Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kuhubiri Habari Njema

Kuhubiri Habari Njema

Kwa nini Wakristo wote wa kweli wanafanya tangazo la hadharani la imani yao?

Yesu alituwekea mfano gani katika kazi ya kuhubiri?

Lu 8:1; Yoh 18:37

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Lu 4:​42-44—Yesu anasema kwamba alitumwa duniani kuhubiri

    • Yoh 4:​31-34—Yesu anasema kwamba kazi yake ya kuhubiri habari njema ni kama chakula kwake

Je, wanaume wanaoongoza katika kutaniko ndio tu wenye jukumu la kuhubiri habari njema?

Zb 68:11; 148:​12, 13; Mdo 2:​17, 18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Fa 5:​1-4, 13, 14, 17—Msichana Mwisraeli anamweleza mke wa bwana wake Msiria kumhusu Elisha, nabii wa Yehova

    • Mt 21:​15, 16—Yesu anapinga maneno ya wakuu wa makuhani na waandishi, wanaowasema vibaya wavulana wanaomsifu Yesu hekaluni

Waangalizi kutanikoni wanawezaje kuwafundisha wengine kuhubiri habari njema?

Yehova na Yesu wanatusaidiaje kutimiza kazi yetu ya kuhubiri?

2Ko 4:7; Flp 4:13; 2Ti 4:17

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mdo 16:​12, 22-24; 1Th 2:​1, 2—Ingawa mtume Paulo na waandamani wake wanatendewa vibaya, kwa msaada wa Mungu wanaendelea kuhubiri kwa ujasiri

    • 2Ko 12:​7-9—Mtume Paulo, mhubiri mwenye bidii, anasumbuliwa na “mwiba katika mwili,” huenda ni tatizo la afya; hata hivyo, Yehova anampa nguvu za kuendelea na kazi ya kuhubiri

Ni nani au ni nini kinachofanya Mkristo astahili kuhubiri?

1Ko 1:​26-28; 2Ko 3:5; 4:13

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yoh 7:15—Watu wanastaajabu kwamba Yesu ana ujuzi mwingi ingawa hakusoma kwenye shule za marabi

    • Mdo 4:13—Mitume wa Yesu wanaonwa kuwa watu wasio na elimu na wa kawaida; hata hivyo, wanahubiri kwa bidii na ujasiri

Tunajuaje kwamba Yehova anataka tuwazoeze wengine katika kazi ya kuhubiri na kufundisha?

Mk 1:17; Lu 8:1; Efe 4:​11, 12

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Isa 50:​4, 5—Kabla ya kuwa mwanadamu, Masihi alipata mazoezi ya kibinafsi kutoka kwa Yehova Mungu

    • Mt 10:​5-7—Akiwa duniani, kwa subira Yesu anawazoeza wanafunzi wake wafanye kazi ya kuhubiri

Tunapaswa kuuonaje mgawo wetu wa kuhubiri habari njema?

Mkristo anahisije anaposhiriki katika kazi ya kuhubiri?

Ni ujumbe gani tunaotangaza tunapohubiri?

Kwa nini Wakristo hufunua mafundisho ya uwongo?

2Ko 10:​4, 5

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mk 12:​18-27—Yesu anajadiliana na Masadukayo kwa kutumia Maandiko ili kuwathibitishia kwamba wana maoni yasiyo sahihi kuhusu ufufuo

    • Mdo 17:​16, 17, 29, 30—Mtume Paulo anajadiliana na Waathene ili kuwaonyesha kwamba ibada ya sanamu ni kosa

Kazi ya kuhubiri inafanywaje?

Tuna msingi gani wa kuhubiri hadharani?

Ni nini kinachoonyesha kwamba tunahitaji kuwa na subira na uvumilivu katika huduma yetu?

Kazi yetu ya kuhubiri ina matokeo gani mazuri?

Kwa nini inafaa kuwa tayari kutumia kila fursa tunayopata ya kuhubiri?

1Ko 9:23; 1Ti 2:4; 1Pe 3:15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yoh 4:​6, 7, 13, 14—Ingawa amechoka, Yesu anamhubiria habari njema mwanamke Msamaria katika kisima

    • Flp 1:​12-14—Hata alipokuwa gerezani, mtume Paulo alitumia kila fursa aliyopata kutoa ushahidi na kuwatia moyo wengine

Je, tunapaswa kutarajia kwamba kila mtu atasikiliza ujumbe wetu?

Yoh 10:​25, 26; 15:​18-20; Mdo 28:​23-28

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yer 7:​23-26—Kupitia Yeremia, Yehova anafafanua jinsi watu Wake wanavyorudia tena na tena kutowasikiliza manabii Wake

    • Mt 13:​10-16—Yesu anafafanua kwamba kama katika siku za Isaya, wengi watasikia ujumbe lakini wataukataa

Kwa nini hatushangai kwamba watu wengi hawatusikilizi kwa sababu wana shughuli nyingi?

Ni nini kinachoonyesha kwamba baadhi ya watu mwanzoni watasikiliza lakini hawataendelea?

Ni mifano gani inayoweza kutusaidia tusishangae baadhi ya watu wanapopinga moja kwa moja kazi yetu ya kuhubiri?

Tunaitikiaje tunapokabili upinzani katika kazi yetu ya kuhubiri?

Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba baadhi ya watu watakubali habari njema?

Wahubiri wa habari njema wana wajibu gani mzito mbele za Mungu?

Kwa nini tunapaswa kuwahubiria watu wote haidhuru dini, rangi, au taifa lao?

Je, inafaa kuhubiri siku yoyote katika juma, kutia ndani siku ya Sabato?

Ni mifano gani inayoonyesha kwamba inafaa kuwahubiria watu wote, hata ikiwa wana Biblia na ni washiriki wa dini fulani?