Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Imani

Imani

Tunajuaje kwamba imani ni jambo muhimu sana kwa Yehova?

Yoh 3:​16, 18; Gal 3:​8, 9, 11; Efe 6:16; Ebr 11:6

Tazama pia 2Ko 5:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ebr 11:1–12:3—Mtume Paulo anaeleza maana ya imani na kutoa mifano mingi ya imani, kuanzia Abeli hadi Yesu Kristo

    • Yak 2:​18-24—Yakobo anatumia mfano wa Abrahamu kuonyesha kwamba imani yetu inapaswa kuambatana na matendo

Ni nini kitakachotusaidia kuimarisha imani yetu?

Ro 10:​9, 10, 17; 1Ko 16:13; Yak 2:17

Tazama pia Ebr 3:​12-14

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Nya 20:​1-6, 12, 13, 20-23—Watu wa Mungu wanapotaka kushambuliwa na maadui, Mfalme Yehoshafati anawaambia kwamba ili wafanikiwe ni lazima wawe na imani katika Yehova na manabii Wake

    • 1Fa 18:​41-46—Nabii Eliya anaonyesha imani kwa kungoja kwa subira hadi Yehova atimize ahadi Yake ya kukomesha ukame uliodumu kwa muda mrefu