Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Zambi

Zambi

Zambi njo nini, na juu ya nini siye wote tunafanyaka zambi?

Namna gani Biblia inatuhakikishia kama tunaweza kupiganisha nia yetu ya kufanya zambi?

Ro 6:​12-14

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

Namna gani kutokujua na kudanganywa kunafanyaka watu wengi wafanye zambi?

Juu ya nini kuzoea kutenda zambi kimakusudi ni mubaya sana?

Shetani anatumikishaka nini juu ya kujaribu kufanya watu wa Mungu watende zambi?

Mez 1:​10, 11, 15; Mt 5:28; Yak 1:​14, 15

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mwa 3:​1-6—Kupitia nyoka, Shetani anachochea tamaa ya Eva na anamufanya asimutumainie Yehova kabisa

    • Mez 7:​6-10, 21-23—Mufalme Sulemani anafasiria namna kijana moya mwenye anakosa akili ya muzuri anaanguka mu kishawishi ya mwanamuke muasherati

Namna gani tunaweza kupinga vishawishi vya Shetani?

Efe 4:27; 6:​10-18; Yak 4:​7, 8

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Mez 5:​1-14—Mufalme Sulemani anatoa mashauri kuhusu namna na sababu ya kuepuka uasherati

    • Mt 4:​1-11—Yesu anatuwekea mufano muzuri wa kushinda vishawishi vya Shetani kwa kutumia Neno ya Mungu

Ni zambi gani fulani zenye kuwa nzito zenye Wakristo wanapaswa kuepuka?

Ona “Matendo ya mubaya

Kuungama zambi

Juu ya nini hatupaswe kujaribu kuficha zambi zetu?

Ni kwa nani njo tunapaswa kutubu zambi zote?

Ni nani njo “musaidizi” mwenye anatuombeaka kwa Yehova?

Mutenda-zambi anaweza kuonyesha kama anatubu kupitia matendo yake?

Mdo 26:20; Yak 4:​8-10

Ona pia “Kutubu

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Kut 22:​1-12—Chini ya Sheria ya Musa, mwizi anaombwa arudishe vitu vyenye aliiba

    • Lu 19:​8, 9—Zakayo, mukubwa wa wakusanya-kodi, anaonyesha kama ametubu kwa kubadilisha matendo yake na kurudisha vitu vyenye alinyanganya

Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yehova anakuwaka nasamehe?

Ona “Musamaha

Yehova ameweka mupango gani juu ya kusaidia na kulinda kutaniko wakati mutu fulani anafanya zambi nzito?

Zambi nzito inaweza kuwa na matokeo gani juu ya wengine mu familia ao mu kutaniko?

Ebr 12:​15, 16

Ona pia Kum 29:18

  • Habari za Biblia zenye zinaweza kusaidia:

    • Yos 7:​1-13, 20-26—Akani anafanya Waisraeli wote wateseke kwa kufanya zambi nzito na kujaribu kuificha

    • Yon 1:​1-16—Juu anamuasi Yehova, Yona anatia mu hatari uzima wa wote wenye iko nao mu mashua

    • 1Ko 5:​1-7—Mutume Paulo anaonyesha kisa ya zambi nzito sana yenye inachafua kutaniko yote ya Korinto

Juu ya nini hatupaswe kukosa kutafuta musaada wa wazee juu tu ya kuogopa kupewa nizamu?

Juu ya nini tunapaswa kuwa hakika kama Yehova ametusamehe kuliko kuendelea kuhuzunika sana juu ya makosa yenye tulifanyaka zamani?

Ona pia “Musamaha

Kama tunajua kuwa mutu fulani alifanya zambi nzito, juu ya nini tunapaswa kuhakikisha kama ule mutenda-zambi amejulisha wazee ile zambi?

Law 5:1

  • Habari ya Biblia yenye inaweza kusaidia:

    • Kum 13:​6-9; 21:​18-20—Sheria ya Musa inasema kama mutu anapaswa kuripoti zambi nzito hata ya mutu wa familia ao mutu mwenye anapendaka sana