​15-22—Mwanamke fulani mwenye hekima katika jiji la Abeli alitoa ushauri uliookoa uhai wa watu wote jijini humo

    • 2Fa 5:​1-14—Msichana mdogo Mwisraeli anatoa pendekezo ambalo linafanya shujaa hodari ajue jinsi anavyoweza kuponywa ukoma

Kwa nini tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu kusikiliza ushauri wa watu wasiomheshimu Yehova au Neno lake?

Zb 1:1; Met 4:14

Tazama pia Lu 6:39

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Nya 10:​13, 14—Mfalme Sauli anatafuta ushauri kutoka kwa mtu anayewasiliana na roho badala ya kutafuta ushauri kutoka kwa Yehova, naye anakufa kwa sababu hakuwa mwaminifu

    • 2Nya 22:​2-5, 9—Mfalme Ahazia alikufa kwa sababu alisikiliza ushauri mbaya

    • Ayu 21:​7, 14-16—Ayubu anakataa mawazo ya watu wasiomheshimu Yehova

Kutoa shauri

Kwa nini ni jambo bora kusikiliza, kupata habari kamili, na kumsikiliza kila mtu anayehusika kabla ya kutoa shauri?

Met 18:​13, 17

Tazama pia Met 25:8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 1:​9-16—Kuhani Mkuu Eli anamshauri Hana kwa ukali kabla ya kupata habari kamili, akifikiri kwamba mwanamke huyo mwaminifu amelewa

    • Mt 16:​21-23—Mtume Petro anamkemea Yesu, anatoa ushauri akiwa na nia nzuri lakini ushauri huo ungeendeleza masilahi ya Shetani badala ya masilahi ya Yehova

Kwa nini tumwombe Yehova mwongozo kabla ya kutoa shauri?

Zb 32:8; 73:​23, 24; Met 3:​5, 6

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kut 3:​13-18—Nabii Musa anamuuliza Yehova kuhusu njia bora ya kujibu maswali ambayo huenda Waisraeli wenzake wangemuuliza

    • 1Fa 3:​5-12—Mfalme kijana Sulemani anamwomba Yehova hekima badala ya kujitegemea mwenyewe, na matokeo ni kwamba Yehova anambariki

Kwa nini ushauri tunaotoa na majibu yetu yanapaswa kutegemea Neno la Mungu?

Zb 119:​24, 105; Met 19:21; 2Ti 3:​16, 17

Tazama pia Kum 17:​18-20

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mt 4:​1-11—Shetani alipomjaribu, Yesu alimjibu si kupitia hekima yake mwenyewe, bali kupitia Neno la Mungu

    • Yoh 12:​49, 50—Yesu anaeleza kwamba mafundisho yake yote yanategemea mambo ambayo Baba yake alimfundisha, hivyo anatuwekea mfano mzuri wa kuiga

Kwa nini tunapaswa kujitahidi kuwa wapole tunapotoa shauri na hata ikiwezekana kutoa pongezi kwa unyoofu pamoja na shauri?

Gal 6:1; Kol 3:12

Tazama pia Isa 9:6; 42:​1-3; Mt 11:​28, 29

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

Ikiwa Mkristo analalamika kwetu kwamba Mkristo mwenzake amemtendea kosa, kama vile ulaghai au uchongezi, kwa nini inafaa kumtia moyo aende kuzungumza faraghani pamoja na mtu huyo aliyemkosea?

Tunawezaje kumtia moyo Mkristo anayehisi amekosewa awe mwenye rehema, subira, na mwenye kusamehe?

Mt 18:​21, 22; Mk 11:25; Lu 6:36; Efe 4:32; Kol 3:13

Tazama pia Mt 6:14; 1Ko 6:​1-8; 1Pe 3:​8, 9

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mt 18:​23-35—Yesu anatoa mfano wenye nguvu unaofafanua kwa nini ni muhimu sana tuwe wenye kusamehe

Kwa nini tunahitaji kushikamana na viwango vya Yehova tunapotoa shauri?

Zb 141:5; Met 17:10; 2Ko 7:​8-11

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 15:​23-29—Alipompatia shauri, nabii Samweli hakumwogopa Mfalme Sauli

    • 1Fa 22:​19-28—Licha ya vitisho na kutendewa vibaya, nabii Mikaya alikataa kubadili ujumbe wake wa onyo kwa Mfalme Ahabu

Tunawezaje kumshauri mtu bila kumsababishia madhara ya kiroho?

Ebr 12:​11-13

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 22:​31-34—Ingawa mtume Petro alifanya makosa mazito, Yesu alikuwa na uhakika kwamba angeyarekebisha na kuendelea kumtumikia Yehova na pia angeweza kuwaimarisha wengine

    • Flm 21—Mtume Paulo ana uhakika kwamba Filemoni atafuata ushauri unaopatana na mapenzi ya Mungu

Tunawezaje kuwa wenye fadhili tunapowashauri watu wenye matatizo au walioshuka moyo?

Tunawezaje kuonyesha kwamba lengo letu ni kumsaidia mtu awe tena na uhusiano mzuri na Yehova?

Tunawezaje kuwaonyesha heshima wale tunaowashauri, haidhuru umri au jinsia yao?

Kwa nini wazee wanapaswa kuwa thabiti zaidi wanapomrekebisha mtu anayekataa mara kwa mara shauri la Kimaandiko?