Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Familia

Familia

Yehova alianzisha familia

Wazazi

Tazama “Wazazi

Baba

Tazama “Baba

Mama

Tazama “Mama

Waume, Wake

Tazama “Ndoa

Wana na Mabinti

Watoto wana majukumu gani katika familia?

Kwa nini watoto wanapaswa kuwatii wazazi wao?

Efe 6:​1-3; Kol 3:20

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Zb 78:​1-8—Waisraeli wanawasimulia watoto wao mambo ambayo babu zao walifanya ili watoto wao wawe na uhakika katika Mungu na wasiwe waasi

    • Lu 2:​51, 52—Ingawa Yesu ni mkamilifu, anaendelea kuwatii wazazi wake wasio wakamilifu katika ujana wake wote

Kwa nini huenda ikawa vigumu kwa watoto kuwatii wazazi wao?

Mungu ana maoni gani kuhusu watoto wanaowaasi wazazi wao?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kum 21:​18-21—Kulingana na Sheria ya Musa, mwana ambaye anakuja kuwa mlevi, mkaidi, mwasi, na anakataa kurekebishwa angeuawa

    • 2Fa 2:​23, 24—Kikundi cha wavulana wanapomdhihaki nabii Elisha, na kumvunjia heshima sana mwakilishi wa Mungu, wanararuliwa na kuuawa na dubu wawili

Wazazi wanapaswa kuhisije kuhusu pendeleo lao la kulea watoto?

Zb 127:3; 128:3

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Law 26:9—Waisraeli waliona kupata watoto kuwa ishara ya baraka kutoka kwa Yehova

    • Ayu 42:​12, 13—Kwa sababu ya kuonyesha utimilifu wa pekee, Yehova anambariki Ayubu kwa kumpa yeye na mke wake watoto kumi zaidi

Yehova anataka watoto watendeane kwa njia gani?

Zb 34:14; Met 15:23; 19:11

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mwa 27:41; 33:​1-11—Yakobo anamwonyesha heshima Esau, ndugu yake, na hivyo kufanya amani, naye Esau anaitikia kwa upendo

Watoto ambao ni watu wazima wana jukumu gani kuelekea wazazi, babu, na nyanya (bibi) zao?

Met 23:22; 1Ti 5:4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 11:​31, 32—Anapoondoka Uru, Abrahamu anamchukua Tera, baba yake, na kumtunza hadi anapokufa

    • Mt 15:​3-6—Yesu anatumia Sheria ya Musa kuonyesha kwamba watoto ambao ni watu wazima wanapaswa kuwategemeza wazazi wao wenye uhitaji

Wakwe

Tazama “Wakwe

Babu na Nyanya (Bibi)

Tazama “Babu na Nyanya (Bibi)