Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Waangalizi; Wazee

Waangalizi; Wazee

Waangalizi Wakristo wanapaswa kutimiza sifa gani?

Ni mu njia gani zingine wazee Wakristo wanapaswa kuwa mufano muzuri?

Watumishi wa huduma wanapaswa kutimiza sifa gani?

Juu ya nini tunaweza kusema kama roho ya Mungu njo inawekaka wazee?

Mdo 20:28

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 13:​2-5; 14:23—Waangalizi wenye kusafiri, Paulo na Barnaba, wanaweka wazee mu makutaniko; waangalizi wa leo wanafanya vilevile pia, wanasali na kufikiria sifa zenye Maandiko inasema mutu anapaswa kutimiza juu akuwe muzee

    • Tit 1:​1, 5—Tito anafanya safari mu makutaniko mbalimbali juu ya kuweka wazee

Kutaniko ni ya nani, na iliuzwa ku bei gani?

Juu ya nini Biblia inasema kama wazee ni watumishi?

Juu ya nini waangalizi wanapaswa kuendelea kuwa wanyenyekevu?

Flp 1:1; 2:​5-8; 1Te 2:​6-8; 1Pe 5:​1-3, 5, 6

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Mdo 20:​17, 31-38—Mutume Paulo anakumbusha wazee wa Efeso mambo yenye aliwafanyia, na wale wazee wanamushukuru juu ya upendo wenye aliwaonyesha

Mwangalizi Mukristo anaonaka namna gani muongozo wenye “mutumwa muaminifu na mwenye busara” anatoa?

Ni njia gani ya muzuri yenye mwangalizi anapaswa kutumia juu ya kufundisha wengine?

1Ti 4:12; 1Pe 5:​2, 3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Ne 5:​14-16—Juu gavana Nehemia anamuheshimia sana Yehova, anakatala kutumia mubaya mamlaka yenye iko nayo juu ya watu wa Mungu; anakatala hata kupokea mambo yenye iko na haki ya kupewa

    • Yoh 13:​12-15—Yesu anafundisha wafuasi wake kwa kuwawekea mufano wa unyenyekevu

Namna gani muzee Mukristo anaweza kuonyesha kama anapenda kila mutu mu kutaniko?

Namna gani wazee wanasaidiaka wale wenye kuwa na lazima ya kurudisha tena urafiki wao pamoya na Yehova?

Muzee anakuwaka na daraka gani wakati iko nafundisha?

Juu ya nini wazee wanapaswa kujikaza sana juu kutaniko iendelee kuwa safi?

Wazee wanapatiaka wengine mazoezi gani?

2Ti 2:​1, 2

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mt 10:​5-20—Yesu anazoeza mitume wake 12 mbele awatume mu kazi ya kuhubiri

    • Lu 10:​1-11—Yesu anapatia wanafunzi wake 70 maagizo mbele awatume mu kazi ya kuhubiri

Nini njo itasaidia wazee watimize madaraka yao mbalimbali?

1Pe 5:​1, 7

Ona pia Mez 3:​5, 6

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 3:​9-12—Mufalme Sulemani anamuomba Yehova utambuzi na uelewaji ili aweze kuhukumu watu wa Mungu

    • 2Ny 19:​4-7—Mufalme Yehoshafati anaweka waamuzi mu miji ya Yuda, na anawakumbusha kama Yehova atakuwa pamoya nao mu ile mugao ya maana

Kutaniko inapaswa kuona namna gani waangalizi waaminifu?

1Te 5:​12, 13; 1Ti 5:17; Ebr 13:​7, 17

Ona pia Efe 4:​8, 11, 12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 20:37—Wazee wa Efeso hawakusita kuonyesha kama wanamupenda mutume Paulo

    • Mdo 28:​14-16—Wakati mutume Paulo iko mu safari ya kuenda Roma, ndugu wa mu ile muji wanafanya safari ya kilometre 65 hivi mupaka ku Soko ya Apio juu ya kumukaribisha na kumutia moyo