Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Unyenyekevu

Unyenyekevu

Yehova anawaonaje wanyenyekevu na wenye kiburi?

Zb 138:6; Met 15:25; 16:​18, 19; 22:4; 1Pe 5:5

Tazama pia Met 29:23; Isa 2:​11, 12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Nya 26:​3-5, 16-21—Mfalme Uzia anakuwa na kiburi; anavunja sheria ya Mungu na kukasirika anaposhauriwa; Mungu anampiga kwa ukoma

    • Lu 18:​9-14—Yesu anatumia mfano kueleza jinsi Yehova anavyohisi kuhusu sala ya mtu mwenye kiburi na ya mnyenyekevu

Yehova anatendaje mtu anapotubu kwa unyenyekevu na unyoofu?

2Nya 7:​13, 14; Zb 51:​2-4, 17

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Nya 12:​5-7—Mfalme Rehoboamu na wakuu wa Yuda wanajinyenyekeza mbele za Yehova, na wanaepuka msiba

    • 2Nya 32:​24-26—Mfalme mzuri Hezekia anakuwa na kiburi, lakini anapojinyenyekeza Yehova anamsamehe

Kuonyesha unyenyekevu kunatusaidiaje kuboresha uhusiano wetu na wengine?

Efe 4:​1, 2; Flp 2:3; Kol 3:​12, 13

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 33:​3, 4—Esau alikuwa amemkasirikia Yakobo lakini Yakobo alionyesha unyenyekevu wa pekee alipokutana na ndugu yake, na kwa sababu hiyo wanakuwa na amani tena

    • Amu 8:​1-3—Kwa unyenyekevu, Mwamuzi Gideoni anawaambia wanaume wa Efraimu kwamba wao ni bora kuliko yeye, hivyo hasira yao inapoa na wanaepuka kugombana

Yesu Kristo alifundishaje umuhimu wa unyenyekevu?

Mt 18:​1-5; 23:​11, 12; Mk 10:​41-45

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Isa 53:7 Flp 2:​7, 8—Kama ilivyotabiriwa, kwa unyenyekevu Yesu anakubali mgawo wa kuja duniani na hata kukabili kifo chenye maumivu makali na kinachoaibisha

    • Lu 14:​7-11—Yesu anatumia mpangilio wa kuketi kwenye karamu kuonyesha manufaa ya unyenyekevu

    • Yoh 13:​3-17—Yesu anawawekea mfano mzuri wafuasi wake kwa kufanya kwa unyenyekevu kazi ya hali ya chini ya kuosha miguu ya mitume wake

Kuwa na maoni yanayofaa kujihusu na kuwahusu wengine kunatusaidiaje kuwa wanyenyekevu?

Kwa nini unyenyekevu bandia hauna thamani?