Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Utimilifu

Utimilifu

Utimilifu ni nini?

Zb 18:​23-25; 26:​1, 2; 101:​2-7; 119:​1-3, 80

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Law 22:​17-22—Yehova anaagiza kwamba wanyama wa dhabihu hawapaswi “kuwa na kasoro”; neno la Kiebrania linatafsiriwa “asiye na kasoro” linahusiana kwa ukaribu na neno linalotafsiriwa kuwa “utimilifu,” na hilo linadokeza kwamba utimilifu unahusisha kujitoa kikamili kwa Yehova

    • Ayu 1:​1, 4, 5, 8; 2:3—Maisha ya Ayubu yanaonyesha kwamba ili mtu awe mtimilifu anahitaji kumheshimu sana Yehova, kumwabudu kwa moyo wote, na kuepuka mambo ambayo ni mabaya machoni pa Yehova

Kwa nini tunahitaji utimilifu?

Ni nini kinachoweza kutuchochea kudumisha utimilifu wetu?

Tunawezaje kusitawisha na kudumisha utimilifu wetu?

Yos 24:​14, 15; Zb 101:​2-4

Tazama pia Kum 5:29; Isa 48:​17, 18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 31:​1-11, 16-33—Ayubu anadumisha utimilifu katika maisha yake ya kila siku kwa kuepuka maadili mapotovu na kwa kuwatendea wengine kwa fadhili na heshima. Anadumisha ibada yake ikiwa safi na anaepuka ibada ya sanamu na kupenda mali

    • Da 1:​6-21—Ingawa wanazungukwa na watu wasiomwabudu Yehova, Danieli na rafiki zake watatu wanadumisha utimilifu hata wanapochagua vyakula

Ikiwa mtu anafanya mfululizo wa mambo mabaya, je, anaweza kuwa mtimilifu tena?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 9:​2-5; Zb 78:​70-72—Kwa kuwa Mfalme Daudi alitubu dhambi zake na kupata msamaha, Yehova anamwona Daudi kuwa mtu aliyeishi maisha ya utimilifu

    • Isa 1:​11-18—Ingawa Yehova anawashutumu watu wake kuwa wanafiki na waliojaa dhambi, anaahidi kwamba anaweza kuwasafisha kikamili ikiwa wanatubu na kugeuka