Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Moyo

Moyo

Biblia inaonyeshaje kwamba moyo wa mfano ni yule mtu wa ndani, yaani mawazo, nia, sifa, na hisia zetu?

Zb 49:3; Met 16:9; Lu 5:22; Mdo 2:26

Tazama pia Kum 15:7; Zb 19:8

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Lu 9:​46-48—Yesu anawarekebisha mitume wake kwa sababu ya roho ya kujitakia makuu iliyo moyoni mwao

Kwa nini ni muhimu tuulinde moyo wetu?

1Nya 28:9; Met 4:23; Yer 17:9

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 6:​5-7—Uovu ulio katika moyo wa wanadamu unawafanya wawe wakatili na kusababisha Mungu alete Gharika

    • 1Fa 11:​1-10—Mfalme Sulemani anashindwa kuulinda moyo wake, anaoa wake wa kigeni ambao wanamfanya amwache Yehova

    • Mk 7:​18-23—Yesu anaeleza kwamba moyo ndio chanzo cha mambo yote yanayoweza kumtia mtu unajisi machoni pa Mungu

Tunawezaje kuulinda moyo wetu?

Zb 19:14; Met 3:​3-6; Lu 21:34; Flp 4:8

Tazama pia Ezr 7:​8-10; Zb 119:11

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Efe 6:​14-18; 1Th 5:8—Anapofafanua kuhusu vazi la silaha la kiroho, mtume Paulo anaeleza kwamba uadilifu, imani, na upendo ni sifa zinazoweza kuulinda moyo wetu wa mfano kama tu ambavyo bamba la kifuani linavyoulinda moyo halisi

Tunawezaje kujua ikiwa moyo wetu wa mfano una tatizo?

Met 21:​2-4; Ebr 3:12

Tazama pia Met 6:​12-14

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Nya 25:​1, 2, 17-27—Kwa muda fulani, Mfalme Amazia anafanya mambo yaliyo sawa machoni pa Mungu lakini si kwa moyo kamili; baadaye, anakuwa na kiburi na anakosa uaminifu na kupata matokeo mabaya

    • Mt 7:​17-20—Yesu anaonyesha kwamba kama tu jinsi mti mbaya unavyozaa matunda mabaya, ndivyo hali mbaya ya moyoni inavyotokeza matendo mabaya

Kwa nini tunapaswa kusitawisha moyo mzuri, na tunawezaje kufanya hivyo?

Met 10:8; 15:28; Lu 6:45

Tazama pia Zb 119:​97, 104; Ro 12:​9-16; 1Ti 1:5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Fa 20:​1-6—Anapokabili kifo, Mfalme Hezekia anamsihi Yehova amwonyeshe rehema kwa sababu alimtumikia kwa moyo kamili

    • Mt 21:​28-32—Yesu anatumia mfano kuonyesha kwamba hali ya moyoni ya mtu inafunuliwa zaidi kupitia mambo anayofanya, badala ya mambo anayosema atafanya

Kwa nini inafariji kujua kwamba Yehova anachunguza moyo wetu?

1Nya 28:9; Yer 17:10

Tazama pia 1Sa 2:3

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 16:​1-13—Nabii Samweli anatambua kwamba Yehova hafanyi maamuzi kwa kuangalia sura ya nje; badala yake, anaona ndani ya moyo wa mtu

    • 2Nya 6:​28-31—Sala ya Mfalme Sulemani aliyotoa wakati wa kuwekwa wakfu kwa hekalu la Yehova inaonyesha kwamba Mungu anasoma mioyo ya wanadamu kwa rehema na kwa usahihi