Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Dhambi

Dhambi

Dhambi ni nini, na kwa nini inatuathiri sisi sote?

Biblia inatuhakikishiaje kwamba tunaweza kushinda mielekeo yetu ya dhambi?

Ro 6:​12-14

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 2Sa 11:​2-5, 14, 15, 26, 27; 12:​1-13 —Mfalme Daudi anatenda dhambi nzito sana, anapata nidhamu kali, na anajitahidi sana kurekebisha njia zake

    • Ro 7:​15-24—Mtume Paulo, ambaye ni mfano bora wa mtu mwenye imani yenye nguvu na anayemtumikia Mungu kwa bidii, anaeleza jinsi anavyopambana na mwelekeo wake mwenyewe wa dhambi

Kutojua na kupotoshwa kumewaongozaje watu wengi kwenye dhambi?

Kwa nini zoea la kufanya dhambi kimakusudi ni jambo zito sana?

Huenda Shetani akatumia nini ili kuwashawishi watumishi wa Mungu watende dhambi?

Met 1:​10, 11, 15; Mt 5:28; Yak 1:​14, 15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 3:​1-6—Akizungumza kupitia nyoka, Shetani anamjaribu Hawa kwa kuchochea tamaa mbaya ya ubinafsi na kudhoofisha uhakika wake katika Yehova

    • Met 7:​6-10, 21-23—Mfalme Sulemani anaeleza jinsi mwanamume kijana asiye na busara anavyoshawishiwa na mwanamke mwenye maadili mapotovu

Tunawezaje kupinga vishawishi vya Shetani?

Efe 4:27; 6:​10-18; Yak 4:​7, 8

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Met 5:​1-14—Kama baba anavyozungumza na mwana wake, Mfalme Sulemani anatoa ushauri ulioongozwa na roho kuhusu kwa nini na kwa njia gani tunaweza kuepuka kishawishi cha kufanya uasherati

    • Mt 4:​1-11—Yesu anatuwekea kielelezo kikamilifu cha kupinga vishawishi vya Shetani vyenye ujanja kwa kutegemea Neno la Mungu

Baadhi ya mifano ya dhambi nzito ambazo Mkristo anapaswa kuepuka

Tazama “Mazoea Yasiyofaa

Kuungama dhambi

Kwa nini hatupaswi kujaribu kuficha dhambi zetu?

Tunapaswa kuungama dhambi zetu zote kwa nani?

Ni nani anayetenda kama “msaidizi” kwa kututetea mbele za Yehova?

Je, mtenda dhambi anaweza kuonyesha toba kupitia matendo yake?

Mdo 26:20; Yak 4:​8-10

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Kut 22:​1-12—Chini ya Sheria ya Musa, mwizi anapaswa kuwalipa wale aliowaibia

    • Lu 19:​8, 9—Zakayo, mkuu wa wakusanya kodi, anaonyesha toba kwa kubadili njia zake na kwa kuwarudishia pesa wale aliowadhulumu

    • Tazama pia “Toba

Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika na msamaha wa Yehova?

Tazama “Kusamehe

Yehova ameandaa mpango gani unaotoa msaada na kulilinda kutaniko mtu anapofanya dhambi nzito?

Dhambi nzito inaweza kuwaathirije wengine katika familia au kutanikoni?

Ebr 12:​15, 16

Tazama pia Kum 29:18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Yos 7:​1-13, 20-26—Akani anawaletea msiba Waisraeli wote kwa kufanya dhambi nzito na kujaribu kuificha

    • Yon 1:​1-16—Kwa sababu anamwasi Yehova, nabii Yona anahatarisha uhai wa watu walio katika meli pamoja naye

    • 1Ko 5:​1-7—Mtume Paulo anafunua kisa cha dhambi nzito huko Korintho, inayolidhuru kutaniko lote

Kwa nini woga wa kutiwa nidhamu haupaswi kamwe kutuzuia kutafuta msaada wa wazee?

Kwa nini tunapaswa kukubali msamaha wa Mungu badala ya kuendelea kuhuzunika kwa sababu ya makosa tuliyofanya wakati uliopita?

Tazama “Kusamehe

Ikiwa tunajua kwamba mtu fulani amefanya dhambi nzito, kwa nini tunapaswa kuhakikisha kwamba mtenda dhambi anaenda kuwajulisha wazee wa kutaniko?

Law 5:1

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Kum 13:​6-9; 21:​18-20—Sheria ya Musa inamtaka mtu atoe ripoti ya dhambi nzito iliyofanywa hata na mtu wa familia au mpendwa wake