Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Sala

Sala

Tunajuaje kwamba Yehova anasikiliza na kujibu sala?

Zb 65:2; 145:18; 1Yo 5:14

Tazama pia Zb 66:19; Mdo 10:31; Ebr 5:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 18:​36-38—Yehova anajibu mara moja sala ya nabii Eliya kwenye Mlima Karmeli anapokabiliana na manabii wa Baali

    • Mt 7:​7-11—Yesu anatutia moyo tuendelee kusali na anatuhakikishia kwamba Yehova, akiwa Baba mwenye upendo, anatusikiliza

Wakristo wanapaswa kusali kwa nani tu?

Tunapaswa kusali kupitia kwa nani?

Yehova anasikiliza sala za nani?

Yehova hasikilizi sala za nani?

Met 15:29; 28:9; Isa 1:15; Mik 3:4; Yak 4:3; 1Pe 3:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yos 24:​9, 10—Yehova anakataa kusikiliza sala ya Balaamu kwa sababu anasali kinyume na mapenzi ya Mungu

    • Isa 1:​15-17—Kwa kuwa watu wake wamekuwa wanafiki na wana hatia ya damu, Yehova anakataa kusikiliza sala zao

Ni neno gani ambalo sikuzote tunasema mwishoni mwa sala, na kwa nini?

Je, Biblia inasema kwamba tunapaswa kuwa katika mkao fulani hususa tunaposali?

Ni baadhi ya mambo gani ambayo watumishi wa Yehova wanaweza kutaja kwenye sala wanapokutana kwa ajili ya ibada?

Mdo 4:​23, 24; 12:5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Nya 29:​10-19—Mfalme Daudi anaongoza kutaniko la Israeli katika sala wakati michango ya hiari ya watu kwa ajili ya hekalu inapokusanywa

    • Mdo 1:​12-14—Mitume, ndugu za Yesu, Maria mama ya Yesu, na baadhi ya wanawake waaminifu wapo katika chumba cha juu jijini Yerusalemu wakisali pamoja

Kwa nini mtu anayesali hapaswi kamwe kujikweza au kujitafutia sifa?

Kwa nini inafaa kusali kabla ya kula?

Kwa nini tunapaswa kuendelea kusali kwa Yehova, Baba yetu wa mbinguni, bila kuacha?

Ro 12:12; Efe 6:18; 1Th 5:17; 1Pe 4:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Da 6:​6-10—Hata baada ya tishio la kuuawa, nabii Danieli anaendelea na zoea lake la kusali kwa Yehova waziwazi

    • Lu 18:​1-8—Yesu anatumia mfano wa mwamuzi asiye mwadilifu ambaye aliamua kumsaidia mwanamke aliyeendelea kumwomba amtendee kwa haki, kuonyesha kwamba Baba yetu mwadilifu atajibu bila kukawia sala za watumishi wake wanaoendelea kumwomba msaada

Tunapaswa kuwa na mtazamo gani ikiwa tunataka Mungu asikilize sala zetu za kumwomba msamaha?

2Nya 7:​13, 14

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Fa 22:​11-13, 18-20—Kwa kuwa Mfalme Yosia anajinyenyekeza na kujitahidi kumfurahisha Yehova, anatendewa kwa rehema na fadhili nyingi

    • 2Nya 33:​10-13—Mfalme Manase anasali kwa unyenyekevu, jambo linalofanya apate msamaha wa Yehova na kurudishiwa ufalme wake

Yehova anataka tufanye nini ikiwa tunataka atusamehe?

Kwa nini tunapaswa kutaja kwenye sala zetu kwamba tunaunga mkono kutendeka kwa mapenzi ya Mungu?

Kwa nini sala zetu zinapaswa kuonyesha kwamba tuna imani katika Baba yetu wa mbinguni?

Tunaweza kusali kuhusu mambo gani yanayofaa?

Kutakaswa kwa jina la Mungu

Kuja kwa Ufalme wa Mungu ili utawale dunia yote

Kutimizwa kwa mapenzi ya Yehova

Kuomba mahitaji yetu ya kimwili

Kuomba msamaha wa dhambi zetu

Kuomba ulinzi dhidi ya majaribu

Kushukuru

Kuomba kujua mapenzi ya Mungu, kupata uelewaji, na hekima

Met 2:​3-6; Flp 1:9; Yak 1:5

Tazama pia Zb 119:34

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • 1Fa 3:​11, 12—Yehova anafurahishwa na ombi la Mfalme Sulemani la kutaka apate hekima, na Yehova anampatia hekima nyingi sana

Kuomba roho takatifu

Kusali kwa niaba ya waabudu wenzetu, kutia ndani wale wanaokabili mateso

Kumsifu Yehova

Zb 86:12; Isa 25:1; Da 2:23

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 10:21—Yesu anamsifu Baba yake hadharani kwa kuwafunulia kweli ya kiroho watu wanyenyekevu ambao ni kama watoto

    • Ufu 4:​9-11—Familia ya Yehova ya mbinguni inampa heshima na utukufu anaostahili

Kuomba watu wenye mamlaka wachochewe kuturuhusu tumwabudu Yehova kwa amani na kuwahubiria watu

Je, inafaa kusali tunapobatizwa?

Je, inafaa kusali kwa niaba ya watu walio wagonjwa kiroho?

Kwa nini kwa kawaida wanaume hawafuniki vichwa vyao wanaposali, na kwa nini wakati fulani wanawake wanafunika vichwa vyao wanaposali?

Ni jambo gani lililo muhimu zaidi kuliko urefu wa sala au hisia tunazoonyesha tunaposali?

Omb 3:41; Mt 6:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 18:​25-29, 36-39—Eliya alipokuwa akikabiliana na manabii wa Baali, walilia kwa mungu wao kwa saa nyingi—lakini hawakujibiwa

    • Mdo 19:​32-41—Waabudu sanamu jijini Efeso wanampaazia sauti mungu wa kike Artemi kwa saa mbili, lakini hawakutimiza jambo lolote, bali wanakemewa na karani wa jiji