Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mashauri

Mashauri

Kushauriwa

Juu ya nini tunapaswa kutafuta mashauri yenye kutoka mu Biblia?

Juu ya nini ni muzuri kukubali shauri kuliko kutafuta kujitetea?

Mez 12:15; 29:1

Ona pia Mez 1:​23-31; 15:31

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 15:​3, 9-23—Wakati nabii Samweli anamushauria, Sauli anajitetea na anakatala shauri; ile inafanya Yehova amukatale

    • 2Ny 25:​14-16, 27—Mufalme Amazia anafanya zambi na anakatala mashauri yenye nabii wa Yehova anamupatia; ile inafanya Yehova asiendelee kumukubali na kumulinda

Juu ya nini tunapaswa kuheshimia waangalizi wenye wanatupatia mashauri?

1Te 5:12; 1Ti 5:17; Ebr 13:​7, 17

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • 3Yo 9, 10—Mutume Yohana, mwenye kuzeeka, anamulaumu Diotrefe juu haheshimiake wale wenye kuongoza mu kutaniko ya Kikristo

Juu ya nini tunapaswa kusikiliza wenye kuzeeka?

Law 19:32; Mez 16:31

Ona pia Yob 12:12; 32:7; Tit 2:​3-5

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 23:​16-18—Mufalme Daudi anasikiliza shauri ya Yonatani, mwenye ni mukubwa kwake na miaka karibu 30; na ile inamupatia nguvu

    • 1Fa 12:​1-17—Mufalme Rehoboamu anakatala shauri ya muzuri ya wanaume wenye kuzeeka, na anakubali shauri ya mubaya kutoka kwa wanaume vijana; ile inaleta matokeo ya mubaya

Nini njo inaonyesha kama wanamuke waaminifu na watumishi wa Yehova wenye wangali vijana wanaweza kutoa shauri ya muzuri?

Yob 32:​6, 9, 10; Mez 31:​1, 10, 26; Muh 4:13

Ona pia Zb 119:100

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 25:​14-35—Abigaili anamupatia Daudi shauri yenye inaokoa watu wengi na inasaidia Daudi asikuwe na hatia ya damu

    • 2Sa 20:​15-22—Mwanamuke moya mwenye hekima mu muji wa Abeli anaokoa muji muzima kupitia shauri yake

    • 2Fa 5:​1-14—Mutoto mwanamuke Muisraeli anatoa pendekezo yenye inasaidia mukubwa fulani wa jeshi mwenye nguvu ajue namna anaweza kupona ukoma

Juu ya nini tunapaswa kuwa waangalifu wakati tunashauriwa na mutu mwenye haheshimie Yehova na Neno yake?

Zb 1:1; Mez 4:14

Ona pia Lu 6:39

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Ny 10:​13, 14—Mufalme Sauli anazungumuza na roho fulani kupitia muchawi kuliko kutafuta shauri ya Yehova na anakufa juu ya kukosa kuwa muaminifu

    • 2Ny 22:​2-5, 9—Mufalme Ahazia anasikiliza washauri wabaya na anafikia kufa

    • Yob 21:​7, 14-16—Yobu anakatala kukubali mawazo ya wale wenye hawamuheshimie Yehova

Kutoa shauri

Mbele ya kutoa shauri, juu ya nini ni muzuri zaidi kusikiliza, kuelewa mambo yote muzuri, na kupata habari kwa wote wenye kuhusika?

Mez 18:​13, 17

Ona pia Mez 25:8

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 1:​9-16—Kuhani mukubwa Eli, anamushauria Hana kwa ukali mbele ya kujua habari yote, anawaza kama ule mwanamuke mwaminifu iko mulevi

    • Mt 16:​21-23—Juu mutume Petro hajue habari yote, anamupatia Yesu shauri yenye ingemufurahisha Shetani kuliko yenye ingemufurahisha Yehova

Juu ya nini ni muzuri kusali kwa Yehova mbele ya kupatia mutu shauri?

Zb 32:8; 73:​23, 24; Mez 3:​5, 6

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Kut 3:​13-18—Nabii Musa anamuuliza Yehova namna ya muzuri ya kujibia maulizo yenye Waisraeli wenzake wanaweza kuuliza

    • 1Fa 3:​5-12—Mufalme Sulemani anamuomba Yehova hekima kuliko kujitumainia yeye mwenyewe; na Yehova anamubariki juu ya ile

Juu ya nini mashauri yetu inapaswa kutegemea kabisa Neno ya Mungu?

Zb 119:​24, 105; Mez 19:21; 2Ti 3:​16, 17

Ona pia Kum 17:​18-20

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 4:​1-11—Wakati Shetani anamujaribu, Yesu anajibu kwa kutegemea hekima ya Yehova, hapana yake

    • Yoh 12:​49, 50—Yesu anafasiria kama mafundisho yake yote inategemea mambo yenye Baba yake alimufundisha, na ile ni mufano muzuri kwetu

Juu ya nini tunapaswa kujikaza kuwa wapole wakati tunashauria mutu na hata kumupongeza kutoka ku moyo wakati inawezakana?

Gal 6:1; Kol 3:12

Ona pia Isa 9:6; 42:​1-3; Mt 11:​28, 29

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Kama Mukristo mwenzetu anatuambia kama Mukristo mwingine alimukosea, kwa mufano kwa kumuiba ao kumusingizia, juu ya nini ni muzuri tumuambie aende tu aongee na ule Mukristo mwenye alimukosea?

Namna gani tunaweza kutia moyo Mukristo mwenye anajisikia kuwa amekosewa juu akuwe na rehema, akuwe muvumilivu, na akuwe tayari kusamehe?

Mt 18:​21, 22; Mk 11:25; Lu 6:36; Efe 4:32; Kol 3:13

Ona pia Mt 6:14; 1Ko 6:​1-8; 1Pe 3:​8, 9

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mt 18:​23-35—Yesu anatoa mufano ya muzuri sana ili kufasiria juu ya nini ni jambo ya maana kusamehe

Wakati tuko nashauria mutu, juu ya nini hatupaswe kuenda pembeni ya Maandiko?

Zb 141:5; Mez 17:10; 2Ko 7:​8-11

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 15:​23-29—Nabii Samweli anakatala kuogopeshwa na Mufalme Sauli

    • 1Fa 22:​19-28—Nabii Mikaya anakatala kubadilisha ujumbe wa kumuonya Mufalme Ahabu, hata kama ule mufalme anamuogopesha na kumutendea mubaya

Namna gani tunaweza kushauria mutu bila kumuumiza?

Ebr 12:​11-13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Lu 22:​31-34—Hata kama Petro alifanya makosa makubwa, Yesu anamuhakikishia kama ataweza kutia nguvu wengine

    • Flm 21—Mutume Paulo anaonyesha kama iko hakika Filemoni atafuata shauri yenye anamupatia

Namna gani tunaweza kuonyesha fazili wakati tunashauria mutu mwenye kuwa na mahangaiko ao mwenye kuvunjika moyo?

Namna gani tunaweza kuonyesha mutu mwenye alifanya zambi kama nia yetu ni kumusaidia?

Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunaheshimia mutu mwenye tunapatia shauri, hata akuwe wa miaka ngapi ao ikuwe ni mwanamuke ao mwanaume?

Juu ya nini wazee hawapaswe kubadilisha musimamo wakati wako nashauria mutu mwenye kila mara anakatalaka mashauri yenye kutegemea Biblia?