Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Pesa

Pesa

Kwa nini kupenda pesa ni hatari?

Tazama “Kupenda Mali

Biblia inaonyeshaje kwamba si vibaya kutafuta pesa kwa ajili ya kutunza familia?

Mhu 7:12; 10:19; Efe 4:28; 2Th 3:10; 1Ti 5:​8, 18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 31:​38-42—Ili kuiandalia familia yake, Yakobo anamfanyia kazi kwa unyoofu baba mkwe wake, Labani, ambaye anamtendea isivyo haki; hata hivyo, Yehova anabariki jitihada za Yakobo za kuiandalia familia yake

    • Lu 19:​12, 13, 15-23—Yesu anatoa mfano unaoonyesha kwamba lilikuwa zoea la kawaida katika siku zake kwa mtu kuwekeza pesa ili apate pesa zaidi

Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kutuongoza kuhusu kukopa na kukopesha pesa?

Kwa nini ni vizuri kuepuka madeni yasiyo ya lazima?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ne 5:​2-8—Baadhi ya Waisraeli katika siku za Nehemia waliwatendea bila fadhili watu waliowakopesha

    • Mt 18:​23-25—Mfano wa Yesu unatukumbusha kwamba mkopaji anayeshindwa kulipa anaweza kuadhibiwa

Ni tahadhari gani ambazo mtu anahitaji kuchukua kabla ya kuingia katika makubaliano ya biashara na mtu ambaye ni mwabudu mwenzake, mtu wa ukoo, au mtu ambaye si mwamini?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 23:​14-20—Abrahamu alinunua mbele ya mashahidi shamba na pango ambalo angetumia kumzika Sara; huenda alifanya hivyo ili kuzuia kutoelewana au kutokea kwa ugomvi wakati ujao

    • Yer 32:​9-12—Yeremia anaponunua shamba kutoka kwa mwana wa ndugu ya baba yake, anaandika hati, anatengeneza nakala ya hati hiyo, na kulipa pesa mbele za mashahidi

Kwa nini ni jambo la hekima kupanga bajeti ya matumizi ya pesa kwa uangalifu?

Kwa nini Wakristo hawapaswi kuruhusu kutoelewana kuhusu pesa kusababishe migawanyiko kutanikoni?

Tunawezaje kutumia pesa zetu katika njia itakayotuletea furaha ya kweli?