Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Familia

Familia

Yehova njo alianzishaka familia

Wazazi

Ona “Wazazi

Baba

Ona “Baba

Mama

Ona “Mama

Bwana, Bibi

Ona “Ndoa

Watoto

Watoto wako na daraka gani mu familia?

Juu ya nini watoto wanapaswa kutii wazazi wao?

Efe 6:​1-3; Kol 3:20

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Zb 78:​1-8—Waisraeli wanaelezea watoto wao matendo ya mababu zao juu watoto wamutumainie Yehova na wasimuasi

    • Lu 2:​51, 52—Hata kama Yesu ni mukamilifu, wakati iko kijana anaendelea kutii wazazi wake wenye hawakamilike

Juu ya nini pengine inakuwaka nguvu kwa watoto kuheshimia wazazi wao?

Mungu anaonaka namna gani watoto wenye kuasi?

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Kum 21:​18-21—Sheria ya Musa inaamuru kuua mutoto mwenye anakuwa kichwa-nguvu, muasi, na mulevi, lakini mwenye anakatala kurekebishwa

    • 2Fa 2:​23, 24—Wakati kikundi ya vijana wanamukosea heshima nabii Elisha, mwenye alimuwakilisha Mungu, wengi wanauawa na dubu wawili

Namna gani wazazi wanapaswa kuona pendeleo ya kukomalisha watoto?

Zb 127:3; 128:3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Law 26:9—Kwa waisraeli, kuzala watoto ni baraka ya Yehova

    • Yob 42:​12, 13—Juu Yobu alionyesha uaminifu-mushikamanifu, Yehova anamubariki yeye na bibi yake kwa kuwapatia watoto wengine kumi

Namna gani watoto mu familia wanapaswa kutendeana mu njia yenye itamufurahisha Yehova?

Zb 34:14; Mez 15:23; 19:11

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mwa 27:41; 33:​1-11—Yakobo anafanya yote yenye anaweza juu ya kumuonyesha Esau heshima na juu ya kufanya amani; Esau naye anamutendea kwa upendo

Watoto wenye walishakomala, wako na daraka gani kuelekea wazazi wao na watate (ao wakambo) wao?

Mez 23:22; 1Ti 5:4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 11:​31, 32—Wakati anatoka Uru, Abrahamu anaenda na baba yake, Tera, na anamuhangaikia mupaka wakati ule baba yake anakufa

    • Mt 15:​3-6—Kupitia Sheria ya Musa Yesu anaonyesha kama watoto wenye kukomala wanapaswa kusaidia wazazi wenye wako mu uhitaji

Wakwe

Ona “Wakwe

Watate

Ona “Watate