Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Rehema

Rehema

Rehema inatia ndani nini?

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Zb 51:​1, 2—Wakati Mufalme Daudi anamuomba Yehova amuonyeshe rehema, anamuomba amusamehe zambi zake

    • Lu 10:​29-37—Yesu anafundisha somo kuhusu rehema kwa kuzungumuzia mufano wa Musamaria mwenye alihangaikia Muyahudi na kumutendea kwa fazili

Juu ya nini wanadamu wote wako na lazima ya rehema?

Kuhusu rehema, Yehova anatuwekea mufano gani?

Kut 34:6; Ne 9:17; Zb 103:8; 2Ko 1:3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yob 42:​1, 2, 6-10; Yak 5:11—Yehova anaonyesha Yobu rehema na anamufundisha akuwe pia na rehema

    • Lu 15:​11-32—Yesu anatusaidia tuelewe namna Yehova anakuwaka na rehema kwa kuzungumuzia mufano wa baba mwenye anatendea muzuri mutoto mwenye anatubu

Juu ya nini Yehova anatuonyeshaka Rehema?

Namna gani zabihu ya Kristo inatusaidia tupate musamaha wa zambi zetu?

Juu ya nini tunapaswa kuomba rehema na kuendelea kuwa wenye shukrani juu ya ayo?

Lu 11:​2-4; Ebr 4:16

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Zb 51:​1-4—Mufalme Daudi iko mwenye kuvunjika moyo juu ya zambi zenye alifanya na anamulilia Yehova amuonyeshe rehema

    • Lu 18:​9-14—Yesu anatumia mufano juu ya kukazia kama Yehova anaonyeshaka rehema kwa wale wenye wanatambua uzaifu wao kwa unyenyekevu

Juu ya nini hata wale wenye walifanya zambi nzito wanaweza kutumainia kuonyeshwa rehema?

Kum 4:​29-31; Isa 55:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 33:​9-13, 15—Hata kama Manase ni mufalme muovu sana, anatubu na kumulilia Yehova amuonyeshe rehema; kisha anarudishwa kuwa mufalme na anafikia kuonyesha kupitia matendo yake kama amebadilika kabisa

    • Yon 3:​4-10—Hata kama Waninawi ni watu wenye jeuri sana, wanatubu na Mungu anawaonyesha rehema

Juu ya nini ni jambo ya maana kuungama zambi zetu kwa Yehova na kubadilisha matendo yetu juu Yehova atuonyeshe rehema?

Rehema ya Yehova haituzuie kupata azabu ao matokeo ya zambi zetu

Juu ya nini tunapaswa kuwa wenye rehema?

Kama hatuonyeshe rehema, ile inaweza kuwa na matokeo gani juu ya uhusiano wetu pamoya na Yehova?

Mt 9:13; 23:23; Yak 2:13

Ona pia Mez 21:13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 18:​23-35—Kupitia mufano, Yesu anaonyesha kama mutu mwenye haonyeshe wengine rehema, Yehova pia hatamuonyesha rehema

    • Lu 10:​29-37—Yesu anatumia mufano juu ya kuonyesha kama yeye na Baba yake wanachukia wale wenye hawaonyeshe rehema, lakini wanafurahia wale wenye kuonyesha rehema, sawa ule Musamaria

Yehova anatendeaka namna gani watu wenye kuonyesha rehema?