Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Kusuluhisha Hali ya Kutoelewana

Kusuluhisha Hali ya Kutoelewana

Mtu anapotukosea, kwa nini tunapaswa kuepuka kukasirika au kulipiza kisasi?

Met 20:22; 24:29; Ro 12:​17, 18; Yak 1:​19, 20; 1Pe 3:​8, 9

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 25:​9-13, 23-35—Nabali anapomtukana Daudi na wanaume wake na kukataa kuwasaidia, Daudi anafanya maamuzi ya haraka-haraka ya kutaka kumuua Nabali na wanaume katika nyumba yake, lakini ushauri wenye hekima wa Abigaili unamsaidia Daudi kuepuka hatia ya damu

    • Met 24:​17-20—Akiongozwa na roho, Mfalme Sulemani anawaonya watu wa Mungu kwamba kushangilia maadui wetu wanapoteseka ni jambo lisilomfurahisha Yehova; tunaacha kazi ya kuhukumu mikononi mwa Yehova

Ikiwa Mkristo amekosana na mtu, je, anapaswa kuepuka kuzungumza naye au kumwekea kinyongo?

Law 19:​17, 18; 1Ko 13:​4, 5; Efe 4:26

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mt 5:​23, 24—Yesu anaeleza kwamba tunapaswa kujitahidi sana kufanya amani pamoja na ndugu ambaye ana jambo fulani dhidi yetu

Tunapaswa kuchukua hatua gani yenye upendo tunapokosewa?

Kwa nini tunapaswa kuwasamehe hata wale ambao wametutendea dhambi tena na tena ikiwa wanatubu kutoka moyoni?

Ikiwa kosa ni zito sana hivi kwamba hatuwezi kuliachilia—kwa mfano, katika visa vya uchongezi au ulaghai—ni nani anayepaswa kuzungumza na mkosaji, na akiwa na lengo gani?

Mt 18:15

Tazama pia Yak 5:20

Tunapaswa kufanya nini ikiwa mtu ambaye ametulaghai au kutuchongea anakataa kutubu tunapozungumza naye tukiwa wawili?