Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Sala

Sala

Tunajua namna gani kama Yehova anasikiaka na kujibia sala?

Zb 65:2; 145:18; 1Yo 5:14

Ona pia Zb 66:19; Mdo 10:31; Ebr 5:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 18:​36-38—Yehova anajibia sala ya nabii Eliya ku Mulima Karmeli wakati iko nashindana na manabii wa Baali

    • Mt 7:​7-11—Yesu anatutia moyo tudumu katika sala na anatuhakikishia kama Yehova atatusikia juu yeye ni Baba mwenye upendo

Ni kwa nani tu njo Wakristo wanapaswa kusali?

Tunapaswa kusali mu jina ya nani?

Yehova anasikilizaka sala ya watu wa namna gani?

Yehova hasikilizake sala ya watu wa namna gani?

Mez 15:29; 28:9; Isa 1:15; Mik 3:4; Yak 4:3; 1Pe 3:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yos 24:​9, 10—Yehova anakatala kumusikiliza Balaamu juu mambo yenye anaomba iko tofauti na mapenzi ya Mungu

    • Isa 1:​15-17—Yehova anakatala kusikiliza sala ya watu wake juu wamekuwa wanafiki na wako na hatia ya damu

Tunapaswa kusema nini ku mwisho wa sala zetu, na juu ya nini?

Biblia inasema kama kila mara tunapaswa kuikala ao kusimama ao kuwa mu hali ingine juu ya kusali?

Watumishi wa Yehova wanaweza kusali juu ya mambo gani wakati wanakusanyika pamoya?

Mdo 4:​23, 24; 12:5

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Ny 29:​10-19—Mufalme Daudi anawakilisha kutaniko ya Israeli mu sala wakati watu wanatoa michango kwa ajili ya hekalu

    • Mdo 1:​12-14—Mitume, ndugu za Yesu, Maria mama ya Yesu, na wanamuke wengine waaminifu wako nasali pamoya mu chumba ya juu Yerusalemu

Juu ya nini mutu mwenye kuwakilisha wengine mu sala anapaswa kuepuka kujisifu na kufanya watu wamukazie uangalifu?

Ni muzuri kusali mbele ya kula?

Juu ya nini hatupaswe hata kidogo kuzarau pendeleo yenye tuko nayo ya kusali kwa Baba yetu wa mbinguni?

Ro 12:12; Efe 6:18; 1Te 5:17; 1Pe 4:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Da 6:​6-10—Hata kama wanamuogopesha kuwa ikiwa anasali watamuua, Danieli anaendelea kusali kama kawaida

    • Lu 18:​1-8—Yesu anatumia mufano wa muamuzi mwenye hamuogope Mungu mwenye anasaidia mwanamuke mwenye alikuwa namuomba bila kuacha; anazungumuzia ile mufano juu ya kuonyesha kama Baba yetu wa mbinguni atajibia watumishi wake wenye wako nalilia musaada kwake bila kuacha

Tunapaswa kuwa na mutazamo gani kama tunapenda Mungu asikie sala yetu ya kumuomba musamaha?

2Ny 7:​13, 14

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Fa 22:​11-13, 18-20—Juu Mufalme Yosia anajinyenyekeza na anajikaza kumufurahisha Yehova, anatendewa kwa rehema nyingi na kwa fazili

    • 2Ny 33:​10-13—Juu Mufalme Manase anasali kwa unyenyekevu, Yehova anamusamehe na anamurudishia ufalme wake

Tunapaswa kufanya nini kama tunapenda Yehova asamehe zambi zetu?

Juu ya nini tunapaswa kuonyesha kama tunategemeza mapenzi ya Yehova mu sala zetu?

Juu ya nini sala zetu zinapaswa kuonyesha kama tunatumainia Baba yetu wa mbinguni?

Tunaweza kusali juu ya mambo gani?

Kutakaswa kwa jina ya Mungu

Kuya kwa Ufalme juu ya kutawala dunia yote

Kutimizwa kwa mapenzi ya Mungu

Mahitaji yetu ya kimwili

Musamaha wa zambi zetu

Kutulinda na vishawishi

Kushukuru

Ujuzi wa mapenzi ya Mungu, uelewaji, na hekima

Mez 2:​3-6; Flp 1:9; Yak 1:5

Ona pia Zb 119:34

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • 1Fa 3:​11, 12—Yehova anafurahi juu Mufalme Sulemani anamuomba hekima, na anamupatia ayo kwa uwingi

Roho takatifu

Kusali juu ya waabudu wenzetu, kutia ndani wale wenye wako napata mateso

Maneno ya kumusifu Mungu

Zb 86:12; Isa 25:1; Da 2:23

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Lu 10:21—Yesu anamusifu Baba yake mbele ya watu juu anafunua kweli kwa watu wenye kuwa wanyenyekevu sawa watoto

    • Ufu 4:​9-11—Familia ya Yehova ya mbinguni inamupatia Yehova heshima na utukufu wenye anastahili

Kusali juu wenye mamlaka watuache tumuabudu Yehova na tuhubirie watu kwa amani

Ni muzuri kusali wakati ya ubatizo yetu?

Ni muzuri kusali kwa ajili ya watu wenye wako na matatizo ya kiroho?

Juu ya nini wanaume wanakuwaka nasali kichwa wazi, na juu ya nini wakati fulani wanamuke wanajifungaka kitambala juu ya kusali?

Wakati mutu iko nasali, nini njo ya maana zaidi kushinda hata urefu na hisia zenye anatia mu sala?

Omb 3:41; Mt 6:7

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 1Fa 18:​25-29, 36-39—Wakati nabii Eliya anajaribu manabii wa Baali, wanalilia mungu wao kwa wakati murefu lakini hawapate jibu yoyote

    • Mdo 19:​32-41—Waabudu-sanamu wa Efeso wanamulalamikia mungu mwanamuke Artemi kwa saa mbili, lakini hakuna jambo yenye inatokea na ofisa wa muji anawakataza kufanya makelele