Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uaminifu-Mushikamanifu

Uaminifu-Mushikamanifu

Uaminifu-Mushikamanifu njo nini?

Zb 18:​23-25; 26:​1, 2; 101:​2-7; 119:​1-3, 80

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Law 22:​17-22—Yehova anaagiza kama munyama mwenye anatolewa zabihu anapaswa kuwa “mwenye hana kasoro;” neno ya Kiebrania yenye inatafsiriwa “mwenye hana kasoro” inapatana kabisa na neno yenye inatafsiriwa “uaminifu-mushikamanifu;” ile inaonyesha kama kuwa muaminifu-mushikamanifu inamaanisha kuwa bila kasoro, ao kujitoa kabisa kwa Yehova

    • Yob 1:​1, 4, 5, 8; 2:3—Maisha ya Yobu inaonyesha kama juu mutu akuwe muaminifu-mushikamanifu, anapaswa kumuheshimia kabisa Yehova, kumuabudu kwa moyo wote, na kuepuka mambo yenye anachukia

Juu ya nini tuko na lazima ya kuwa waaminifu-washikamanifu?

Nini njo inaweza kutusaidia tuendelee kuwa waaminifu-washikamanifu?

Namna gani tunaweza kukomalisha sifa ya uaminifu-mushikamanifu na kuendelea kuionyesha?

Yos 24:​14, 15; Zb 101:​2-4

Ona pia Kum 5:29; Isa 48:​17, 18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yob 31:​1-11, 16-33—Mu maisha yake yote Yobu anaonyesha uaminifu-mushikamanifu kwa kuepuka uasherati na kwa kutendea wengine kwa fazili na kwa heshima. Anaendelea kumuabudu Yehova kwa moyo safi na anaepuka ibada ya sanamu na kupenda vitu vya kimwili

    • Da 1:​6-21—Hata kama wanazungukwa na watu wenye hawako waamini, Danieli na marafiki wake watatu wanaendelea kuwa waaminifu-washikamanifu hata wakati inaomba waamue ni chakula gani njo watakula

Kama mutu anafanya makosa mingi, anaweza tena kuwa muaminifu-mushikamanifu?

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 9:​2-5; Zb 78:​70-72—Juu Mufalme Daudi alitubu zambi zake na alisamehewa, Yehova anamuona kuwa mwanaume mwenye alikuwa muaminifu-mushikamanifu mu maisha yake

    • Isa 1:​11-18—Hata kama Yehova anaona watu wake kuwa wanafiki na wenye kuyala zambi, anaahidi kuwasafisha kabisa kama wanatubu na kubadilisha njia zao