Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Uzee; Wenye Kuzeeka

Uzee; Wenye Kuzeeka

Mambo inakuwaka namna gani wakati mutu anazeeka?

Zb 71:9; 90:10

Ona pia “Kitulizo—Mipaka yenye inatokana na magonjwa ao uzee

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Muh 12:​1-8—Mu maneno ya mufano, Mufalme Sulemani, anazungumuzia mambo yenye inafikiaka mutu wakati anazeeka; sawa vile kutokuona muzuri (“mabibi wenye kuangalia kupitia madirisha wanaona giza”) na kutokusikia muzuri (“mabinti wa wimbo wanazimia”)

Wenye kuzeeka wanaweza kuendelea kuwa na furaha ijapokuwa magumu na mipaka fulani yenye wako nayo juu ya uzee?

2Ko 4:​16-18; Yak 1:​2-4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 12:​2, 23—Nabii Samweli mwenye kuzeeka anajua ulazima wa kuendelea kusali kwa ajili ya watu wa Yehova

    • 2Sa 19:​31-39—Mufalme Daudi anapenda kuonyesha shukrani kwa Barzilai mwenye kuzeeka, juu alimusaidia; na kwa kiasi Barzilai anakubali kama hataweza kufanya mambo yenye inapita uwezo wake

    • Zb 71:​9, 18—Mufalme Daudi anaogopa kama Yehova hataendelea kumutumikisha juu alishazeeka; kwa hiyo, anamuomba Yehova asiache kumutumikisha, lakini amupatie nguvu juu afundishe kizazi yenye kuya juu ya Yehova

    • Lu 2:​36-38—Nabii mwanamuke Ana, mujane mwenye kuzeeka, anabarikiwa juu ya kazi yake ya kujitolea na ya ushikamanifu

Namna gani Yehova anahakikishia wenye kuzeeka kama wako wa maana kwake?

Zb 92:​12-14; Mez 16:31; 20:29; Isa 46:4; Tit 2:​2-5

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 12:​1-4—Wakati Abrahamu iko na miaka 75, Yehova anamupatia mugao wenye unamuomba atoke mu inchi yake

    • Da 10:​11, 19; 12:13—Malaika anamutembelea Danieli mwenye iko na miaka 90 juu ya kumuhakikishia kama iko wa maana sana kwa Yehova na kama Yehova atamubariki juu ya uaminifu wake

    • Lu 1:​5-13—Yehova anamubariki Zekaria na Elizabeti wenye kuzeeka kwa kuwapatia mutoto, Yohana, kupitia muujiza

    • Lu 2:​25-35—Yehova anamupatia Simeoni mwenye kuzeeka, pendeleo ya kuona mutoto mwenye atakuwa Masiya; Simeoni anasema maneno ya unabii juu ya ule mutoto

    • Mdo 7:​23, 30-36—Nabii Musa iko na miaka 80 wakati Yehova anamupatia daraka ya kuongoza watu wake, Israeli

Namna gani tunapaswa kutendea watumishi waaminifu wa Yehova wenye kuzeeka?

Law 19:32; 1Ti 5:1

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Namna gani Wakristo wanaweza kusaidia wenye kuzeeka mu kutaniko?