Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuhubiri Habari Njema

Kuhubiri Habari Njema

Juu ya nini Wakristo wanakuwaka natangaza imani yao mbele ya watu wote?

Yesu alituwekea mufano gani kuhusu kazi ya kuhubiri?

Lu 8:1; Yoh 18:37

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Lu 4:​42-44—Yesu anasema kama alitumwa ku dunia juu ya kuhubiri

    • Yoh 4:​31-34—Yesu anasema kama kazi ya kuhubiri iko sawa vile chakula kwake

Ni wale wenye wako na madaraka mu kutaniko njo tu wanapaswa kuhubiri habari njema?

Zb 68:11; 148:​12, 13; Mdo 2:​17, 18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • 2Fa 5:​1-4, 13, 14, 17—Kijana mwanamuke Mwisraeli anaambia bibi ya Naamani kuhusu Elisha, nabii wa Yehova

    • Mt 21:​15, 16—Yesu anapinga mawazo ya wakubwa wa makuhani na waandishi wenye wanakatala vijana wanaume wamusifu Yesu mu hekalu

Waangalizi Wakristo wanakuwaka na daraka gani kuhusu kuhubiri habari njema na kufundisha wengine?

Namna gani Yehova na Yesu wanatusaidiaka tuhubiri?

2Ko 4:7; Flp 4:13; 2Ti 4:17

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mdo 16:​12, 22-24; 1Te 2:​1, 2—Hata kama Paulo na wenzake wanatendewa mubaya, kwa musaada wa Mungu wanaendelea kuhubiri habari njema bila kuogopa

    • 2Ko 12:​7-9—Mutume Paulo, muhubiri mwenye hachokake, anateseka juu ya “mwiba katika mwili,” pengine ilikuwa tatizo fulani ya afya; lakini Yehova anamupatia nguvu ya kuendelea kuhubiri

Nini ao nani njo anapatiaka Mukristo mamlaka ya kuhubiri?

1Ko 1:​26-28; 2Ko 3:5; 4:13

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yoh 7:15—Wanaume wa wakati wa Yesu wanashangaa kuona kama Yesu iko na ujuzi sana hata kama hakusomaka ku masomo ya warabi

    • Mdo 4:13—Mitume wa Yesu wanaonwa kuwa watu wa kawaida; lakini, wako na bidii na wanahubiri bila woga

Tunajua namna gani kama Yehova anapenda tuzoeze wengine mu kazi ya kuhubiri na ya kufundisha?

Mk 1:17; Lu 8:1; Efe 4:​11, 12

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Isa 50:​4, 5—Mbele akuye ku dunia, Yesu alizoezwa na Yehova

    • Mt 10:​5-7—Wakati alikuwa ku dunia, kwa uvumilivu, Yesu alizoeza wanafunzi wake mu kazi ya kuhubiri

Tunapaswa kuona namna gani daraka yenye tuko nayo ya kuhubiri habari njema?

Tunajisikiaka namna gani wakati tunahubiri habari njema?

Tunazungumuziaka mambo gani wakati tunahubiri habari njema?

Juu ya nini Wakristo wanaonyeshaka wazi mafundisho ya uongo?

2Ko 10:​4, 5

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mk 12:​18-27—Yesu anafikiri na Wasadukayo kwa kutumia Maandiko juu ya kuwaonyesha kama mawazo yao kuhusu ufufuo haiko sawa

    • Mdo 17:​16, 17, 29, 30—Mutume Paulo anafikiri na watu wa Atene juu ya kuwaonyesha kama kuabudu sanamu ni kosa

Kazi ya kuhubiri inafanyiwaka namna gani?

Juu ya nini tunahubiriaka mahali pa watu wengi?

Nini njo inaonyesha kama inaomba tukuwe na uvumilivu na bidii mu kazi ya kuhubiri?

Tunapataka matokeo gani ya muzuri mu kazi ya kuhubiri?

Juu ya nini ni muzuri kuhubiri kila mara wakati tunapata nafasi?

1Ko 9:23; 1Ti 2:4; 1Pe 3:15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yoh 4:​6, 7, 13, 14—Hata kama amechoka, Yesu anahubiria mwanamuke Musamaria habari njema ku kisima

    • Flp 1:​12-14—Hata kama iko mwenye kufungwa, mutume Paulo anatumia nafasi zenye iko nazo juu ya kuhubiri na kutia wengine moyo

Tunapaswa kutazamia kama watu wote watasikiliza ujumbe wetu?

Yoh 10:​25, 26; 15:​18-20; Mdo 28:​23-28

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yer 7:​23-26—Kupitia Yeremia, Yehova anafasiria namna mara mingi watu wake walikosa kusikiliza manabii

    • Mt 13:​10-16—Yesu anasema kama sawa vile mu siku za Isaya, watu wengi watasikiliza ujumbe lakini hawatabadilika

Juu ya nini hatushangae kuona kama watu wengi hawatusikilize juu wako na mambo mingi ya kufanya?

Nini njo inaonyesha kama watu fulani watasikiliza na kubadilika ku mwanzo lakini kisha hawataendelea?

Ni mifano gani inatusaidia tusishangae wakati watu wanatupinga mu mahubiri?

Tunatendaka namna gani wakati watu wanatupinga mu mahubiri?

Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama watu fulani watakubali habari njema?

Wahubiri wa habari njema wako na daraka gani nzito mbele ya Mungu?

Juu ya nini tunapaswa kuhubiria watu wa dini zote, rangi zote, na inchi zote?

Ni muzuri kuhubiri siku yoyote mu juma, kutia ndani siku ya Sabato?

Ni mifano gani inaonyesha kama ni muzuri kuhubiria watu, hata kama wako na Biblia na wako mu dini fulani?