Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Wazazi

Wazazi

Ni baadhi ya sababu gani zilizofanya Yehova aanzishe mpango wa ndoa?

Wazazi wanapaswa kuwaonaje watoto wao?

Zb 127:​3-5; 128:3

Tazama pia “Watoto; Vijana

Wazazi wana wajibu gani kuhusiana na watoto wao?

Kum 6:​6, 7; 11:​18, 19; Met 22:6; 2Ko 12:14; 1Ti 5:8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 1:​1-4—Elkana anaipeleka familia yake huko Shilo kwa ajili ya sherehe, hivyo anahakikisha kwamba kila mtoto anaweza kushiriki

    • Lu 2:​39, 41—Yosefu na Maria wana desturi ya kusafiri pamoja na watoto wao kutoka Nazareti kwenda Yerusalemu kwa ajili ya sherehe ya Pasaka

Kuna manufaa gani ya kuwazoeza watoto katika njia za Yehova?

Met 1:​8, 9; 22:6

Tazama pia 2Ti 3:​14, 15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 2:​18-21, 26; 3:19—Wazazi wa Samweli wanamtoa mwana wao atumikie kwenye hema la ibada, lakini wanamtembelea mvulana huyo kwa ukawaida na kumpelekea vitu anavyohitaji; baadaye anakuwa mwanamume wa kiroho mwenye sifa za pekee

    • Lu 2:​51, 52—Yesu anaendelea kujitiisha kwa wazazi wake ingawa si wakamilifu

Wazazi wanaweza kupata wapi mwongozo wa kuwalea watoto wao?

Kum 6:​4-9; Efe 6:4; 2Ti 3:​14-17

Tazama pia Zb 127:1; Met 16:3

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Amu 13:​2-8—Baada ya kuambiwa kwamba mke wake atapata mwana kimuujiza, Manoa anaomba mwongozo zaidi wa jinsi ya kumlea mtoto huyo

    • Zb 78:​3-8—Yehova anataka wazazi washiriki na watoto wao ujuzi wa Kimaandiko walio nao

Hata ingawa mtoto analelewa katika familia inayompenda Mungu, kwa nini huenda akaacha kumtumikia Yehova?

Eze 18:​1-13, 20

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 6:​1-5; Yud 6—Licha ya kutumia muda mwingi pamoja na Yehova mbinguni, wana wengi wa kiroho wa Mungu walichagua kumwasi

    • 1Sa 8:​1-3—Ingawa Samweli ni nabii mwaminifu na mwadilifu, wana wa Samweli hawakuwa wanyoofu na walipokea rushwa

Wazazi wanapaswa kuanza lini kuwafundisha watoto wao njia za Mungu?

2Ti 3:15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kum 29:​10-12, 29; 31:12; Ezr 10:1—Watoto wanashiriki pia kwenye makusanyiko ya kidini ili kujifunza kuhusu njia za Yehova

    • Lu 2:​41-52—Yosefu na Maria wana desturi ya kuwapeleka watoto wao, kutia ndani Yesu, kwenye sherehe ya Pasaka katika hekalu jijini Yerusalemu

Wazazi wanapaswa kufuata mfano gani wanapowalinda watoto wao kutokana na watu ambao huenda wakawadhuru?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kut 19:4; Kum 32:​11, 12—Yehova anajilinganisha na tai ambaye anawabeba, anawalinda, na kuwatunza watoto wake

    • Isa 49:15—Yehova anaahidi kuwatunza na kuwalinda watumishi wake kwa njia inayozidi huruma ambayo mama anayenyonyesha humwonyesha mtoto wake

    • Mt 2:​1-16—Shetani anajaribu kumwangamiza mtoto Yesu kwa kuwaongoza wanajimu wapagani kwa mfalme mwovu Herode, lakini Yehova anamlinda mwana Wake kwa kumwongoza Yosefu ahamishe familia yake kwenda Misri

    • Mt 23:37—Yesu analinganisha tamaa yake ya kuwasaidia watu wake na jinsi kuku anavyowakusanya vifaranga wake na kuwalinda chini ya mabawa yake

Kwa nini wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao kuhusu masuala ya ngono?

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Law 15:​2, 3, 16, 18, 19; Kum 31:​10-13—Sheria ya Musa inazungumzia waziwazi kuhusu masuala ya ngono, na Yehova anaagiza watoto wawepo inaposomwa kwa sauti

    • Zb 139:​13-16—Mtunga zaburi Daudi anamsifu Yehova kwa jinsi alivyoumba mwili wa mwanadamu kwa njia yenye kustaajabisha, kutia ndani uwezo wa kupata watoto

    • Met 2:​10-15—Ujuzi na hekima kutoka kwa Yehova unaweza kutulinda kutokana na wale wanaofanya mambo mabaya na wenye hila

Kwa nini nidhamu inapaswa kutolewa kwa njia ya upendo?

Met 13:24; 29:17; Yer 30:11; Efe 6:4

Tazama pia Zb 25:8; 145:9; Kol 3:21

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Zb 32:​1-5—Ingawa Mfalme Daudi anahisi uzito wa nidhamu ya Yehova, anafarijika kujua kwamba Yehova huwasamehe wale wanaotubu kikweli dhambi zao

    • Yon 4:​1-11—Nabii Yona anazungumza na Yehova kwa hasira na bila heshima; hata hivyo, kwa subira Yehova anamfundisha kuhusu rehema

Kwa nini nidhamu inaweza kuonwa kuwa wonyesho wa upendo?