Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Uvumilivu

Uvumilivu

Je, watumishi wa Yehova wanahitaji uvumilivu?

Kwa nini tunapaswa kutarajia kwamba baadhi ya watu watatupuuza au kututesa tunapowahubiria?

Mt 10:22; Yoh 15:​18, 19; 2Ko 6:​4, 5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Pe 2:5; Mwa 7:23; Mt 24:​37-39—Ingawa Noa ni “mhubiri wa uadilifu,” watu wengi wanakataa ujumbe wake, hivyo yeye na familia yake tu ndio wanaookoka wakati wa Gharika

    • 2Ti 3:​10-14—Mtume Paulo anatumia mfano wake wa uvumilivu kumtia moyo Timotheo avumilie

Kwa nini tunaweza kutarajia upinzani hata kutoka kwa watu wa familia yetu?

Mt 10:​22, 36-38; Lu 21:​16-19

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 4:​3-11; 1Yo 3:​11, 12—Kaini anamuua ndugu yake kwa sababu matendo ya Kaini ni maovu, na matendo ya Abeli ni ya uadilifu

    • Mwa 37:​5-8, 18-28—Ndugu za Yosefu wanamshambulia na kumuuza Yosefu awe mtumwa baada ya kuwasimulia ndoto kutoka kwa Yehova

Tunapoteswa, kwa nini hatuhitaji kuogopa kifo?

Mt 10:28; 2Ti 4:​6, 7

Tazama pia Ufu 2:10

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 3:​1-6, 13-18—Shadraki, Meshaki, na Abednego hawakuabudu sanamu ingawa mfalme alisema kwamba wangeuawa ikiwa wangekataa kuabudu sanamu

    • Mdo 5:​27-29, 33, 40-42—Licha ya tishio la kuuawa, mitume wanaendelea kuhubiri kwa uvumilivu

Ni nini kitakachotusaidia kuendelea kuwa waaminifu kwa Yehova hata tunapotiwa nidhamu?

Met 3:​11, 12; Ebr 12:​5-7

Kwa nini inaweza kuwa vigumu kuvumilia wengine wanapoacha kumtumikia Yehova?

Yer 1:​16-19; Hab 1:​2-4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Zb 73:​2-24—Mtunga zaburi anapoona amani na ufanisi wa watu waovu, anatilia shaka thamani ya kuvumilia katika utumishi wake kwa Yehova

    • Yoh 6:​60-62, 66-68—Ingawa watu wengi wanaacha kumfuata Yesu, mtume Petro anaazimia kuendelea kumfuata Yesu

Ni nini kitakachotusaidia kuvumilia?

Kushikamana na Yehova

Kupata ujuzi wa Neno la Mungu kupitia kujifunza na kutafakari

Kumkaribia Yehova kwa ukawaida kupitia sala za kutoka moyoni

Ro 12:12; Kol 4:2; 1Pe 4:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 6:​4-11—Nabii Danieli anaendelea kusali bila kujificha na kwa ukawaida, licha ya kwamba kufanya hivyo kungehatarisha uhai wake

    • Mt 26:​36-46; Ebr 5:7—Katika usiku wa mwisho wa maisha yake hapa duniani, Yesu anasali kwa bidii na kuwatia moyo wengine wafanye hivyo

Kushirikiana kwa ukawaida na waabudu wenzetu katika ibada

Kufikiria kuhusu baraka ambazo Yehova ametuahidi

Kuimarisha upendo wetu kwa Yehova, kwa ndugu na dada zetu Wakristo, na kupenda uadilifu

Kuimarisha imani yetu

Kudumisha mtazamo mzuri kuelekea kuteseka

Kuvumilia kwa uaminifu kuna manufaa gani?

Tunamheshimu Yehova Mungu

Met 27:11; Yoh 15:​7, 8; 1Pe 1:​6, 7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 1:​6-12; 2:​3-5—Shetani anamshtaki Yehova kuhusu utimilifu wa Ayubu, shtaka ambalo linaweza kujibiwa tu na Ayubu anapovumilia kwa uaminifu akiwa mtumishi wa Yehova

    • Ro 5:19; 1Pe 1:​20, 21—Kwa kuvumilia kwa uaminifu hadi mwisho, Yesu anajibu swali hili muhimu: Je, mwanadamu mkamilifu anaweza kudumisha utimilifu chini ya majaribu makali zaidi?

Tunawatia moyo wengine wavumilie

Uvumilivu unatusaidia kuwa na matokeo katika huduma yetu

Tunapata kibali cha Yehova na baraka alizoahidi