Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kupenda Mali

Kupenda Mali

Je, Biblia inafundisha kwamba ni vibaya kuwa na pesa au vitu vya kimwili?

Mhu 7:12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 3:​11-14—Yehova anambariki Mfalme Sulemani kwa kumpatia utajiri mwingi kwa sababu ni mnyenyekevu

    • Ayu 1:​1-3, 8-10—Ingawa Ayubu alikuwa na mali nyingi sana, alijulikana zaidi kwa kuwa mtu mtimilifu

Kwa nini kuwa na mali na utajiri hakutufanyi turidhike au kuwa na amani ya akili?

Ni wakati gani utajiri hauwezi kutusaidia hata kidogo?

Ni hatari gani kubwa zaidi inayoletwa na pesa na mali?

Nguvu za utajiri zinawezaje kutudanganya?

Met 11:​4, 18, 28; 18:11; Mt 13:22

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mdo 8:​18-24—Kwa upumbavu Simoni anaamini kwamba anaweza kutumia pesa kununua pendeleo katika kutaniko la Kikristo

Kupenda pesa kunaweza kutugharimu nini?

Mt 6:​19-21; Lu 17:​31, 32

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mk 10:​17-23—Mwanamume kijana tajiri ambaye anapenda sana mali zake anapoteza pendeleo la kuwa mfuasi wa Yesu

    • 1Ti 6:​17-19—Mtume Paulo anawaonya Wakristo matajiri waepuke majivuno, ambayo yanaweza kufanya wapoteze kibali cha Mungu

Kupenda mali kunawezaje kudhoofisha imani yetu na kusababisha tupoteze kibali cha Mungu?

Kum 8:​10-14; Met 28:20; 1Yo 2:​15-17

Tazama pia Zb 52:​6, 7; Amo 3:​12, 15; 6:​4-8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ayu 31:​24, 25, 28—Ayubu anaona waziwazi hatari ya kutumaini mali, kwa sababu kufanya hivyo ni kama kumkana Mungu

    • Lu 12:​15-21—Yesu anatoa onyo kuhusu kupenda mali kwa kumzungumzia mwanamume tajiri ambaye si tajiri kwa Mungu

Tunawezaje kuridhika na vitu tulivyo navyo?

Ni hazina gani ambazo ni muhimu zaidi kuliko vitu vya kimwili, na kwa nini?

Met 3:​11, 13-18; 10:22; Mt 6:​19-21

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Hag 1:​3-11—Kupitia nabii Hagai, Yehova anaeleza kwamba anawanyima watu Wake hata baraka za kimwili kwa sababu wanatanguliza nyumba zao na starehe badala ya kujenga upya hekalu Lake takatifu

    • Ufu 3:​14-19—Yesu analikemea kutaniko la Laodikia kwa kutanguliza mali badala ya kuthamini zaidi utumishi wao kwa Mungu

Kwa nini tunapaswa kutumaini kwamba Yehova atatuandalia mahitaji yetu ya kimwili?