Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Wazazi

Wazazi

Ni sababu gani zenye zilifanyaka Yehova aanzishe ndoa?

Namna gani wazazi wanapaswa kuona watoto wao?

Zb 127:​3-5; 128:3

Ona pia “Watoto; Vijana

Wazazi wanapaswa kufanyia nini watoto wao?

Kum 6:​6, 7; 11:​18, 19; Mez 22:6; 2Ko 12:14; 1Ti 5:8

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 1:​1-4—Elkana anapeleka familia yake Shilo kwa ajili ya sikukuu, na anakamata mipango juu kila mutoto aweze kutoa zabihu

    • Lu 2:​39, 41—Kama kawaida, Yosefu na Maria wanasafiri na watoto wao kutoka Nazareti kuenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pasaka

Kuzoeza watoto mu njia za Yehova kunaletaka faida gani?

Mez 1:​8, 9; 22:6

Ona pia 2Ti 3:​14, 15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Sa 2:​18-21, 26; 3:19—Wazazi wa Samweli wanatoa mutoto wao juu atumike ku tabenakulo, lakini wanamutembelea kila mara na wanamusaidia kutimiza mahitaji yake; wakati Samweli anakomala anakuwa mutu wa kiroho na anamutumikia Yehova kwa uaminifu

    • Lu 2:​51, 52—Yesu anaendelea kutii wazazi wake hata kama hawakamilike

Wazazi wanaweza kupata wapi muongozo juu ya kukomalisha watoto wao?

Kum 6:​4-9; Efe 6:4; 2Ti 3:​14-17

Ona pia Zb 127:1; Mez 16:3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Amu 13:​2-8—Kisha kuambiwa kama bibi yake atazala mutoto, Manoa anaomba maagizo juu ya namna ya kukomalisha ule mutoto

    • Zb 78:​3-8—Yehova anapenda wazazi wafundishe watoto wao mambo yenye wamejifunza mu Biblia

Hata kama mutoto anakomalia mu familia yenye kumupenda Mungu, nini njo inaweza kufanya afikie kumuacha Yehova?

Eze 18:​1-13, 20

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 6:​1-5; Yud 6—Hata kama walipitisha miaka mingi sana pamoya na Yehova mbinguni, malaika wengi waliamua kumuasi

    • 1Sa 8:​1-3—Hata kama Samweli ni nabii muaminifu na mwenye haki, watoto wake wanafikia kuwa wadanganyifu na wenye kupotoka

Wazazi wanapaswa kuanza kufundisha watoto wao njia za Mungu wakati gani?

2Ti 3:15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Ni mifano gani inaweza kusaidia wazazi walinde watoto wao juu wengine wasiwatendee mubaya?

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Kut 19:4; Kum 32:​11, 12—Yehova anajilinganisha na tai, mwenye anabebaka, kulinda, na kuhangaikia vitoto vyake

    • Isa 49:15—Yehova anaahidi kama atahangaikia na kulinda watumishi wake kwa huruma, kupita hata vile mama anahangaikiaka mutoto wake

    • Mt 2:​1-16—Shetani anajaribu kumuua mutoto Yesu kwa kuongoza watu wenye elimu ya nyota waende kwa mufalme muovu Herode, lakini Yehova anamulinda mwana wake kwa kumuongoza Yosefu na familia yake waende Misri

    • Mt 23:37—Yesu anafananisha nia yake ya kusaidia watu wake na namna kuku anakusanyaka vitoto vyake chini ya mabawa

Juu ya nini wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao kuhusu mambo ya ngono?

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Law 15:​2, 3, 16, 18, 19; Kum 31:​10-13—Sheria ya Musa inasema mambo waziwazi juu ya ngono, na Yehova anaomba watoto wakuwe pale wakati ile sheria inasomwa

    • Zb 139:​13-16—Daudi, muandikaji wa zaburi, anamusifu Yehova juu ya namna aliumbaka mwili wa mwanadamu na namna alipatiaka wanadamu uwezo wa kuzala watoto

    • Mez 2:​10-15—Ujuzi na hekima kutoka kwa Yehova vinaweza kutulinda juu watu wenye kupotoka wasitutendee mubaya

Juu ya nini wazazi wanapaswa kutolea watoto wao nizamu kwa upendo?

Mez 13:24; 29:17; Yer 30:11; Efe 6:4

Ona pia Zb 25:8; 145:9; Kol 3:21

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Zb 32:​1-5—Hata kama Daudi anaona kuwa nizamu ya Yehova inamulemea, kujua kama Yehova anakuwaka anasamehe wenye wanatubu kikweli kunamutuliza

    • Yon 4:​1-11—Nabii Yona iko naongea na Yehova kwa kasirani na bila heshima; hata vile, Yehova anamufundisha rehema kwa uvumilivu

Juu ya nini tunaweza kusema kama kupatia mutoto nizamu ni kumupenda?