Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Unyenyekevu

Unyenyekevu

Yehova anaonaka namna gani watu wanyenyekevu na watu wenye kiburi?

Zb 138:6; Mez 15:25; 16:​18, 19; 22:4; 1Pe 5:5

Ona pia Mez 29:23; Isa 2:​11, 12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 26:​3-5, 16-21—Mufalme Uzia anakuwa na kiburi; anavunja Sheria ya Mungu na kukasirika wakati wanamushauria; kisha Yehova anamupiga ukoma

    • Lu 18:​9-14—Yesu anatumia mufano juu ya kuonyesha namna Yehova anaonaka sala ya watu wenye kiburi, na ya wanyenyekevu

Yehova anafanyaka nini wakati mutu anajinyenyekeza na anatubu kwa moyo wote?

2Ny 7:​13, 14; Zb 51:​2-4, 17

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 12:​5-7—Mufalme Rehoboamu na wakubwa wa Yuda wanajinyenyekeza mbele ya Yehova, na ile inawasaidia waepuke magumu

    • 2Ny 32:​24-26—Mufalme muzuri Hezekia anakuwa na kiburi, lakini Yehova anamusamehe wakati anajinyenyekeza

Namna gani unyenyekevu unafanyaka tukuwe na uhusiano wa muzuri na wengine?

Efe 4:​1, 2; Flp 2:3; Kol 3:​12, 13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 33:​3, 4—Yakobo anaonyesha unyenyekevu wa ajabu kwa kumusalimia ndugu yake Esau mwenye alimukasirikia, ile inafanya kukuwe amani kati yao

    • Amu 8:​1-3—Kwa unyenyekevu Gideoni anaambia watu wa Efraimu kama wako wa maana kuliko yeye, ile inapunguza kasirani yao na inafanya wasikosane

Namna gani Yesu alifundisha ulazima wa kuwa na sifa ya unyenyekevu?

Mt 18:​1-5; 23:​11, 12; Mk 10:​41-45

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Isa 53:7; Flp 2:​7, 8—Vile unabii ulionyesha, kwa unyenyekevu Yesu anaitika kuya ku dunia na anaitika kufa kifo ya maumivu na ya haya

    • Lu 14:​7-11—Yesu anazungumuzia mufano wa viti vya ku karamu juu ya kuonyesha kama unyenyekevu ni sifa ya maana

    • Yoh 13:​3-17—Yesu anawekea wafuasi wake mufano muzuri wa unyenyekevu kwa kunawisha wanafunzi wake miguu

Namna gani kuwa na mawazo yenye kufaa juu yetu na juu ya wengine kutatusaidia tukuwe wanyenyekevu?

Juu ya nini unyenyekevu wa bongo hauna faida hata kidogo?