Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mateso

Mateso

Juu ya nini Wakristo wanapaswa kutazamia kama watatesa?

Wakati wanatutesa juu ya nini tunapaswa kutafuta musaada kwa Yehova?

Zb 55:22; 2Ko 12:​9, 10; 2Ti 4:​16-18; Ebr 13:6

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 19:​1-18—Wakati nabii Eliya anateswa, anamufungulia Yehova moyo wake na Yehova anamutia moyo na kumufariji

    • Mdo 7:​9-15—Ndugu za Yosefu wanamutesa, lakini Yehova anabakia mushikamanifu kwake, anamuokoa, na anamutumikisha juu ya kuokoa familia yake

Kuko aina gani fulani za mateso?

Kusemwa mubaya

2Ny 36:16; Mt 5:11; Mdo 19:9; 1Pe 4:4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Fa 18:​17-35—Rabshake, musemaji wa mufalme wa Ashuru, anamutukana Yehova na anachokoza watu wa Yerusalemu

    • Lu 22:​63-65; 23:​35-37—Watu wenye kumutesa Yesu wanamutukana na kumuchekelea wakati iko mwenye kufungwa na wakati iko ku muti wa mateso

Kupingwa na watu wa familia

Kufungwa na kupelekwa mbele ya wenye mamlaka

Kutendewa kwa jeuri

Kushambuliwa na kikundi ya watu

Kuuawa

Wakristo wanapaswa kujiendesha namna gani wakati wanapata mateso?

Mt 5:44; Mdo 16:25; 1Ko 4:​12, 13; 1Pe 2:23

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 7:57–8:1—Kikundi ya watu inakaribia kumuua mwanafunzi Stefano, lakini anamuomba Mungu awaonyeshe rehema wale wenye kumutesa, kutia ndani Sauli wa Tarso

    • Mdo 16:​22-34—Hata kama mutume Paulo amepigwa na kutiwa mu mikatale, anatendea mulinzi wa gereza kwa fazili, na ile inafanya ule mulinzi na watu wote wa nyumba yake wafikie kuwa waamini

Nini njo ilifikia Wakristo fulani wa karne ya kwanza?

Tunapaswa kuwa na mawazo gani juu ya mateso?

Namna gani tumaini yetu inatusaidia tukuwe na nguvu ya kuvumilia wakati tunateswa?

Juu ya nini hatupaswe kuacha mateso itufanye tusikie haya, tuogope, ao tuvunjike moyo, na juu ya nini hatupendi kuacha kumutumikia Yehova?

Zb 56:​1-4; Mdo 4:​18-20; 2Ti 1:​8, 12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Ny 32:​1-22—Wakati jeshi kubwa ya Mufalme Senakeribu inamuogopesha Mufalme Hezekia, Hezekia anamutegemea Yehova na anatia nguvu watu wake; Yehova anamubariki sana juu ya ile

    • Ebr 12:​1-3—Watu wenye kumutesa Yesu wanatafuta kumupatisha haya, lakini Yesu haangaikie ile na haache ile imuvunje moyo hata kidogo

Mateso inaweza kuleta mambo gani ya muzuri?

Uvumilivu wetu unamufurahisha Yehova na unaletea jina yake heshima

1Pe 2:​19, 20; 4:​12-16

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yob 1:​6-22; 2:​1-10—Hata kama hajue kama Shetani njo iko namuletea mateso, Yobu anakatala kumuacha Yehova, na ile inatukuza Mungu na kuonyesha kama Shetani ni muongo

    • Da 1:​6, 7; 3:​8-30—Hanania, Mishaeli, na Azaria (Shadraki, Meshaki, na Abednego) wako tayari kufa kifo ya mateso kuliko kumukosea Yehova; ile inafanya mufalme mupagani Nebukadneza amutukuze Yehova mbele ya watu

Mateso inaweza kutupatia nafasi ya kutoa ushahidi

Lu 21:​12, 13; Mdo 8:​1, 4

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 11:​19-21—Wakristo wametawanyika juu ya mateso, lakini wanaendelea kutangaza habari njema mu miji mingi

    • Flp 1:​12, 13—Mutume Paulo anafurahi juu kifungo yake inamupatia nafasi ya kutangaza habari njema

Wakati tunavumilia mateso ile inaweza kutia nguvu waamini wenzetu

Mara mingi, nani njo wanatesaka watumishi waaminifu wa Yehova?

Yer 26:11; Mk 3:6; Yoh 11:​47, 48, 53; Mdo 25:​1-3

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 19:​24-29—Mu Efeso, wale wenye wako natengeneza vihekalu vya Artemi wanatesa Wakristo juu wanaogopa ujumbe wa Wakristo usifanye watu wakose kuuza vitu vyao

    • Gal 1:​13, 14—Juu anapenda sana dini ya Wayahudi, mbele akuwe Mukristo, Paulo (Sauli) anatesa kutaniko

Nani njo iko nafanya watu wa Mungu wateseke?