Utii
Kwa nini ni muhimu kutii?
Kut 19:5; Kum 10:12, 13; Mhu 12:13; Yak 1:22
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
1Sa 15:17-23—Nabii Samweli anamkemea Mfalme Sauli kwa kutomtii Yehova; kisha Samweli anakazia umuhimu wa kutii
-
Ebr 5:7-10—Ingawa sikuzote Yesu amekuwa Mwana mkamilifu wa Mungu, alijifunza kuwa mtiifu alipotendewa kwa njia isiyofaa akiwa duniani
-
Mkristo anapaswa kufanya nini ikiwa wanadamu wenye mamlaka wanamwambia asimtii Mungu?
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Da 3:13-18—Hata walipohatarisha uhai wao, Waebrania watatu waaminifu walikataa kuinamia sanamu iliyosimamishwa na Mfalme Nebukadneza
-
Mt 22:15-22—Yesu anaeleza kwamba wafuasi wake wanawatii wenye mamlaka isipokuwa tu wenye mamlaka wawaambie wasimtii Yehova Mungu
-
Mdo 4:18-31—Hata walipoamriwa na wenye mamlaka waache kuhubiri, mitume waliendelea kuhubiri kwa ujasiri
-
Ni lazima tufanye nini ikiwa tunataka kuendelea kutii amri za Yehova?
Kum 6:1-5; Zb 112:1; 1Yo 5:2, 3
Tazama pia Zb 119:11, 112; Ro 6:17
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Ezr 7:7-10—Kuhani mwaminifu Ezra anatayarisha moyo wake ili aweze kuweka mfano mzuri wa kutii amri za Mungu na kuwafundisha wengine
-
Yoh 14:31—Yesu anafunua kwa nini anatenda kama vile Baba yake alivyomwamuru
-
Ni nini kinachopaswa kutuchochea kumtii Yehova na Yesu?
Utii wetu unaonyeshaje imani yetu?
Ro 1:5; 10:16, 17; Yak 2:20-23
Tazama pia Kum 9:23
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Mwa 6:9-22; Ebr 11:7—Noa anaonyesha imani yake kwa kujenga safina kama tu Yehova anavyomwamuru, ‘ndivyo anavyofanya’
-
Ebr 11:8, 9, 17—Abrahamu anaonyesha imani yake kwa kutii amri za Yehova, kutia ndani kuondoka Uru, na kumtoa mwana wake
-
Yehova anatupa baraka gani tunapotii?
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Law 26:3-6—Yehova anaahidi kuwabariki na kuwatunza wale wanaomtii
-
Hes 13:30, 31; 14:22-24—Kalebu anaonyesha roho ya utii, na hivyo anapata baraka za Yehova
-
Ni nini kitakachotokea tusipotii?
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Mwa 2:16, 17; 3:17-19—Kwa sababu hawamtii Yehova Mungu, Adamu na Hawa wanapoteza Paradiso, ukamilifu, na uzima wa milele
-
Kum 18:18, 19; Mdo 3:12, 18, 22, 23—Yehova anatabiri kuja kwa Nabii mkuu zaidi ya Musa na kufunua kwamba kutomtii Nabii huyo kutasababisha matokeo mabaya sana
-
Yud 6, 7—Malaika waasi na watu wa Sodoma na Gomora wanamkasirisha Yehova kwa sababu ya kutotii
-
Kwa nini tunapaswa kumtii Yesu Kristo?
-
Simulizi la Biblia linalohusika:
-
Yoh 12:46-48; 14:24—Yesu anaeleza kwamba kutotii maneno yake kutaongoza kwenye hukumu kali
-
Kwa nini Wakristo wanawatii wale wanaoongoza kutanikoni?
Kwa nini mke Mkristo anapaswa kujitiisha kwa mume wake?
Kwa nini watoto wawatii wazazi wao?
-
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
-
Mwa 37:3, 4, 8, 11-13, 18—Kijana Yosefu anamtii baba yake na kusafiri kwenda kuwaona ndugu zake hata ingawa wanamchukia
-
Lu 2:51—Yesu anaendelea kuwatii Yosefu na Maria hata ingawa yeye ni mkamilifu na wazazi wake wa kibinadamu si wakamilifu
-
Kwa nini ni jambo la hekima kumtii mwajiri wetu hata ikiwa hatuonwi na wengine?
Kwa nini Wakristo wanatii serikali?