Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Waangalizi

Waangalizi

Waangalizi Wakristo wanapaswa kufikia sifa zipi kwa kiwango kinachofaa ili wastahili kutumikia?

Waangalizi kutanikoni wanahitaji kuwa mfano mzuri katika kutimiza matakwa gani mengine ya Kikristo?

Watumishi wa huduma wanapaswa kufikia sifa zipi kwa kiwango kinachofaa ili wastahili kutumikia?

Roho ya Mungu inahusikaje akina ndugu wanapowekwa rasmi kuwa waangalizi?

Mdo 20:28

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mdo 13:​2-5; 14:23—Waangalizi wanaosafiri, Paulo na Barnaba, wanawaweka rasmi wanaume wanaotegemeka kuwa wazee katika makutaniko mbalimbali; leo, waangalizi wa mzunguko wanafanya vivyo hivyo, wanamwomba Yehova roho takatifu na kufuata kwa makini Maandiko yaliyoongozwa na roho, ambayo yanataja sifa za kustahili

    • Tit 1:​1, 5—Tito anakabidhiwa kazi ya kutembelea makutaniko mbalimbali, na kuwaweka rasmi wazee

Kutaniko ni mali ya nani, na lilinunuliwa kwa gharama gani?

Kwa nini waangalizi wanafafanuliwa kuwa wale wanaohudumu, au wanaowatumikia wengine?

Kwa nini ni lazima waangalizi waendelee kuwa wanyenyekevu?

Flp 1:1; 2:​5-8; 1Th 2:​6-8; 1Pe 5:​1-3, 5, 6

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mdo 20:​17, 31-38—Mtume Paulo anawakumbusha wazee kutoka Efeso kuhusu kazi aliyofanya kwa miaka mingi kwa ajili yao, nao wanaonyesha uthamini kwa ajili ya upendo aliowaonyesha

Mwangalizi Mkristo anaonaje mwongozo unaotoka kwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara”?

Ni njia gani bora ambayo wazee wanaweza kutumia kuwafundisha wengine?

1Ti 4:12; 1Pe 5:​2, 3

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ne 5:​14-16—Kwa sababu anamheshimu sana Yehova, Gavana Nehemia anakataa kutumia vibaya mamlaka aliyo nayo juu ya watu wa Mungu, hata anakataa mambo anayostahili kupata

    • Yoh 13:​12-15—Yesu anawafundisha wafuasi wake kwa kuwawekea kielelezo cha kuwa wanyenyekevu

Mchungaji Mkristo anawezaje kuonyesha upendo kwa kila mtu kutanikoni?

Wazee wanawasaidiaje wale walio wagonjwa kiroho?

Wazee wana jukumu gani wanapofundisha?

Kwa nini ni lazima wazee wajitahidi sana kuhakikisha kwamba kutaniko ni safi kiadili?

Wazee wanajitahidi kuwazoeza akina nani?

2Ti 2:​1, 2

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mt 10:​5-20—Yesu anawazoeza mitume wake 12 kabla ya kuwatuma katika kazi ya kuhubiri

    • Lu 10:​1-11—Yesu anawapatia wanafunzi wake 70 maagizo muhimu kabla ya kuwatuma katika kazi ya kuhubiri

Ni nini kitakachowasaidia wazee kushughulikia majukumu yao mengi?

1Pe 5:​1, 7

Tazama pia Met 3:​5, 6

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 3:​9-12—Mfalme Sulemani anasali kwa Yehova apate utambuzi na uelewaji anaohitaji ili kuwahukumu watu wa Yehova

    • 2Nya 19:​4-7—Mfalme Yehoshafati anawaweka rasmi waamuzi katika majiji ya Yuda, na kuwakumbusha kwamba Yehova atakuwa pamoja nao wanapotimiza mgawo huo muhimu

Kutaniko linapaswa kuwaonaje waangalizi waaminifu?

1Th 5:​12, 13; 1Ti 5:17; Ebr 13:​7, 17

Tazama pia Efe 4:​8, 11, 12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mdo 20:37—Wazee wa Efeso hawasiti kuonyesha jinsi wanavyompenda mtume Paulo

    • Mdo 28:​14-16—Mtume Paulo anaposafiri kwenda Roma, akina ndugu kutoka katika jiji hilo wanasafiri kilomita 65 hivi ili kukutana naye katika Soko la Apio, na kumtia moyo sana