Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kifo

Kifo

Ni mifano gani ya Biblia inaonyesha kama ni kawaida kuhuzunika wakati mutu anakufa?

Nini inaonyesha kama Yehova anapenda sana kufariji wale wenye kuhuzunika?

Namna gani kujua hali ya wafu kunatutuliza?

Muh 9:​5, 10; 1Te 4:13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Lu 20:​37, 38—Yesu anafasiria kama ufufuo ni jambo ya kweli kabisa, juu kwa maoni ya Yehova wenye walishakufa wako tu sawa wako naishi

    • Yoh 11:​5, 6, 11-14—Kisha rafiki yake mupendwa Lazaro kufa, Yesu anafananisha kifo na usingizi

    • Ebr 2:​14, 15—Mutume Paulo anaonyesha kama hatupaswe kuwa watumwa wa kuogopa kifo

Namna gani mutu anaweza kuwa wa maana zaidi kwa Yehova wakati anakufa kuliko wakati alizaliwa?

Biblia inasema nini juu ya kifo, na Mungu atafanya nini juu ya kifo?

Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama kutakuwa ufufuo?

Isa 26:19; Yoh 5:​28, 29; Mdo 24:15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Biblia inazungumuzia ufufuo kenda wa watu; munane kati yao walifufuliwa juu ya kuishi ku dunia. Kwa wale wenye wako na huzuni juu walipoteza mupendwa wao, kila habari inaweza kuwafariji na kuwapatia tumaini

      • 1Fa 17:​17-24—Nabii Eliya anafufula mutoto wa mujane wa Sarefati, mu muji wa Sidoni

      • 2Fa 4:​32-37—Nabii Elisha anafufula kijana mwanaume mu muji wa Shunemu na anamupana kwa wazazi wake

      • 2Fa 13:​20, 21—Mwanaume mwenye anatokea kufa anafufuka wakati maiti yake inagusa mifupa ya nabii Elisha

      • Lu 7:​11-15—Mu muji wa Naini, Yesu anasimamisha watu wenye walikuwa naenda kuzika mutoto mwanaume wa mujane fulani na anamufufula

      • Lu 8:​41, 42, 49-56—Yesu anafufula mutoto mwanamuke wa Yairo, ofisa wa sinagogi

      • Yoh 11:​38-44—Yesu anafufula rafiki yake mupendwa Lazaro

      • Mdo 9:​36-42—Mutume Petro anafufula Dorkasi, Mukristo mupendwa mwenye anajulikana juu ya matendo yake ya fazili

      • Mdo 20:​7-12—Mutume Paulo anafufula kijana mwanaume mwenye kuitwa Eutiko, mwenye alikufa kisha kuanguka ku dirisha

    • Yesu anafufuliwa na kuwa kiumbe wa roho mwenye hawezi kufa; ile inatuhakikishia kama kutakuwa ufufuo

    • Yesu njo wa kwanza kufufuliwa juu ya kuishi mbinguni akiwa na hali ya kutokufa, lakini haiko wa mwisho; wafuasi wake watiwa-mafuta 144000 wanafufuliwa pia wakiwa na hali ya kutokufa

Namna gani tunaweza kusaidia wale wenye kuhuzunika juu walipoteza mupendwa wao?