Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kitia-Moyo

Kitia-Moyo

Juu ya nini watu wa Mungu wanapaswa kutiana moyo?

Isa 35:​3, 4; Kol 3:16; 1Te 5:11; Ebr 3:13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 32:​2-8—Mufalme Hezekia anatia watu wake moyo wakati maadui wanawaogopesha

    • Da 10:​2, 8-11, 18, 19—Malaika anamutia moyo na kumupatia nguvu nabii Danieli mwenye kuzeeka na mwenye kuchoka

Wale wenye wako na madaraka wanaombwa nini kuhusu kutia wengine moyo?

Isa 32:​1, 2; 1Pe 5:​1-3

Ona pia Mt 11:​28-30

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Kum 3:28; 31:​7, 8—Sawa vile Yehova anamuambia afanye, Musa anamutia moyo na kumutia nguvu Yoshua, mwenye atakamata nafasi yake

    • Mdo 11:​22-26; 14:22—Wakati ya mateso, mutume Paulo na Barnaba wanatia moyo Wakristo wa Antiokia

Juu ya nini ni jambo ya maana kupongeza mutu kutoka ku moyo wakati tuko namutia moyo?

Mez 31:​28, 29; 1Ko 11:2

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Amu 11:​37-40—Wanamuke wa Israeli wanamutembelea mutoto mwanamuke wa Yefta juu ya kumupongeza kwa ajili ya roho yake ya kujinyima

    • Ufu 2:​1-4—Hata kama inaomba Yesu arekebishe Wakristo wa Efeso, anawaambia pia mambo yenye walikuwa nafanya muzuri

Namna gani watumishi waaminifu wa Yehova wanaweza kutiana moyo?

Mez 15:23; Efe 4:29; Flp 1:​13, 14; Kol 4:6; 1Te 5:14

Ona pia 2Ko 7:​13, 15, 16

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 23:​16-18—Yonatani anamutafuta rafiki yake kijana Daudi na anamutia moyo mu magumu

    • Yoh 16:33—Yesu anatia moyo wanafunzi wake kwa kuwakumbusha kama alishinda ulimwengu na ikiwa wanaiga mufano wake wataweza pia kushinda ulimwengu

    • Mdo 28:​14-16—Wakati Paulo iko naenda Roma juu asambishwe, ndugu waaminifu wanakuya kumutia moyo na ile inamupatia nguvu

Juu ya nini ni muzuri kuonyesha wengine heshima kuliko kuwasemea mubaya?

Flp 2:​14-16; Yud 16-19

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Juu ya nini kuwa pamoya na waamini wenzetu kunatutiaka moyo?

Mez 27:17; Ro 1:​11, 12; Ebr 10:​24, 25; 12:12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 20:​1-19—Wakati Mufalme Yehoshafati anaogopeshwa na jeshi kubwa, anakusanya watu pamoya na wanasali

    • Mdo 12:​1-5, 12-17—Kisha mutume Yakobo kuuawa na kisha mutume Petro kufungwa, kutaniko ya Yerusalemu inakutana pamoya juu ya kusali

Namna gani kuwa na mawazo ya muzuri kunatutiaka moyo tuvumilie magumu?

Mdo 5:​40, 41; Ro 8:​35-39; 1Ko 4:​11-13; 2Ko 4:​16-18; 1Pe 1:​6, 7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 39:​19-23; 40:​1-8—Hata kama walimusingizia na kumufunga bila kosa, Yosefu anaendelea kuwa mushikamanifu na iko kabisa tayari kusaidia wengine

    • 2Fa 6:​15-17—Nabii Elisha haogope mbele ya hatari kubwa, na anasali juu mutumishi wake naye asikuwe na woga

Kupata vitia-moyo mu Neno ya Mungu

Yehova anatuahidi kama atatusaidia namna gani?

Namna gani kufikiria uvumilivu na rehema ya Yehova kunaweza kututia moyo?

Yehova anaweza kufanyia nini wale wenye wanajisikia kuwa zaifu?

Zb 46:1; Isa 12:2; 40:​29-31; Flp 4:13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 1:​10, 11, 17, 18—Yehova anamusikiliza Hana wakati anasali na anamusaidia apate kitulizo wakati iko na huzuni na uchungu

    • 1Fa 19:​1-19—Wakati nabii Eliya iko mwenye kuvunjika moyo, Yehova anamusaidia. Anamutia moyo na kumufariji na anamutuliza kwa kumupatia tumaini

Namna gani tumaini yetu yenye kutegemea Biblia inatutia moyo?

2Ny 15:7; Zb 27:​13, 14; Ebr 6:​17-19; 12:2

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yob 14:​1, 2, 7-9, 13-15—Hata mu wakati ya magumu sana, Yobu anapata kitulizo kupitia tumaini ya ufufuo

    • Da 12:13—Nabii Danieli, mwenye iko na miaka karibu 100, anapata kitia-moyo kutoka kwa malaika mwenye anamuambia kuhusu zawabu yenye atapata

Juu ya nini kusali na kutafakari juu ya Yehova kunaweza kututia moyo?

Zb 18:6; 56:​4, 11; Ebr 13:6

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 30:​1-9—Wakati Mufalme Daudi iko na magumu, anasali kwa Yehova na anapata nguvu

    • Lu 22:​39-43—Wakati iko mu magumu ya nguvu sana, Yesu anasali na Yehova anamujibia kwa kumutumia malaika juu amutie moyo

Ni vitia-moyo gani vyenye tunaweza kupata kwa kusikiliza habari za muzuri na kuziambia wengine?

Mez 15:30; 25:25; Isa 52:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 15:​2-4—Mutume Paulo na Barnaba wanatia moyo makutaniko yenye wanatembelea

    • 3Yo 1-4—Wakati alishazeeka, mutume Yohana anatiwa moyo kwa kusikia kama wale wenye aliambia habari njema wanaendelea kuwa waaminifu